Usichukie kumuona Hersi kwenye matukio makubwa ya klabu

demigod

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
8,292
Reaction score
15,250
Kuna hasira ambayo Eng Hersi Saidi anawasababishia mno watu kwa kuonekana kwenye kila tukio kubwa la Klabu.

Muonekano wake unasababisha kero na chuki hasa kwa wale wasio #WANANCHI.

Kama wewe ni mmoja wao, basi utachukizwa naye kwa muda mrefu sana.

Yanga SC wanaendesha klabu yao kwa namna ambayo timu kubwa. Za Spain. Zinaendesha timu zao.

Rais wa Klabu ndio anakuwa uso wa kibiashara na haiba kwa klabu. Yanga walijifunza hili kutoka kwa Wakufunzi wao Sevilla. Ni jambo jipya ndio maana linawakera wengi mno walio katika tasnia ya soka la Tanzania. Hawajazoea kuona mambo mapya.

Wengi mna mfahamu Fiorentino Perez lakini mtendaji mkuu wa Real Madrid hamumfahamu (labda ugugo ivi sasa)

Wengi mna mfahamu J. Laporta wa Barcelona lakini mtendaji mkuu wa Barca hamumfahamu (labda ugugo ivi sasa).

Yes wamechagua kuendrsha klabu yao kisasa zaidi.


Sisi simba bado hatujafikia hatua hiyo kubwa. Ndio maana kila mtu kwenye klabu yetu anajiitia ovyo ovyo waandishi wa habari. Yaani kiufupi hakuna utaratibu kama walio nao wenzetu Yanga.

Tusipo kubali kubadilika na kutamani kuwa. Kama yanga sc basi siku zote tutamuonea wivu Eng Hersi Said na Yanga SC yao!
 
Wenzenu sio tu matukio bali hata viongozi wakubwa wa FIFA wanawatambua na wanakaa meza moja kupiga stori kama mtu na swahiba wake.
 
Nasikia rais amepoka job description ya mtendaji. Yaani ni yale yale yaliyomshinda senzo hahaaa.
 
Labda wewe ndio unachuki
 
Mimi nadhani Raisi huwezi fanya kazi zote za club zilizo mbele yako ili tu uonekane na mashabiki..ukifanya kila kitu unapunguza ufanisi ..sasa wewe Raisi ukafanye scouting wewe, usajli, mikataba na negotiations, migogoro, kusafiri huko na huko kwa mambo ya timu etc....Raisi unatakiwa hasa uconcentrate na mambo makubwa na vision za kujenga club.
 
CEO kaona club inaendeshwa kiswahili swahili na yeye kasepa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…