Ushirikiano na Kenya usiangalie kingine ila maslahi ya Tanzania

Ushirikiano na Kenya usiangalie kingine ila maslahi ya Tanzania

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
Ushirikiano na Kenya usiangalie kingine ila maslahi ya Tanzania.

Rais Samia Suluhu Hassan ameitembelea Kenya katika ziara inayoelezwa kuwa imefungua ukurasa mpya wa mtangamano unaoashiria kuimarisha udugu na ujirani baina ya mataifa hayo.

SAMIA%20KENYATA.jpg
Akiwa Nairobi anahutubia wafanyabiashara na wabunge wa bunge la kitaifa na la seneti wote akiwahakikishia kuwa anatamani kuona uhusiano endelevu kati ya Kenya na Tanzania.

Anawaambia wabunge:
"Binafsi nashangazwa sana na wale wanaodhani Kenya na Tanzania ni wapinzani. Mbaya zaidi ni kule kuamini kwao kwamba hilo linawezekana tu mmoja wetu kumwangusha mwenzake. Hawa ni watu wenye mioyo ya choyo, maono mafupi na akili mbovu."
"Ni bahati mbaya kuwa wapo katika pande zote mbili, Kenya na Tanzania. Hutokea pia wachache wao wakawa ni watumishi wa serikali na hata wanasiasa wa pande mbili…"

Aidha, Rais anaahidi kuwa awamu ya sita itahakikisha kuwa Kenya inabaki kuwa ndugu, jirani na mshirika wa mkakati, ahadi ambayo baadhi ya wadau wanaisifu na kuona kuwa ni mwanzo wa kudumisha ushirikiano, lakini ni lazima ulenge kwenye maslahi ya Watanzania na zaidi ya hapo utakuwa hauna tija.

Akizungumza na Nipashe kuhusu hotuba na ziara ya Rais Nairobi, Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwaa la Katiba Tanzania, (JUKATA) Bob Wangwe, anakumbusha haya:

“Jambo la muhimu pamoja na udugu na ujirani wetu na Kenya lolote lazima liwe ni maslahi ya Watanzania. Hiki ndicho kiwe kipaumbele katika kila uamuzi tunaochukua kama nchi.”

Anaunga mkono ziara ya Rais Samia, akisema ni muhimu kwani itazisaidia nchi zote mbili kujenga uelewano ambao ni muhimu katika maendeleo ya mataifa hayo kwani Kenya na Tanzania zinategemeana.

Hata hivyo, anapoulizwa kuhusu hofu kuwa mara nyingi ushirikiano umekuwa na wasiwasi, anasema hofu hazikosekani ni lazima ziwepo kwani kila nchi inafikiria zaidi kutumia fursa inazopata kwa ajili ya kuendeleza mipango na mikakati yake, hivyo kipaumbele cha kuwanufaisha Watanzania ndicho kiwe suala la msingi.

Anakumbusha kuwa ili kuwa na uhusiano na ushirikiano wenye tija kwa pande zote mbili au ‘win win situation’ ni vyema serikali mbili zingine kwenye makubaliano kwa kutambua na kuzingatia tofauti baina zao.

Anapoulizwa kuhusu suala la baadhi ya Watanzania kuona kuwa kuna mambo yanayofanywa na majirani zao ambayo yanakwenda tofauti na mustakabali wa taifa lao, mfano kutangaza Mlima Kilimanjaro kuwa uko nchi jirani.

Aidha, mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa soko kuu la bidhaa za Tanzania kinyume cha utaratibu Wangwe anasema.
“Inapotokea nchi inavunja makubaliano ya pamoja ya jumuiya hiyo ni jukumu kwa jumuiya kuwajibika katika kulinda misingi na makubaliano ya pamoja. Siyo vyema kutupiana lawama.”

Mkurugenzi Mtendaji wa JUKATA, anahimiza kuendelea kukuza uelewano wenye tija baina ya nchi wanachama na hili ndilo litakaloleta utashi wa pamoja katika kuheshimu misingi wanachama waliojiwekea.

