Ushuhuda Toka Loliondo....Serikali Inaficha Nini Loliondo..Wakati Wanajua Hakuna Tiba?

Hapo awali ilisemekana kama Ulikuwa kwenye ARV, ukipata kikombe cha babu basi uziache hizo ARV.
Sasa hivi kibao kimegeuka, ukiwa kwenye ARV, kisha ukapata kikombe cha babu, basi endelea tu na hizo ARV. sasa mimi najiuliza mbona haya masharti yanabadirika badirika?.

Kuna kitu kimoja, kna mtu alishawahi kuniambia, kwamba pindi Nchini kunapokuwa na mijadala mikali sana kiasi kwamba kutishia amani Usalama wa Taifa huwa wanaibua kituko fulani ili kubadili upepo wa mijadala. chukulieni mfano wa ishu ya mtu Kuota manyoya Salender bridge, inasemekana hiyo ishu iliibuliwa kimakusudi na usalama wa Taifa ili watu wapay attention kwa hiyo issue waache kuhoji mambo fulani. Au Chukulieni issue ya Popo bawa kule Zanzibar katika miaka ya 90.

This time inawezekana wameamua kumtumia babu, japo inawezekana Babu mwenyewe haelewi hii game inavyochezwa, yeye anaamini kwamba kweli kafunuliwa, kumbe usalama wa Taifa wanatumia vyombo vya habari kumpaisha, na unaweza kukuta viongozi wengine wanaokwenda huko ni maajenti wa usalama, wanajua wanachokifanya, wengine hawajui kwa sababu si viongozi wote wanapata classified info za usalama wa Taifa n.k, Ukizingatia hali ya kisiasa ilivyo tete nchini, kuanzia uchaguzi mkuu uliopita, Dowans, Inflation kali, Kupanda kwa bei ya Umeme, Mishahara minono ya Wabunge, Mgawo wa umeme. Hii yote ni mijadala mikali ambayo imezaa hasira kwa wananchi, na hasira hizo kujionyesha wazi kwenye maandamano ya Chadema, hivi hamuoni kwamba inawezekana kweli Usalama wa Taifa kujaribu kudivert attention za watu?

Tuweni makini waungwana, tusije tukawa tumepigwa changa la macho.

Kuhusu kupata nafuu kwa wagonjwa wa kisukari, huo mti wa Babu wataalamu wa madawa ya kiasili ya mimea wanasema una tabia ya kusaidia wagonjwa wa kisukari, kwa hiyo suala hapa siyo imani, bali ni kwamba huo mti kwa asili yake unasaidia wenye kisukari, ni vyema watu wakajitafutia huo mti na kujitengenezea dawa, kuliko kwenda kwa Babu anayedai eti lazima dawa akupe yeye ndo upone!
 
kupanga ni kuchagua. unaweza kuchagua koroma ukaacha nazi! nashauri tu wale wasio na imani waendelee kula ARVs kwani babu hajakataza lakini wanaoamini kuwa wanpona naomba waende kwa babu kwani mtu akiwa ni mgonjwa anamateso makubwa mnu zaidi ya mtu kumwona mwenzake akifia kwenye foleni! Jamani kwa babu ni hiari kabisa na wala babu hajaita mtu ila watu wanajipeleka. La msingi hapa ni kupata ushahidi ili kama mtu akiamua kwenda basi aende huku akijua kuwa watu hawaponi au wanapona. Ni muhimu tukajua kuwa kuna watu wanampiga vita babu kwani wengine walikuwa wamejikweza kuwa ni viboko wa magonjwa na majini na kumwona Mungu kama hana nafasi katika uponyaji wanaoufanya. hapa kwao babu ni threat hivyo wanaweza kuweka mapandikizi humu na usipokuwa makini unaweza kusema kuwa yaliyoandikwa ni kweli kumbe watu wanatetea sadaka iliyopungua!!
 

Pole sana ndugu.


Kwakweli inasikitisha kusikia mambo kama hayo ila ieleweke kuwa serikali haiwezi kufanya lolote katika haya kwasababu inafaidika kwa kiasi fulani.

