Ushirikiano wa Tanzania na Hungary wazidi kung’aa

Ushirikiano wa Tanzania na Hungary wazidi kung’aa

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
publer-1740007239797.jpg

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amewasili jijini Budapest, Hungary kwa ziara ya kikazi ya siku nne (4) inayolenga kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na kiuchumi baina ya Tanzania na Hungary.

Baada ya kuwasili, Waziri Kombo amefanya kikao cha ndani cha maandalizi na timu ya Tanzania kwa lengo la kutathimini maeneo ya kipaumbele ya ushirikiano baina ya Tanzania na Hungary katika sekta ya maji, elimu na kujengeana uwezo, afya, biashara na uwekezaji, utalii, nishati na mazingira, michezo na utamaduni.

publer-1740007236490.jpg


Ziara hiyo ya siku nne (4) inafuatia mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Hungary, Mhe. Péter Szijjártó kufuatia kuendelea kuimarika kwa ushirikiano kati ya Nchi hizo mbili.

Aidha, Mhe. Kombo ameongozana na Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb.); Balozi wa Tanzania nchini Hungary Mhe. Hassan Mwamweta; Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri na viongozi wengine waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

publer-1740007242331.jpg
publer-1740007247764.jpg
 

Attachments

  • publer-1740007233604.jpg
    publer-1740007233604.jpg
    83.7 KB · Views: 2
  • publer-1740007245045.jpg
    publer-1740007245045.jpg
    70.6 KB · Views: 2
  • publer-1740007250426.jpg
    publer-1740007250426.jpg
    56.7 KB · Views: 2
  • publer-1740007253193.jpg
    publer-1740007253193.jpg
    77.9 KB · Views: 2
  • publer-1740007255890.jpg
    publer-1740007255890.jpg
    77.4 KB · Views: 3
Hapo chawa mnafurahia misaada tu, kuwalamba miguu Hungury watoe misaada.

Kwenye huo udhirikiano anaefurahia zaidi ni chawa ili aendelee kunyonya damu za wahangury.

Hao Hungury na wengine hawawezi kutoa hata robo ya hela iliyokua ikitoka USAID, hakuna.

Hata tukijifariji na watu gani bado baba mwenye nyumba ni USA. Kaeni mkao wa kutulia dawa chungu iwaingie.
 
Hungary yenyewe ni nchi maskini tu. Imekuwa inategemea misaada ya EU sana na rais wake ni mtu mbaguzi kweli kweli. Hapo wabongo wanonekana takataka tu. Orban ni kopi ya Trump; kwa hiyo nyinyi hapo ni A$$hole tu
 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amewasili jijini Budapest, Hungary kwa ziara ya kikazi ya siku nne (4) inayolenga kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na kiuchumi baina ya Tanzania na Hungary.

Baada ya kuwasili, Waziri Kombo amefanya kikao cha ndani cha maandalizi na timu ya Tanzania kwa lengo la kutathimini maeneo ya kipaumbele ya ushirikiano baina ya Tanzania na Hungary katika sekta ya maji, elimu na kujengeana uwezo, afya, biashara na uwekezaji, utalii, nishati na mazingira, michezo na utamaduni.

View attachment 3242328

Ziara hiyo ya siku nne (4) inafuatia mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Hungary, Mhe. Péter Szijjártó kufuatia kuendelea kuimarika kwa ushirikiano kati ya Nchi hizo mbili.

Aidha, Mhe. Kombo ameongozana na Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb.); Balozi wa Tanzania nchini Hungary Mhe. Hassan Mwamweta; Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri na viongozi wengine waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

View attachment 3242329View attachment 3242331
Hapo chawa mnafurahia misaada tu, kuwalamba miguu Hungury watoe misaada.

Kwenye huo udhirikiano anaefurahia zaidi ni chawa ili aendelee kunyonya damu za wahangury.

Hao Hungury na wengine hawawezi kutoa hata robo ya hela iliyokua ikitoka USAID, hakuna.

Hata tukijifariji na watu gani bado baba mwenye nyumba ni USA. Kaeni mkao wa kutulia dawa chungu iwaingie.
Hungary yenyewe ni nchi maskini tu. Imekuwa inategemea misaada ya EU sana na rais wake ni mtu mbaguzi kweli kweli. Hapo wabongo wanonekana takataka tu. Orban ni kopi ya Trump; kwa hiyo nyinyi hapo ni A$$hole tu

Hungary kwanza hawapendi Watu weusi, nchi maskini na mbaya zaidi Sana Watawala wa Hungary na Wananchi wao wameegemea Siasa za Itikadi za Ukomunisti/Ujamaa Kama ilivyo kwa Urusi
 
Rais wake mbaguzi nchi masikini inayopewa misaada na EU sisi ndio wa kwenda kutembeza bakuli kwao?
So funny ila ni matonyaland tumemaliza China, Arabuni, Korea EU ,US wamekata mrija sasa tunaenda kwa maskini wenzetu.
Ombaombania.
 
Timu Hungary ya Taifa miaka ya 80 ilikuwa inakimbiza sana ..sijui imekuwa je!!?? hata wanachezaji wake siwasikii kwenye ligi kubwa!!! kuhusu mambo ya ushirikiano nawatkia kheri ila iwe ya kupeana ujuzi zaidi siyo kuombana pesa!!!!!!
 
Likitamkwa neno Hungary mimi kichwani natafsiri Ikarus 😀, marafiki wa kweli wa Tanzania yetu.
 
Back
Top Bottom