KUTAZAMA TOFAUTI
Wangwe akizungumzia ahadi za Kenya kwa Watanzania mfano Rais Uhuru Kenyatta, anaahidi kwamba nchi yake iko tayari kuwapokea Watanzania kuendesha shughuli zao bila vibali vya ukazi na kazi.

Anafafanua kuwa kwa Kenya ni sawa lakini Tanzania ikiruhusu hilo itakuwa imefanya kosa kubwa kwa kuwa bado watu wake hawajaandaliwa.

“Hii itakuwa sahihi kama tukifanya hivyo kwa wawekezaji hasa wa daraja “A”. Tanzania tuna ardhi kubwa kweli, lakini ni kwa ajili ya Watanzania. Leo tukibadilisha mifumo yetu ya kisheria kwa lengo la “kuhonga” ardhi yetu kwa msamiati wa udugu na ujirani tutakuwa tumewakosea sana wajukuu zetu na wazee wetu ambao walitulindia ardhi hiyo.”

Anaeleza kuwa ni muhimu kushirikiana lakini maslahi ya Watanzania yawe ndicho kipaumbele bila kujali kingine na mipango ifanyike kwa kuangalia tofauti zilizopo baina ya washirika.

Rais anaahidi kuboresha na kuondoa vikwazo vya biashara vilivyopo Tanzania vinavyoathiri ushirikiano kati ya wafanyabiashara wa mataifa hayo akiahidi kuvishughulikia na ili kuwepo na biashara isiyo na vikwazo, lengo liwe ushirikiano unaoleta tija.
Wangwe anazidi kukumbusha kuwa katika hatua yoyote lazima suala la tofauti ya nchi zote mbili lizingatiwe ili mataifa yote yanufaike.
“Ni bahati mbaya sana kwamba hatua zetu Watanzania kama nchi bado ni chache ukilinganisha na Kenya, hivyo lazima tushirikiane kwa kutambua hili.”

MAONI YA WADAU
Mmoja wa wakulima wanaozungumzia biashara baina ya Kenya na Tanzania anaomba serikali itazame sheria za kununua mazao mabichi mashambani.

Wakulima Arnold Mkupete na Kulaga Ngomale, wanasema wanalima maeneo ya Mvuha na kijiji chao kinazungukwa na maji ya Mto Mvuha na mara nyingi wanafikiwa na wakulima kutoka nchi jirani ambao wananunua mazao mashambani tena kwa bei kiduchu.

Mkupete anasema: “Kuna maeneo ambayo yanawaumiza wakulima ni wageni wanaofika vijijini kununua mazao mabichi. Kwa mfano wananunua iliki mbichi kwa bei ndogo sana. Tunaomba hili likaangaliwe.”

Anaungwa mkono na Kulaga anayeshauri kuwa kuwe na magulio vijijini kama yalivyo kwenye kuuza na kununua korosho, ufuta na pamba na serikali itoe bei elekezi ili wakulima wafaidike badala ya kuacha mambo yabaki kama yalivyo ambayo hayana tija.

Baadhi ya wakulima wengine wanaozungumzia biashara za mashambani ni wa kutoka Kilimanjaro na Arusha wanaosema wafanyabiashara majirani wananunua maparachichi, mbaazi, vitunguu na mazao mengi kwa bei ndogo na kutaka kuwe na utaratibu mpya wenye tija mbali na kutaka magulio.

Wanashauri kuwe na utaratibu wa kutaja asili ya bidhaa (place of origin) na serikali kusaidia wakulima na Watanzania kupata soko la bidhaa nje moja kwa moja badala ya kuachia wageni wanaozinunua na kuziuza ughaibuni kwa faida kubwa kama za wakati walizinunua vijijini kwa bei kiduchu.

