Ushindi wa maonyesho ya nanenane

Ushindi wa maonyesho ya nanenane

Umutimbaru

Member
Joined
Jul 22, 2011
Posts
91
Reaction score
5
Maonyesho ya Nanenane ni maonyesho ambayo wakulima huwa wanonyesha mzao yao. Wataalamu wa zana mbalimbali na wafanya biashara kuonyesha zana zitumikazo kurahisishia wakulima hao kupata mazao yaliobora kwa gharama ndogo. Wana JF shida yangu ni namna gani hawa wanaoandaa maonyesho haya na nivigezo gani wanavyovitumia katika kuchaguwa washindi. Ni wakulima gani wagani wanaoshindanishwa. Na mshindi anapopatikana huwa Anakuwa amefundisha nini jamii ya wakulima ambao niwengi wenye uwezo wao ni mdogo na wakati.Mwaka Fulani nilitembelea kiwanja kimoja cha maonyesho na ilikuwa ni siku ya kutangaza Mshindi wa maonyesho ya kilimo cha bustani na kweli aliechaguliwa bustani yake ilipendeza ilikuwa nzuri sana kuliko zote katika uwanja huo, kwani mchicha ilipendeza sana sukuma wiki ilipendeza sana na mazao yote yalioandaliwa yalikuwa mazuri sana yalivutia.Shida ya hawa wanao pima matokeo haya wanazingatia gharama ya kuzalisha hayo mazao. Mkulima wakawaida baada ya kuona mazao haya anafaidika nini? au anajifunza nini?.Kwa mawazo yangu hawa wanaotadhimini ushindi wa hao wataalamu wangelikuwa wanalenga ni njia ipi mkulima wakawaida anaweze kulima kwakuzingati hali halisi ya eneo, upatikanaji wa mahitajio mfano maji, mbolea, mbegu bora na vinginevyo na kupata mazao Kama yao. Likini unakuta Mshindi anatumia gharama kubwa ambayo hata hailingani na zao Hilo likiuzwa katika soko la kawaida.Wana JF Mnaonaje hilo wazo.
 
Mawazo yako ni ya msingi hasa ukizingatia safari hii mshindi alikuwa wizara ya afya. Imagine, wizara kama hii itashindaje maonyesho ya wakulima?
 
Mawazo yako ni ya msingi hasa ukizingatia safari hii mshindi alikuwa wizara ya afya. Imagine, wizara kama hii itashindaje maonyesho ya wakulima?
<br />
<br />
kama imeruhusiwa kushiriki kwanini isipate nafasi sawa ya ushindi kama washiriki? Kama ni makosa basi yameanzia mbali.
 
Ni kweli maonyesho wa wakulima ya itukuwaje ishindanishe hospitali
 
Ni kama mashindano ya urembo. Anayeshinda siyo lazima au kweli kuwa ndiye mzuri kuliko wote katika eneo husika.
 
Wakuu tujiulize Hivi wizara ya Afya inaingiaje kwenye maonyesho ya kilimo? Na c hiyo tu kulikuwa na tume ya Taifa ya kuratibu filamu Tanzania je tume ya kuratibu filamu na kilimo wapi na wapi?

Hapa Arusha kulikuwa na maonyesho kama hayo, ila cha ajabu TASO wameruhusu waachuzi na maonyesho yalijaa mabanda ya Vitu vya kichina kama nguo, vyombo vya ndani na kazalika. na mabanda ya kupromot pombe ndo yalikuwa mengi sana kwenye maonyesho haya pamoja na mabanda ya makampuni ya simu yalikuwa kila kona.

HAYA YANAWEZEKANA KWA TANZANIA TU, NCHI NYINGINE MAONYESHO YA KILIMO NI KILIMO TU
 
Maonyesho ya wakulima yawe yanazingati uhalisia wa eneo. Unapoonyesha kilimo cha mboga na umwagiliaji kwa kutumia zana ambazo hata huyo unaemonyesha hawezi kukimiliki sijui kuna maana ipi ya monyesho. Nashauri waandaji wazingatie uhalisia.
 
lengo limeshapotoshwa zamani saaaaana. huwa naona ni km sehemu ya waandaaji kuiba pesa tu na si kutafuta tija. kila mwaka mashindano sijui maonesho yanafanyika lkn hatuoni faida yake. wizi mtupu!
 
Back
Top Bottom