Wengi siku hizi hawaongelei kuhusu matatizo ya nchi. Mambo kama katiba mpya, Dowans n.k. Kila mtu ni loliondo kwahiyo serikali haiwezi kusema wala kuripoti chochote kuhusu hao wanaotupa maiti za ndugu zao kwasababu serikali inapata muda wa kupumua (wakati wananchi wakipumbazwa) ilimradi siku ziende.

Loliondo hakuna uponyaji ila ni placebo effect ndiyo inayofanya kazi. Ni kweli kwakutumia uwezo wa akili (mind) mtu anaweza kupata ahuweni na hata kupona kwasabau "mind" ikishirikiana na mwili inaweza kuongeza immune system (at the cellular level).

Je, ni kweli babu alioteshwa na Mungu? Labda babu ana mungu wake nisiye mjua mimi ila niseme tuu binadabu tuna kitu kinaitwa mawazo (thoughts) amabayo yanaweza kubadilisha hata jinsi mfumo wa fahamu (nervous system) na mifumo mingine ya mwili ufanyaji wake kazi. Kwahiyo kama kunawalio pona basi wajue si kikombe bali in placebo effect tuu.
 
Serikali inajua kwa Babu ni magumashi tu. Vinginevyo Ocean Road Cancer Institute ingeshafungwa, TACAIDS ingeshavunjwa. Waliingia mkenge kwa kigagula huyu wakamwacha akatamba sana. Na kwa vile VIONGOZI wetu wengi ni wagonjwa sugu wakajikuta nao wamenasa!
 
ONYO: DAWA ZISIBEBESHWE KAZI ISIYO YAKE

.... dawa hazina akili
.... dawa hazina hekima
..... dawa hazitafakari
..... dawa hazina nidhamu
.... dawa hazina maadili
.... dawa hazimjui Mungu
.... dawa hazina imani
.... dawa hazihitaji kujiwajibikia
.....dawa hazihitaji kujiheshimu
....dawa hazihitaji kujisimamia, kujivumulia tamaa, hamu na hisia mbaya...

HAYA YOTE NI MAJUKUMU YA MTU... NI UJINGA KUSUBIRI DAWA ITUFANYIE YOTE HAYA.

NI UPUUZI ZAIDI KUONA SEREKALI IKISUBIRI DAWA ZIFANYE MAJUKUMU YAKE...

NB: TUJIWAJIBIKIE kama watu timamu na akili zilizopevuka tuache porojo!!!!
 
Pole sana jirani, ila mie nina maoni kidogo kwa hawa waliokwisha kunywa dawa ya babu, mana wengi wanaoshuhudia ni wenye visukari tu na presha nakadhalika nadhani kwa statistic ya ushuhudiaji kwa magonjwa hayo inatosha kumjengea mtu imani ila bado statistic ya kutosha tena yenye vielelezo haijawekwa wazi ya kuhusu gonjwa la Ukimwi. Wito wangu.. Jamani mliokwisha kunywa kikombe cha babu na mmeathirika tumwagieni maushuhuda kama alivofanya jirani yangu, na pia hata huku mitaani kwetu tuwajue ni akina nani hasa waliopona na statistics yao itatujengea imani zaidi.
Msisahau Imani hutenda kazi pasipo Mashaka.
 

Sasa hivi unadhani umepona, ila ikilipuka unaenda kwenye coma.
 

Yes, mind is a very complex organ, we live in one earth but different worlds, ndiyo maana hata ndoto kila mtu huota kivyake, na ndoto hazifanani. Unaweza kuota unaungua, umekutana na Mungu au Yesu au Malaika, umenyeshewa maji kumbe uko kitandani umelala tu. Ipo siku ukweli utajulikana kuhusu wanaodai kuoteshwa na Mungu while actually they are chasing figments of their own immaginations zinazochangiwa na umaskini na ufukara.
 

