Ushawishi wa G7 wapungua kutokana na vitendo vya kinyume na mkondo wa zama

Ushawishi wa G7 wapungua kutokana na vitendo vya kinyume na mkondo wa zama

Yoyo Zhou

Senior Member
Joined
Jun 16, 2020
Posts
126
Reaction score
215
无标题.jpg

Mkutano wa kilele wa G7 umefungwa hivi karibuni huko Puglia nchini Italia. Taarifa iliyotolewa baada ya mkutano huo kwa mara nyingine tena imekashifu China katika masuala mbalimbali bila ya msingi wowote. Kuhusu migogoro kati ya Russia na Ukraine na kati ya Palestina na Israel, msimamo wa kundi hilo pia umelalamikiwa na jamii ya kimataifa.

Kuhusu masuala ya China, kwenye mkutano huo, G7 imeendelea na madai yake yaleyale yaliyotolewa mwaka jana kwenye mkutano wa Hiroshima nchini Japan, na kuipaka matope China katika masuala ya Taiwan, Bahari ya Mashariki, Bahari ya Kusini, Hong Kong, Xinjiang na Tibet. Mwaka huu, suala jipya linaloitwa “uwezo wa uzalishaji wa kupita kiasi” nchini China pia limetajwa. Kwenye taarifa iliyotolewa baada ya mkutano huo, G7 imesisitiza haja ya kubainisha minyororo muhimu ya ugavi ndani ya kundi hilo, ikiilengea China ambayo ni injini kubwa zaidi ya uchumi wa dunia.

Kuhusu mgogoro kati ya Russia na Ukraine, G7 inaiunga mkono kwa nguvu zote Ukraine kuendelea na vita na Russia, lakini kwa upande mwingine, hailaani hata kidogo vitendo vya Israel kwenye Ukanda wa Gaza ambavyo vinakiuka vibaya sheria za kimataifa. Aidha, kuhusu masuala haya mawili, Marekani na nchi wanachama wengine wa G7 pia zina mivutano mingi ya ndani, hali ambayo imeyafanya masuala hayo yawe magumu zaidi.

G7 ilianzishwa mwaka 1976, na wanachama wake ni pamoja na Marekani, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Japan, Italia na Canada. Wakati huo, Pato la Taifa la Marekani lilichukua zaidi ya asilimia 29 ya uchumi wa dunia, kwa pamoja na Ujerumani na Japani, ambazo uchumi wao ulikuwa ukiendelea kwa kasi kubwa, kundi hilo liliwahi kudhibiti sehemu kubwa ya uchumi wa dunia, na kuwa nguvu muhimu ya kiuchumi duniani.

Ikiwa “Klabu ya Nchi Tajiri Zaidi Duniani”, G7 ingeweza kutoa mchango mkubwa katika kutatua matatizo ya kimataifa. Lakini katika miaka ya hivi karibuni, kundi hilo limeshindwa kuchukua hatua halisi za kukuza uchumi wa dunia, wala kuzisaidia nchi zinazoendelea kupata maendeleo. Ripoti iliyotolewa na Shirika la Kimataifa la Kutoa Misaada la Oxfam inakadiria kuwa, G7 imezikopesha nchi za Kusini takriban dola trilioni 13.3 za kimarekani, ikiwa ni pamoja na ahadi za misaada ya maendeleo na misaada ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Katika miaka ya hivi karibuni, uchumi wa G7 imeshuka mwaka hadi mwaka, na umeshindwa na kundi la BRICS ukihesabiwa kwa bei ya ununuzi halisi. Licha ya hayo, hivi sasa mchango wa G7 kwa ukuaji wa uchumi wa dunia ni mdogo kuliko ule uliotolewa na China. Kundi hilo limegeuka kuwa chombo cha nchi za Magharibi kufanya umwamba.
 
Mkutano wa kilele wa G7 umefungwa hivi karibuni huko Puglia nchini Italia. Taarifa iliyotolewa baada ya mkutano huo kwa mara nyingine tena imekashifu China katika masuala mbalimbali bila ya msingi wowote. Kuhusu migogoro kati ya Russia na Ukraine na kati ya Palestina na Israel, msimamo wa kundi hilo pia umelalamikiwa na jamii ya kimataifa.

Kuhusu masuala ya China, kwenye mkutano huo, G7 imeendelea na madai yake yaleyale yaliyotolewa mwaka jana kwenye mkutano wa Hiroshima nchini Japan, na kuipaka matope China katika masuala ya Taiwan, Bahari ya Mashariki, Bahari ya Kusini, Hong Kong, Xinjiang na Tibet. Mwaka huu, suala jipya linaloitwa “uwezo wa uzalishaji wa kupita kiasi” nchini China pia limetajwa. Kwenye taarifa iliyotolewa baada ya mkutano huo, G7 imesisitiza haja ya kubainisha minyororo muhimu ya ugavi ndani ya kundi hilo, ikiilengea China ambayo ni injini kubwa zaidi ya uchumi wa dunia.

Kuhusu mgogoro kati ya Russia na Ukraine, G7 inaiunga mkono kwa nguvu zote Ukraine kuendelea na vita na Russia, lakini kwa upande mwingine, hailaani hata kidogo vitendo vya Israel kwenye Ukanda wa Gaza ambavyo vinakiuka vibaya sheria za kimataifa. Aidha, kuhusu masuala haya mawili, Marekani na nchi wanachama wengine wa G7 pia zina mivutano mingi ya ndani, hali ambayo imeyafanya masuala hayo yawe magumu zaidi.

G7 ilianzishwa mwaka 1976, na wanachama wake ni pamoja na Marekani, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Japan, Italia na Canada. Wakati huo, Pato la Taifa la Marekani lilichukua zaidi ya asilimia 29 ya uchumi wa dunia, kwa pamoja na Ujerumani na Japani, ambazo uchumi wao ulikuwa ukiendelea kwa kasi kubwa, kundi hilo liliwahi kudhibiti sehemu kubwa ya uchumi wa dunia, na kuwa nguvu muhimu ya kiuchumi duniani.

Ikiwa “Klabu ya Nchi Tajiri Zaidi Duniani”, G7 ingeweza kutoa mchango mkubwa katika kutatua matatizo ya kimataifa. Lakini katika miaka ya hivi karibuni, kundi hilo limeshindwa kuchukua hatua halisi za kukuza uchumi wa dunia, wala kuzisaidia nchi zinazoendelea kupata maendeleo. Ripoti iliyotolewa na Shirika la Kimataifa la Kutoa Misaada la Oxfam inakadiria kuwa, G7 imezikopesha nchi za Kusini takriban dola trilioni 13.3 za kimarekani, ikiwa ni pamoja na ahadi za misaada ya maendeleo na misaada ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Katika miaka ya hivi karibuni, uchumi wa G7 imeshuka mwaka hadi mwaka, na umeshindwa na kundi la BRICS ukihesabiwa kwa bei ya ununuzi halisi. Licha ya hayo, hivi sasa mchango wa G7 kwa ukuaji wa uchumi wa dunia ni mdogo kuliko ule uliotolewa na China. Kundi hilo limegeuka kuwa chombo cha nchi za Magharibi kufanya umwamba.
Nilivyosoma tu jina la mtoa mada, nikajua the rest ni ujanja ujanja.
 
Viongozi wengi wapo kwenye nyakati za uchaguzi. Hawana uhakika wa kurejea. Ila G7 ina ushawishi mkubwa. Miaka kadhaa TZ inaweza kuwa kwenye ukanda wa Africa
 
Back
Top Bottom