Ushirikiano wa BRICS unakuwa na manufaa zaidi kutokana na ujumuishi

Ushirikiano wa BRICS unakuwa na manufaa zaidi kutokana na ujumuishi

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG211203260160.png

Mkutano wa Mawaziri wa Kundi la BRICS umefanyika kuanzia Juni 10 hadi 11 huko Nizhny Novgorod, nchini Russia. Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi alihudhuria mkutano pamoja na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za BRICS na wawakilishi kutoka Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai na ASEAN. Pia wawakilishi kutoka Umoja wa Afrika na Umoja wa Nchi za Kiarabu pia walialikwa katika mkutano huo.

Katika wakati huu ambapo nguvu za mrengo wa kulia zinaathiri Bunge la Ulaya na vita kati ya Israel na Palestina vinagawa mitazamo ya dunia, BRICS inaendelea kuwa na umoja na kufanikiwa, na kuvutia ufuatiliaji wa kimataifa kutokana na utulivu wake.

Saudi Arabia, Misri, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Iran na Ethiopia zilijiunga rasmi na BRICS mwezi Jamuari mwaka huu, na kuwa alama kubwa ya maendeleo ya mfumo wa BRICS. Upanuzi wa familia ya BRICS inayojumuisha nchi za Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini bado unaendelea, huku nchi nyingi zikionyesha kuvutiwa ama kuwasilisha maombi rasmi ya kujiunga na mfumo wa BRICS. Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan alisema wakati akiwa ziarani hapa China Juni 3 kwamba, Uturuki inatarajia kujiunga na BRICS, na mwishoni mwa mwezi Mei, serikali ya Thailand iliridhia muswada wa barua rasmi inayoashiria nia ya nchi hiyo kuwa mwanachama wa BRICS. Jamii ya kimataifa inafuatilia sana utambulisho wa nchi hizo mbili kama ‘mwanachama wa NATO’ na ‘nchi ya ASEAN,’ hali ambayo sio tu inapanua fikira za familia ya BRICS lakini pia inatoa ujumbe wa kipekee wa ujumuishi kwa ajili ya ushirikiano mpana zaidi wa BRICS.

Kiuhalisia, ‘uwazi, ujumuishi, ushirikiano na kunufaishana’ daima vimekuwa ni moto ya mfumo wa BRICS. Tangu mwanzo, mfumo huu umejiwekea kanuni ya kutojihusisha na masuala ya kisiasa, kutoegemea upande wowote katika migogoro, na kutotaka kuondoa mtu yoyote. Kanuni hizi hazijabadilika kabla na hata baada ya kundi hilo kuongeza nchi wanachama. Nchi zinazoendelea zinatambua kabisa moyo wa BRICS na kutambua mfumo wa ushirikiano wa kundi hilo. Mshauri wa Rais wa Nicaragua, Laureano Ortega Murillo anazifananisha nchi za BRICS na familia kubwa inayojitahidi kujenga dunia ya usawa zaidi. Kwa jamii ya kimataifa, hii haimaanishi tu kwamba ushirikiano zaidi katika Nyanja ya fedha, kutoa msukumo kwa uchumi wa dunia kukabiliana na changamoto, lakini muhimu zaidi, ina maana kuwa idadi kubwa ya watu watapata fursa ya kuwa na sauti ambayo kwa hakika wanastahili, jambo ambalo ni kiini cha kutimiza usawa na haki katika utaratibu wa kimataifa.

Wakati huohuo, Kundi la Nchi 7 (G7) nalo linafanya mkutano wake kuanzia Juni 13 hadi 15 nchini Italia, na kabla ya mkutano huo, ajenda ya kulazimisha vikwazo kwa upande mmoja na kuchochea mivutano kati ya kambi imewekwa wazi na vyombo vya habari. Imeripotiwa kuwa, Kundi hilo linatarajiwa sio tu kuendelea kuegemea upande mmoja katika vita kati ya Russia na Ukraine, bali pia kuichafua China kwa ‘kuisaidia Russia kukwepa vikwazi vya nchi za Magharibi.’ G7, linalojumuisha Marekani na wenza wake wakuu, linawakilisha kundi la nchi tajiri zaidi duniani lakini mara nyingi linaonyesha upekee na kulenga maslahi katika mtazamo wake finyu. Mtindo huu wa ‘kurusha ngumi’ ili kudumisha mamlaka yake duniani kwa kweli hauvutii, na pia si ajabu kwamba ufahari na ushawishi wa G7 si mkubwa kama ilivyokuwa awali.