Yaani its unbelievable! Wana excuse kwenye kila linalotokea kwa huyo kigagula. Wanaokunywa dawa ya babu wasipone wanaambiwa hawana imani. Wanaokufa njiani wakielekea huko wanaambiwa Mungu kapanga kifo chao, wanaotokea mahospitanili wakiwa hoi kuelekea huko wakafa baada ya kunywa kikombe wanaambiwa wangebaki hospitalini maana wanaumwa sana. I just cant understand why would almost the whole country believe in such a blatant deception!!!
 

No wonder jina lako ni GALAGALAUKA, haliko mbali sana na GAGULA. Amelaaniwa kwao kivipi, inaonekana huko kwenu ndio watu wanaachiana laana ovyo. Kuwa na busara kijana.
 
Kama kweli wanaopata kikombe cha Babu wanapona ni vyetu vya kabla na baada ndivyo vinavyoweza kuthibitisha.
 

pole ila pia wakati wake wa kufa ulifika. hata angekunjwa arvs angefikia mwisho tu.
kwa wale wanaodhani kupona na kuendeleza dhambi inakula kwao.
watu kufa wanakufa tu hata kama sio kwa babu. kila siku wanafia kwenye mabenchi kabla hawajawaona madaktari. huko vijijini ndo usiseme kabsaaaa. afu mi naona hakuna wa kumlaumu maana kila mtu anakwenda there kwa UTASHI WAKE MWENYEWE. alielazimishwa aseme hapa eebo.kama vipi kila alielazimishwa ampeleke aliemlazimisha polisi akajibu tuhuma.
 

kuna mama mmoja inaesadikiwa ndie wa kwanza kunywa kikombe tangu mwaka jana. alikua na hali mbaya ila baada ya kikombe aliendelea na ARVs hadi pale daktari alipomwambia aache maana SD4 zake ziliongezeka sana tu. so nadhani si suala la leo kikombe kesho bila arvs. bi mkubwa wetu anatumia ARVs ingawa alikunywa kikombe na maendeleo yake ni mazuri kwa kweli. alikua hali na mara zote kila wiki anaugua hiki au kile. sasa naona yuko stable anakula vizuri na apetite iko juu. kuchokachoka kumekwisha. hope next month akihudhuria clinic SD4 zitakua zinapanda.
 
Sasa kama Mungu anakuponya kwa nini akambie uendelee na dawa za Hospitali? Yesu alivyoponya watu aliwaambia endeleeni kwenda Hospitali kuchukua dawa?
 

umeyaona eeh???

yaani visingizio haviishi kiasi kwamba hata dhana nzima ya uponyaji hakuna tena! cha ajabu ukipona hawasemi kuwa siku ya kupona ilifika, wala hawasemi Yesu alikuponya bali wanasema ulikuwa na imani juu ya kikombe cha babu (na si kwa Yesu) au utasikia mashabiki wakijipiga vifua na kusema "babu kiboko" !!!

hawa watu tuwape dawa gani wafungue macho? naona hata tukiwagwia fimbo nyeupe kwa upofu huu haitawasaidia

Sasa kama Mungu anakuponya kwa nini akambie uendelee na dawa za Hospitali? Yesu alivyoponya watu aliwaambia endeleeni kwenda Hospitali kuchukua dawa?

hahah, huu uponyaji unachekesha sana.

eti kama unaendelea kutumia dawa nyingine usisitishe dozi baada ya kikombe! ukinywa kikombe na ukasitisha kutumia dawa kama zamani unakufa. si aseme tu kikombe na imani juu ya kikombe pekee havina uwezo wa kutibu?

uponyaji gani huu? mungu anayeponya kwa mseto wa ARVs, na kikombe, mungu gani huyu? kwa kweli Mungu na atufungue macho wapendwa. wengi tunaangamia kwa kukosa maarifa

nyinyi mmekuwa safi kwa sababu ya lile neno
basi zaeni matunda ya heri
 

huyu babu kawaweza sana wajuaji wa kitanzania.....naona katika hii tiba uchwara ya huyu babu CCM na CHADEMA hata tofauti zao wamesahau!kila sehemu babu babu!.....kwa style hii mimi hajanikamata!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…