SOURCE: NIPASHE
 
Haya mambo ya kuwa 'obsessed' na nchi moja kana kwamba bila yenyewe kuwepo hamuwezi kuishi yanasikitisha sana.

Hata rais anajitumbukiza kwenye uamini potofu namna hiyo, inasikitisha sana.
"Binafsi nashangazwa sana na wale wanaodhani Kenya na Tanzania ni wapinzani. Mbaya zaidi ni kule kuamini kwao kwamba hilo linawezekana tu mmoja wetu kumwangusha mwenzake. Hawa ni watu wenye mioyo ya choyo, maono mafupi na akili mbovu."
Atafanya nini ili Tanzania na Kenya wasiwe wapinzani. Ameeleza chochote?

Hiyo ndiyo 'nature' ya mataifa haya mawili. Kenya siku zote anataka abaki juu, na ndio sababu sasa anahangaika kwa vile anaona hana uwezo wa kubaki juu kwenye ukanda huu.

Kwa hiyo mama anakwenda kumsaidia abaki juu..., mwenyewe kishajipachika cheo cha kuwa "an anchor nation; a HUB for everything" kwenye ukanda huu.

Atulie kwanza, atueleze mipango yake ipoje kuhusu atakavyoondoa "upinzani" huo.

Alipoitisha mkutano na wazee wa Dar es Salaam, wengine wetu tulidhani atatumia njia hiyo kueleza mipango yake kuhusu ziara yake hiyo, kumbe anakwenda kupiga soga na wazee!

Mikutano ya aina hiyo, na wazee wa Dar ilikuwa ni ya kueleza mambo mazito yanayolihusu taifa, sasa inageuzwa kuwa mahali pa kuzungumzia mambo ambayo hata wazee wenyewe hawakutoka na lolote?

Atulie nyumbani, afanye kazi na wananchi wake. Atafute njia za kuondoa kero nyingi zinazowazuia wasifanikishe vizuri juhudi zao.
 
Haya mambo ya kuwa 'obsessed' na nchi moja kana kwamba bila yenyewe kuwepo hamuwezi kuishi yanasikitisha sana.

Hata rais anajitumbukiza kwenye uamini potofu namna hiyo, inasikitisha sana.

Atafanya nini ili Tanzania na Kenya wasiwe wapinzani. Ameeleza chochote?

Hiyo ndiyo 'nature' ya mataifa haya mawili. Kenya siku zote anataka abaki juu, na ndio sababu sasa anahangaika kwa vile anaona hana uwezo wa kubaki juu kwenye ukanda huu.

Kwa hiyo mama anakwenda kumsaidia abaki juu..., mwenyewe kishajipachika cheo cha kuwa "an anchor nation; a HUB for everything" kwenye ukanda huu.

Atulie kwanza, atueleze mipango yake ipoje kuhusu atakavyoondoa "upinzani" huo.

Alipoitisha mkutano na wazee wa Dar es Salaam, wengine wetu tulidhani atatumia njia hiyo kueleza mipango yake kuhusu ziara yake hiyo, kumbe anakwenda kupiga soga na wazee!

Mikutano ya aina hiyo, na wazee wa Dar ilikuwa ni ya kueleza mambo mazito yanayolihusu taifa, sasa inageuzwa kuwa mahali pa kuzungumzia mambo ambayo hata wazee wenyewe hawakutoka na lolote?

Atulie nyumbani, afanye kazi na wananchi wake. Atafute njia za kuondoa kero nyingi zinazowazuia wasifanikishe vizuri juhudi zao.
hamna jema nyinyi,katoka dikteta kaingia uyu mama ana ubinadamu,,Bado mshaanza maneno maneno,,

Hii Nchi inafaa iongozwe kwa mkono wa chuma tu, maana mijitu haijulikani inataka nini , ndiomaana yule dikteta aliwanyoosha,
 
hamna jema nyinyi,katoka dikteta kaingia uyu mama ana ubinadamu,,Bado mshaanza maneno maneno,,

Hii Nchi inafaa iongozwe kwa mkono wa chuma tu, maana mijitu haijulikani inataka nini , ndiomaana yule dikteta aliwanyoosha,
Ubinaadam wake nauthamini sana; kama ambavyo sikuthamini hata kidogo ukosaji wa ubinaadam wa mtangulizi wake.

