Pre GE2025 Ushiriki mdogo wa wanawake nafasi za Uongozi CHADEMA unakwamisha juhudi za kufikia usawa wa kijinsia kwenye demokrasia

Pre GE2025 Ushiriki mdogo wa wanawake nafasi za Uongozi CHADEMA unakwamisha juhudi za kufikia usawa wa kijinsia kwenye demokrasia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Joined
Nov 19, 2024
Posts
94
Reaction score
307
Wakuu, kama mnavyojua, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimefanya chaguzi mbalimbali kuanzia ngazi ya Kanda hadi Taifa. Jambo moja lililonivutia kufikiria kwa kina ni ushiriki mdogo wa wanawake katika nafasi za uongozi. Hili ni tatizo linalozidi kuathiri usawa wa kijinsia katika siasa zetu, jambo ambalo linapaswa kujadiliwa na kutafutiwa suluhisho.

Niachane na ngazi ya kanda ambako ni fezea tupu, hali hiyo inaonekana kwa mabaraza ya vyama. Ukiondoa BAWACHA, ambalo kimsingi limeundwa kwa ajili ya wanawake pekee, mabaraza mengine kama BAVICHA na BAZECHA yanaonyesha uwakilishi wa wanawake wa kiwango cha chini mno.

Kupata taarifa na matukio kuelekea uchaguzi mkuu 2025 kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Hii inadhihirika pia kwenye uchaguzi wa jumla wa viongozi wa ngazi za juu, ambapo asilimia 99.9 ya wagombea ni wanaume. Hali hii si tu inaminya fursa kwa wanawake kushiriki kikamilifu katika maamuzi, bali pia inakwamisha juhudi za kufikia usawa wa kijinsia ambao ni sehemu muhimu ya maendeleo ya kidemokrasia.

Soma Pia kwa taarifa zaidi zinazowahusu wanawake kipindi hichi cha uchaguzi: Kipindi hiki cha Uchaguzi wanawake wanapata nafasi ya kutosha kushiriki kwenye masuala ya uchaguzi?

Wakuu, mnadhani nini shida hasa? Na nini kifanyike kupunguza gap hili baina ya wanaume na wanawake?


Chadema.jpg
 
WAPEWE tu upendeleo wa kugombea nafasi nyeti kama hizo kwakua ni Wanawake?.

Walazimishwe tu kugombea ili kufikia Usawa wa Jinsia?.

Hatupaswi kua kizazi Cha kuchagua Viongozi Kwa sababu tu ya Jinsia .
 
Wakuu, kama mnavyojua, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimefanya chaguzi mbalimbali kuanzia ngazi ya Kanda hadi Taifa. Jambo moja lililonivutia kufikiria kwa kina ni ushiriki mdogo wa wanawake katika nafasi za uongozi. Hili ni tatizo linalozidi kuathiri usawa wa kijinsia katika siasa zetu, jambo ambalo linapaswa kujadiliwa na kutafutiwa suluhisho.

Niachane na ngazi ya kanda ambako ni fezea tupu, hali hiyo inaonekana kwa mabaraza ya vyama. Ukiondoa BAWACHA, ambalo kimsingi limeundwa kwa ajili ya wanawake pekee, mabaraza mengine kama BAVICHA na BAZECHA yanaonyesha uwakilishi wa wanawake wa kiwango cha chini mno.

Hii inadhihirika pia kwenye uchaguzi wa jumla wa viongozi wa ngazi za juu, ambapo asilimia 99.9 ya wagombea ni wanaume. Hali hii si tu inaminya fursa kwa wanawake kushiriki kikamilifu katika maamuzi, bali pia inakwamisha juhudi za kufikia usawa wa kijinsia ambao ni sehemu muhimu ya maendeleo ya kidemokrasia.

Wakuu, mnadhani nini shida hasa? Na nini kifanyike kupunguza gap hili baina ya wanaume na wanawake?

Demokrasia yenyewe ipo wapi?

Wasubiri Mugabe awavue chupi wapate VM.
 
Wakuu, kama mnavyojua, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimefanya chaguzi mbalimbali kuanzia ngazi ya Kanda hadi Taifa. Jambo moja lililonivutia kufikiria kwa kina ni ushiriki mdogo wa wanawake katika nafasi za uongozi. Hili ni tatizo linalozidi kuathiri usawa wa kijinsia katika siasa zetu, jambo ambalo linapaswa kujadiliwa na kutafutiwa suluhisho.

Niachane na ngazi ya kanda ambako ni fezea tupu, hali hiyo inaonekana kwa mabaraza ya vyama. Ukiondoa BAWACHA, ambalo kimsingi limeundwa kwa ajili ya wanawake pekee, mabaraza mengine kama BAVICHA na BAZECHA yanaonyesha uwakilishi wa wanawake wa kiwango cha chini mno.

Hii inadhihirika pia kwenye uchaguzi wa jumla wa viongozi wa ngazi za juu, ambapo asilimia 99.9 ya wagombea ni wanaume. Hali hii si tu inaminya fursa kwa wanawake kushiriki kikamilifu katika maamuzi, bali pia inakwamisha juhudi za kufikia usawa wa kijinsia ambao ni sehemu muhimu ya maendeleo ya kidemokrasia.

Wakuu, mnadhani nini shida hasa? Na nini kifanyike kupunguza gap hili baina ya wanaume na wanawake?



..bawacha iimarishwe kwa namna mbalimbali.

..wanawake wakishapitia bawacha ndio waende kwenye maeneo mengine ya uongozi katika chama.

..jambo lingine ni kwamba siasa za upinzani ni jambo la HATARI kwa mhusika kutokana na mashambulizi ya vyombo vya dola. Mazingira hayo yanakatisha tamaa wanawake kujiunga na kishiriki uongozi wa Chadema.
 
Ajenda za haki za wanawake zimeletwa na nchi za magharibi, wanawake wetu wa kiafrika hawajawahi kusema wananyanyaswa labda wachache waluohongwa . Ma feminist.
 
Back
Top Bottom