Bright18
New Member
- Jul 5, 2023
- 1
- 1
UTANGULIZI
A: 1. SEKTA YA UTALII.
Sekta ya utalii ni miongoni mwa sekta mama hapa nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, sekta hii huchangia takribani asilimia kumi na saba (17%) ya pato la nchi pia ni miongoni mwa vyanzo vikubwa vya ajira kwa rika zote kuanzia wamiliki wa makampuni ya utalii, watoa huduma kwa watalii (wasafirishaji na hoteli) hadi waongoza watalii kwenye maeneo husika.
2. FAIDA ZA SEKTA YA UTALII.
Licha ya kua na faida za maendeleo ya kiuchumi utalii huchangia kujenga afya ya mwili na akili kwa kusaidia mshiriki (mtalii) kupunguza msongo wa mawazo, utalii huchangia katika utunzaji na uendelezwaji wa rasilimali na vivutio vya nchi kuanzia wanyama pori, misitu na vyanzo vya maji, vile vile utalii kwa kiasi kikubwa unachangia uhusiano mzuri baina ya wageni na wenyeji na baina ya nchi na nchi.
B: MAKUNDI MAALUMU.
Watu wenye mahitaji maalum wapo wenye ulemavu wa kimaumbo, kiakili na kitabia kundi hili la watu wenye mahitaji maalumu wanaweza kupatikana majumbani na katika vituo vinavyotoa huduma za kuwatunza.
Kwenye jamii zetu za kitanzania na duniani kwa ujumla tunashuhudia ongezeko kubwa la watu wenye mahitaji maalamu ( watu wenye ulemavu) mwaka 2012 watu wenye ulemavu duniani walikua milioni 650 sawa na aslimia kumi (10%) kwa sasa kuna watu bilioni 1.3 sawa na asilimia kumi na sita (16%) ya idadi ya watu wote duniani.
Ongezeko hili la watu wenye mahitaji maalumu lina mchango mkubwa katika sekta ya utalii.
Mwisho, ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu ni muhimu uzingatie afya ya mhusika kwa ujumla, chaguo pekee analopendelea mshiriki, usalama wa shughuli husika, vifaa rasmi kwaajili ya kumuwezesha kushiriki.
Kwa kuwawezesha watu wenye mahitaji maalumu tunawajengea uwezo wa kutoa mchango wao na kua tegemeo ndani ya familia na taifa kwa ujumla.
A: 1. SEKTA YA UTALII.
Sekta ya utalii ni miongoni mwa sekta mama hapa nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, sekta hii huchangia takribani asilimia kumi na saba (17%) ya pato la nchi pia ni miongoni mwa vyanzo vikubwa vya ajira kwa rika zote kuanzia wamiliki wa makampuni ya utalii, watoa huduma kwa watalii (wasafirishaji na hoteli) hadi waongoza watalii kwenye maeneo husika.
2. FAIDA ZA SEKTA YA UTALII.
Licha ya kua na faida za maendeleo ya kiuchumi utalii huchangia kujenga afya ya mwili na akili kwa kusaidia mshiriki (mtalii) kupunguza msongo wa mawazo, utalii huchangia katika utunzaji na uendelezwaji wa rasilimali na vivutio vya nchi kuanzia wanyama pori, misitu na vyanzo vya maji, vile vile utalii kwa kiasi kikubwa unachangia uhusiano mzuri baina ya wageni na wenyeji na baina ya nchi na nchi.
B: MAKUNDI MAALUMU.
Watu wenye mahitaji maalum wapo wenye ulemavu wa kimaumbo, kiakili na kitabia kundi hili la watu wenye mahitaji maalumu wanaweza kupatikana majumbani na katika vituo vinavyotoa huduma za kuwatunza.
Kwenye jamii zetu za kitanzania na duniani kwa ujumla tunashuhudia ongezeko kubwa la watu wenye mahitaji maalamu ( watu wenye ulemavu) mwaka 2012 watu wenye ulemavu duniani walikua milioni 650 sawa na aslimia kumi (10%) kwa sasa kuna watu bilioni 1.3 sawa na asilimia kumi na sita (16%) ya idadi ya watu wote duniani.
Ongezeko hili la watu wenye mahitaji maalumu lina mchango mkubwa katika sekta ya utalii.
- Haki za ushirikishwaji katika nyanja za kiuchumi na kijamii.
- Sababu za kutoshiriki kwenye shughuli za kitalii.
- Mapendekezo kwa serikali na wizara husika.
- Kutoa elimu kwa jamii kuhusu ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu kwenye utalii;
- Kuboresha miundombinu na kuongeza vifaa shirikishi na wezeshi kwa watu wenye ulemavu;
- Kuandaa matamasha makubwa kwaajili ya watu wenye ulemavu; Kwa kuandaa matamasha na majarida mbalimbali ya kitalii kwaajili ya watu wenye mahitaji maalumu yatasaidia kwa kiwango kikubwa kuhamasisha kundi hili kujitokeza kwa wingi na kuongeza ushawishi kwenye jamii na kushiriki katika shughuli tofauti tofauti za kitalii.
- Serikali itenge bajeti maalumu kwaajili ya ushiriki wa watu wenye ulemavu kwenye sekta ya utalii; Bajeti hii itasaidia kuchochea ushiriki wa watu wenye mahitaji maalumu kwa kuandaa zawadi mbalimbali kwa washindi.
- Mapendekezo kwa jamii (Tanzania)
- Kuacha mila ya kwaficha watu wenye ulemavu ndani;
- Jamii izingatie kipaji na uwezo alionao mtu mwenye ulemavu;
- Ushauri kwa Jamii
- Maoni.
Mwisho, ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu ni muhimu uzingatie afya ya mhusika kwa ujumla, chaguo pekee analopendelea mshiriki, usalama wa shughuli husika, vifaa rasmi kwaajili ya kumuwezesha kushiriki.
Kwa kuwawezesha watu wenye mahitaji maalumu tunawajengea uwezo wa kutoa mchango wao na kua tegemeo ndani ya familia na taifa kwa ujumla.
Upvote
1