Ubinaadam wake unatakiwa uanzie kwenye kulinda maslahi ya nchi hii, kwanza na mwisho.

Ubinaadam utakuwa na thamani gani wakati tunaendelea kuwa taifa tegemezi hata kwa watu ambao ndio wanapaswa kututegemea sisi!
 
Huyu jamaa ana uwezo mdogo Sana wa kiakili
Kama Ndugai.
Actually Kama ccm wote, hakuna mwenye ubongo mle.
Wote mafuvu yao yamejaa ugali, tena Dona, maana Bora hata sembe ni mweupe, Kama Ndugai ndo uuuwi mle kwenye fuvu lake Kuna dengu kabisa
 
Tatizo linaweza kuwa si Kenya kama Kenya yenyewe; hivi ulishawahi kulifikiria hilo?

Hebu weka akili yako upande huo, utapata jibu.
Kwann watu mnapenda kumu attack mtu badala ya ku attack topic. This is so weird
 
Mkuu uzi wako unajieleza vizuri. Lakini watu wanafocus sana kukushambulia ww. Mara hujui kufikiri, mara we mjinga, mara we mataga. Kwann watu hawa focus kwenye mada
 
Some Tanzanians are suffering from Acqured Stupidity disease. Ugonjwa mbaya sana huu Mkuu na unaingamiza nchi kwa kasi ya kutisha.
Mkuu uzi wako unajieleza vizuri. Lakini watu wanafocus sana kukushambulia ww. Mara hujui kufikiri, mara we mjinga, mara we mataga. Kwann watu hawa focus kwenye mada
 
Mie naunga mkono kwamba Tanzania ni sharti ipiganie maslahi yake hatua ya kwanza na mwisho ndipo kushikana mikono kwa pamoja tofauti na hapo Kenya hawauzi sura hata siku moja, hawako kwa ajili ya kupoteza kwa kusaidia Tanzania kuinuka kiuchumi kamwe.

Mfano mzuri miaka ya 1970-1990 biadhaa nyingi zilizofurika soko kanda ya ziwa hususani Mwanza, Mara na Shinyanga vilikuwa vinatoka Nairobi kuanzia kanda mbili za mabondo hadi mabati na simenti. Uganda na Zaire kipindi hicho bidhaa zao nyingi zilikuwa Vitenge ambavyo kwa kweli vilikuwa ni bora.

Watanzania kwa kutothamini vya kwao au tamaa binafsi walichangia sana kufifisha kilimo cha pamba na mazao ya bidhaa yake kwenye viwanda nguo Mwatex, Mutex, uchakataji wa mafuta na mashidu kwa matumi ya mifugo.

Rais Uhuru Kenyatta kualika Watanzania kuwekeza au kufanya biashara nchini Kenya bila kizingiti cha vibali ni lugha laghai; Wakenya tunawafahamu fika kwamba hakuna hata mmoja huwa yuko tayari kuongozwa na Mtanzania hata amezidiwa elimu na ujuzi kwa sababu ya kasumba ya ustarabu wa matumizi ya lugha ya kiingereza kuwa ni wajanjawajanja.

Katika ukanda wa Afrika masharika taifa lenye watu wenye majivuno ni Kenya wakijiona wana nguvu za kiuchumi kwa kuwa makampuni mengi ya kigeni yanapotaka kuwekeza yanapitia Kenya na kutengeneza endapo wanapopata kazi Tanzania kipato kinafasiriwa kwa thamani ya dola sio shilingi ya Tanzania.

