Usijiroge ukasema nataka Maparachichi ya Juice, utajuta

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
Habari yenu wakuu,

Nmependa nitumie jukwaa hili kutoa angalizo moja ambalo nina ushuhuda nalo.

Mara nyingi watu hupenda kwenda Sokoni kununua Matunda kwaajili ya kutengeneza Juice majumbani kwao. Na ukifika pale Sokoni swali utakalokutana nalo ni:

Unataka matunda ya juice au ya kula Kawaida?

Hili swali wengi huwa wanajichanganya. Wanasema nipe matunda ya juice.

Ukifika nyumbani wakati wa kutengeneza ndo unaipatapata. Sababu matunda yote yaloharibika ndo utawekewa. Siku nmenunua matunda pale Buguruni nliipatapata. Sirudii tena.

Hivyo basi usithubutu kukutwa unaagiza matunda ya juice.

Mwenzenu nmetubu
 
Hahaa pole sana,ndo tabia zao wauzaji wa matunda. Mie pia ilishanitokea
 
Hiyo picha sio yenyewe takuletea OG, between umenikumbusha nyanya za salo kariakoo na huko buguruni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…