Ushindi wa Jana na Vipaji nje ya Dar!!

Tabutupu

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2010
Posts
13,206
Reaction score
18,549
Sio vizuri kuwapongeza wafungaji tuu lakini nataka kuweka wazi kwamba kwa muda mwingi vipaji vya mpira vimekuwa vikitafutwa Dar pekee yake toka timu za vijana hadi timu za wakubwa.


Lakini mchezo wa Jana umeonyesha kwamba mikoani kunaweza toa talent nzuri sana kama ilivyo kuwa zama za kina Masafu, Lunyamila etc.

Nchimbi ameibukia Njombe Mji, kabla ya kujiunga na Mbeya city na kisha Police. Bahati nzuri wafungaji wote ni wana ruvuma.

Kama TFF wangecbukua jukumu la kusaka vipaji ndio kipau mbele nadhani tungekuwa taifa linalo tisha kwenye soka hata zaidi ya brazil.

Nafikiri badala ya kuwalipa makocha fedha nyingi ni vyema kuwekeza kwenye utafutaji wa vipaji kwa nchi nzima.

TFF lazima ijue Tanzania ni kubwa na inahitaji ubunifu wa hali ya juu kupata talent zinazo hitajika.

Mapendekezo yangu ni haya.

1. Mashindano ya vijana ya mikoa yaanzie kwenye vitongoji hadi mkoa ili kuunda timu ya mkoa kama ilivyo kwa michezo ya wanafunzi.

2. Michezo ya wanafunzi ipewe kipaumbele hata kwenye ufadhili pamoja na promo kwenye vyombo vya habari. Ni aibu kwamba michezo inaisha lakini hakuna mtu anayejua kuliku na tukio muhimu kama hili japa nchi. Huo ndio muda wa vilabu hata vya nje kuja kutafuta vipaji.


3. Wizara na TFF waunde timu itakayo fanya kazi ya kutambua vipaji nchi nzima hadi kwa wasafwa kule mbeya. Mikoa kuna mijitu yenye talent na nguvu kama nchimbi.


4. TFF ibadilike na kuwadhamini watanzania katika kupata furaha yao katika football.

Picha ni strika machachali wa u20 Simchimba Andrew aliye ondoka na magoli 6 cecafa nyumba kwa goli moja na Kelvin John.

Wote wawili wameitwa kwenye kikosi cha taifa stars.

Asanteni.
 
Naomba nibadilishieni heading kuwe na neno Taifa stars.
 
Wakina Ngasa,Boban na Canavaro walivyotupeleka CHAN 2009 walitokea wapi
 
Wakina Ngasa,Boban na Canavaro walivyotupeleka CHAN 2009 walitokea wapi
Sijui lakini kuna tatizo kubwa sana la utafutaji wa vipaji.

Sijasema.wasitafute dar ila waangalie nchi nzima hadi huku nyaishozi
 
Sijui lakini kuna tatizo kubwa sana la utafutaji wa vipaji.

Sijasema.wasitafute dar ila waangalie nchi nzima hadi huku nyaishozi
Wachezaji wanne tu walioanza jana ndio wazawa wa Dar
 
Marekebisho kidogo Nchimbi hajaibukia Njombe mji bali aliibukia Majimaji fc ya Ruvuma,,,Nchimbi ndie aliyefunga goli la kuipandisha ligi kuu majimaji akiwa na Marcelo Boniventura,,,alivyotoka majimaji akaenda mbeya city akaenda njombe mji,,hapo ndio Azam walipomsajili,,,Polisi Tanzania yupo kwa mkopo akitokea Azam
 
sijaona pointi yako zaidi ya kufagilia ukabila hivi unajua wenyeji halisi wa dar ni wapi kabla ya kuzungumza
Tatizo lako unaonaa ikabila ila kilicho zungimzwa ni kupanua upeo wa kusaka vipaji mikoani sio hadi vijana waje dar
 
Muhimu kocha asing'ang'anie wachezaji wa Simba, Yanga na Azam! Watupie macho timu zote nchini bila kusahau Zenji! Wachezaji wengi walioko Dar mbona wametoka mikoani!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…