Hapa kinachotakiwa ni kwa Watanzania ni kuweka pembeni tofauti za kiitikadi za siasa za ndani na kuungana kuitetea Tanzania tu ijapokuwa kwenye mashirikiano yataendelea tu.

Kenya hakuna fursa za uwekezaji wenye faida zaidi ya soko la chakula na nishati kitu ambacho makampuni mengini kutoka Tanzania wanakwepa kwa kuwa hawatabiriki. Pili kwa sasa Kenya hakuna usalama kutokana na tishio la ugaidi kutokea Somalia (Al Shabab) kutamalaki karibu miaka saba

Mwanzo na mwisho inatakiwa kuwa ni Tanzania kwanza kisha sambamba kwa pamoja tunafika endapo kila mmoja atamheshimu mwingine kutokana na hatua anazochukua kukuza uchumi.

Misaada na uwekezaji kutoka nje ya nchi usiwe tegemeo siku zote huku mkiwa mnazurura kutafuta wawekezaji bila ya ninyi wenyewe kubuni miradi ya nchi ya kiuwekezezaji huku wazawa wakipwea fursa za kwanza bila kuwabughudhi wakati huo huo elimu ya utoaji kodui kwa hiari na fahari ukihimizwa.
 
We ni mpuuzi kama id yako
Tanzania ili inyooke kisawasawa inatakiwa kuongozwa kiimla kwa miaka kumi mfululizo kisha wafuate viongozi wasio jasiri, lugha laini na ulaghai kwa mataifa, tofauti ya hapo nchi jirani zinakuja kwa kasi sana kuifanya koloni lake kwa kuwatumia viongozi hao hao waliko madarakani au ambao walishawahi kuongoza kwa mtindo wa ushikaji.

Siasa sa uhasama ndio zinazokwamishwa kufukia malengo ya nchi kwa maendeleo kwa pamoja kwa kuhusi mtu fulani akiweza kuifikisha kwenye kilele cha heshima atawafunika.......huo ni utwana wa kimangi meza ambao unatakiwa kukataliwa.

Hakuna nchi itakuja kuwasaidia kujenga namna bora ya uchumi wenu ili muwazidi!!!

Manyani yanarejea shambani kwa kasi mijini hadi vijijini
 
Kwann watu mnapenda kumu attack mtu badala ya ku attack topic. This is so weird
Kama wewe ni 'genius' kweli kama unavyojitangaza na jina hilo; hebu onyesha kwenye maneno hayo uliyo'quote' ni maneno yapi yanamu"attack" mtu, na useme mtu huyo ni yupi aliye'atakiwa'!

Au umeamua tu kujiandikia ili ujifurahishe mwenyewe?

Kama hutaweza kufanya hivyo, nakushauri ubadili jina ujulikane kama KILAZA JAGUAR MONSTER.
 
Rais Uhuru Kenyatta kualika Watanzania kuwekeza au kufanya biashara nchini Kenya bila kizingiti cha vibali ni lugha laghai;
Ukifuatilia vizuri, hii sio mara yake ya kwanza, na si kwa Tanzania pekee ameyasema maneno hayo. Ni maneno ya kunogesha kadamnasi tu, hayana maana yoyote, kwani hayatimizwi.
 
Wewe kweli hujui kile unachokisema, wadhani kama Kenya haingekuwa salama wale wawekezaji wangekuwa bado wako?

Shida yenu wabongo nikupenda excuses sana, nchi kubwa kama yenu yenye rasilimali kibao na ardhi kubwa na population kubwa haifai kuitazama nchi ndogo kama Kenya kama mshindani.

Kazi tu nikupiga gumzo asubuhi, mchana mpaka usiku kwenye mitandao. Oooh sijui wakenya tuwe makini nao mara oooh wakenya hawaaminiki. Kuweni serious nyinyi kwa sababu kama uchumi ungekuwa unajengwa kwa mdomo, duuh tz ingekuwa super power 😂😂
 
Back
Top Bottom