Tofauti na G7, mfumo wa BRICS unatetea tabia ya ‘kukumbatia’ kuliko ‘kurusha ngumi.’ Mfumo huu unazingatia kuanzisha uaminifu wa kisiasa kwa msingi wa kuheshimu mamlaka na maslahi muhimu ya kila nchi, kushughulika na mabadilishano ya kitamaduni kwa udhati kwa msingi wa kuheshimu staarabu tofauti, historia, na njia za maendeleo, na kukumbatisha ushirikiano wa kiuchumi na kifedha kwa mtazamo wa usawa na kunufaishana bila ya kujihusisha na mazingira yoyote ya kisiasa.

Wakati likivutia nchi nyingi zinazoibuka kiuchumi, BRICS haijazitenga nchi zinazoendelea. Taasisi kama Benki Mpya ya Maendeleo ya BRICS zinakaribisha ushiriki wa nchi zinazoendelea. Wakati Dunia ya Kusini inaendelea kuonyesha kujiamini na haiko tena tayari kushiriki bila ya sauti katika mfumo wa kimataifa, ushirikiano mpana wa BRICS unajibu wito wa maendeleo ya kihistoria.

Katika siku za baadaye, BRICS, itakayokuwa na wanachama zaidi na wenzi, itakuwa kituo cha nguvu ya pande nyingi inayojizatiti katika kujenga utaratibu wa kimataifa ambao ni wa haki, usawa, na jumuishi, na kuifanya hatma ya jamii ya binadamu kuwa bora zaidi.
 
Kwa mtizamo wangu BRICS haitafanikiwa, kwa sababu inaonekana ni kama wanunda kundi hili kuwakomoa G7 na hasa USA. Kumbuka nchi waanzilishi wa hilo kundi ni watukutu, na kwa sababu hiyo nawaona kama wanafunzi walio pumzishwa shule kwa utovu wa nidhamu na sasa wanaunda umoja kumkomoa mwalimu au shule iliyo waadhibu.

Kinachofanywa na Russia,China na Iran sio sawa. Russia inalazimisha kurudisha mataifa yote yaliyounda USSR kwa NGUVU, na CHINA inataka Taiwan irudi China kwa nguvu, Iran wao wanataka kuiteketeza Israel.

Vikwazo wanawekewa na wenye nazo, na technologia, Utukutu sio mzuri waache wafuate mstari. Hii kuunda vikundi vya kugoma na nisawa na majambazi kuwagomea Polisi, na kuunda umoja wa kusaidiana kwamba akikamatwa mmoja wetu basi nasi tunakula sahani moja na polisi. Kwa mantiki yao Dunia inakuwa siyo mahala salama tena.

Bretton woods system nayo ilianzia mbali mpaka kuunda, tangu metalic, gold to paper. Sasa tunaenda digital.
Ngoja tuone watafika wapi.
 
1. Sio BRICS tena maana wanachama wameongezeka,

2. Wengi wao wanajiweza kiuchumi tofauti na Ndugu zetu Malawi ambao hata kutafuta ndege iliyoangukia Mjini wanaomba Msaada dunia nzima wengine ndo wa kuomba omba mikopo kila uchwao.
 
1. Sio BRICS tena maana wanachama wameongezeka,

2. Wengi wao wanajiweza kiuchumi tofauti na Ndugu zetu Malawi ambao hata kutafuta ndege iliyoangukia Mjini wanaomba Msaada dunia nzima wengine ndo wa kuomba omba mikopo kila uchwao.
Si uhamie huko we bwege. We ht ukoo wako unauponda kwa umaskini mlionao.
 
Kwa mtizamo wangu BRICS haitafanikiwa, kwa sababu inaonekana ni kama wanunda kundi hili kuwakomoa G7 na hasa USA. Kumbuka nchi waanzilishi wa hilo kundi ni watukutu, na kwa sababu hiyo nawaona kama wanafunzi walio pumzishwa shule kwa utovu wa nidhamu na sasa wanaunda umoja kumkomoa mwalimu au shule iliyo waadhibu.

Kinachofanywa na Russia,China na Iran sio sawa. Russia inalazimisha kurudisha mataifa yote yaliyounda USSR kwa NGUVU, na CHINA inataka Taiwan irudi China kwa nguvu, Iran wao wanataka kuiteketeza Israel.

Vikwazo wanawekewa na wenye nazo, na technologia, Utukutu sio mzuri waache wafuate mstari. Hii kuunda vikundi vya kugoma na nisawa na majambazi kuwagomea Polisi, na kuunda umoja wa kusaidiana kwamba akikamatwa mmoja wetu basi nasi tunakula sahani moja na polisi. Kwa mantiki yao Dunia inakuwa siyo mahala salama tena.

Bretton woods system nayo ilianzia mbali mpaka kuunda, tangu metalic, gold to paper. Sasa tunaenda digital.
Ngoja tuone watafika wapi.
Muungano au ushirika unaoweza kudumu kwa muda mrefu unahitaji misingi ya kipekee na ya pamoja (common interests and values) inayowaunganisha wanachama katika muungano huo kitu ambacho ni tofauti sana kwenye BRICS.

Ukiuliza baadhi ya wasomi kuhusu lengo la uwepo wa BRICS watakuambia kuwa lengo kuu linaloziunganisha nchi wanachama ni kuondokana na utawala wa "mabavu" wa kiuchumi wa Magharibi (Western economic hegemony).

Tatizo linakuja pale muungano unapokuwa na wanachama wakubwa ambao hawakubaliani katika misingi inayopaswa kujenga umoja na "ujumuishi" anaosema mleta uzi, mfano China na India.

Hawa members wawili wenye uchumi mkubwa zaidi ndani ya BRICS (China na India) ni mahasimu wakubwa na wameshakumbana katika migogoro mingi hususani ya kimipaka na hata kiuchumi vilevile.

Isitoshe, baadhi ya members wana mahusiano ya kiuchumi na kiulinzi/kijeshi na nchi za magharibi ambazo zinatazamwa kama "adui wa kiuchumi" na baadhi ya wanachama wa BRICS. Mfano uleule; India ina ushirikiano mzuri zaidi wa kiuchumi na kijeshi na nchi za magharibi hasa Marekani kuliko ushirikiano ilionao na China ambayo ni mwanachama mwenzake wa BRICS.

Hivyo, muafaka wenye maslahi ya pamoja ndani ya ushirika unakosekana kutokana na utofauti wa misingi/maslahi na uwepo wa uhasama au migogoro kati ya members wenye ushawishi mkubwa zaidi ndani ya ushirika.
 
Muungano au ushirika unaoweza kudumu kwa muda mrefu unahitaji misingi ya kipekee na ya pamoja (common interests and values) inayowaunganisha wanachama katika muungano huo kitu ambacho ni tofauti sana kwenye BRICS.

Ukiuliza baadhi ya wasomi kuhusu lengo la uwepo wa BRICS watakuambia kuwa lengo kuu linaloziunganisha nchi wanachama ni kuondokana na utawala wa "mabavu" wa kiuchumi wa Magharibi (Western economic hegemony).

Tatizo linakuja pale muungano unapokuwa na wanachama wakubwa ambao hawakubaliani katika misingi inayopaswa kujenga umoja na "ujumuishi" anaosema mleta uzi, mfano China na India.

Hawa members wawili wenye uchumi mkubwa zaidi ndani ya BRICS (China na India) ni mahasimu wakubwa na wameshakumbana katika migogoro mingi hususani ya kimipaka na hata kiuchumi vilevile.

Isitoshe, baadhi ya members wana mahusiano ya kiuchumi na kiulinzi/kijeshi na nchi za magharibi ambazo zinatazamwa kama "adui wa kiuchumi" na baadhi ya wanachama wa BRICS. Mfano uleule; India ina ushirikiano mzuri zaidi wa kiuchumi na kijeshi na nchi za magharibi hasa Marekani kuliko ushirikiano ilionao na China ambayo ni mwanachama mwenzake wa BRICS.

Hivyo, muafaka wenye maslahi ya pamoja ndani ya ushirika unakosekana kutokana na utofauti wa misingi/maslahi na uwepo wa uhasama au migogoro kati ya members wenye ushawishi mkubwa zaidi ndani ya ushirika.
Hawa hawana tofauti na OAU au AU. Wana baraza lao lakini kila siku wanapishana kwenye ndege kwenda marekani, ukiwauliza wanakwambia kila mtu anashida zake.

Hata vinchi vyetu hivi kule viameweka wasikilizaji, vipo huko na kule, havijui BRICS itakuwa nini kesho hivyo vimeweka masikio sawa. Kule kukiwaka utavisikia safari za ASIA haziishi kwenda kuomba.
BRICS naona wamesha fail.
 
Back
Top Bottom