Usijizuie kuelewa hatifungani/bond za Serikali

Mwakawasila

Member
Joined
Oct 23, 2024
Posts
23
Reaction score
20
HATIFUNGANI/BOND/AMANA

Ni aina ya dhamana inayotolewa na serikali au kampuni kwa lengo la kukopa fedha. Mkopaji anaweza kuwa serikali au kampuni na anaekopesha ni mwekezaji.

Mwekezaji anaponunua hatifungani, anaikopesha serikali au kampuni fedha yake kwa kipindi flani cha makubaliano.

Serikali au kampuni humlipa mwekezaji riba (isiyobadilika) kila mwaka kwa kipindi chote cha mkopo.

Baada ya kipindi kufika ukomo, mwekezajI hurudishiwa hela aliyowekeza mwanzoni.

Kuna hatifungani za aina mbili; Hatifungani za serikali na Hatifungani za makampuni.

ILA TUTAANGAZIA HATIFUNGANI ZA SERIKALI

FAIDA ZA HATIFUNGANI ZA SERIKALI

1. Uhakika wa Mapato: Hatifungani za serikali zinajulikana kwa kuwa na uhakika wa mapato.

Riba inayotolewa na hatifungani hizi ni kiasi ambacho hakibadiliki na kinajulikana hivyo inafanya hatifungani za serikali kuwa chaguo kwa wawekezaji wanaotafuta mapato ya uhakika.

2. Usalama: Hatifungani za serikali mara nyingi zinachukuliwa kuwa na kiwango cha chini cha hatari kuliko uwekezaji wa hisa au hatifungani za makampuni.

Hii ni kwa sababu serikali ni ngumu sana kutokulipa fedha kwa wawekezaji.

3. Hatifungani za serikali zinaweza kuuzika na ukarudishiwa fedha yako kabla ya kipindi Kuisha

4. Hatifungani za serikali zinaweza kutumika kama dhamana kuchukulia mkopo kwenye taasisi za kifedha kama benki.

Hatari za hatifungani za serikali*

1. Mwekezaji anaweza asirudishiwe riba au kiasi chake cha uwekezaji endapo serikali itashindwa kulipa mkopo huo.

Hatari hii huwa ni ndogo sana na hutokea kwa nadra sana hasa kwenye nchi zilizojaa malimbikizo makubwa sana ya madeni au uchumi kuyumba kwa kasi sana.

Kwa Tanzania, serikali haijawahi kutokuwalipa wawekezaji wa hatifungani za serikali hata mara moja.

Kwa hiyo usiwe na shaka

JINSI YA KUSHIRIKI KWENYE MNADA WA HATIFUNGANI ZA SERIKALI*

1.Fungua akaunti ya uwekezaji (BOT CDS ): Ili kufungua akaunti hii mwekezaji anatakiwa aambatanishe vitu vifuatavyo.

a. Picha 3 za passport
b. Copy ya TIN certificate
c. Copy ya kitambulisho cha taifa

2. Baada ya kuhakikisha viambatanisho vinavyohitajika, mwekezaji anatakiwa Kujaza fomu ya kufungua akaunti ya uwekezaji.

3. Akaunti ikiwa imeshafunguliwa hatua inayofata, mwekezaji anabaini aina ya hatifungani anayotaka (miaka 2, 5, 7,10,15,20 na 25)

pamoja na tarehe ya mnada wa hatifungani iliyochaguliwa kupitia kalenda inayopatikana kwenye tovuti ya Benki kuu ya Tanzania (BOT)

4. Mwekezaji anatakiwa Kujaza bid application form ambayo ataiwasilisha ofisini Kwa wakala aliyemchagua kwenye soko la hisa na kusubiria matokeo ya mnada huo

5. Matokeo hutolewa jioni ya siku ya mnada ambayo hutokana na bei ambayo mwekezaji amejaza kwenye form.

Mwekezaji anapaswa kufanya malipo siku ya kazi inayofuata. Ambayo malipo hayo hufanywa kupitia benki anayotumia muwekezaji.

6. Kiwango cha chini cha kuwekeza ni TZS millioni 1.

*Ikiwa unataka kuuza hatifungani ulionunua kabla haijafika ukomo wake(maturity), wasiliana WAKALA uliye mchagua kwa msaada Zaidi.


Mfano wa jinsi unavyoweza kupata FAIDA

Mfano wa milioni arobaini 40,000,000
Ukiwekeza ambayo utapata interest ya 15%

Tupate asilimia 15% ya 40,000,000

40,000,000÷100=400,000 ni laki nne

Zidisha Kwa 15×400,000=6,000,000 milioni 6 Kwa mwaka

Hiyo milioni 6 zidisha mara miaka 20

6,000,000×20=120,000,000 milioni mia moja ishirini

Hiyo ni faida unakuwa umezalisha Kwa miaka 20 Kwa mtaji wa milioni 40

Siku Miaka 20 ikiisha unapewa milioni 40 yako kama ilivyo

Ukipata Hela kubwa usifanyie matumizi wekeza alafu tumia

Hizo uliyowekeza kama amana ya kukopea mkopo


Kwa hiyo faida ndo inalipa deni lako

Kwa masomo zaidi unaweza I save no yangu

(255744980339) Whatsap and normal
 
mfano wa Mawakala ni Kina Nani?.
Utaratibu wa Malipo upoje ? Je ni baada ya miezi sita au Mwaka?.

Naomba kujua
 
Mawakala Hawa wapo zaidi ya 20 mojawapo Kuna ZAN SECURITY,ORBIT SECURITY,SOLOMON, EXODUS

NA bank za kibiashara
 
NAomba uingeze nyama ktk maelezo yko uliosema kuwa iyo bond inaweza kuwa dhamana ya kukopea mkopo
 
NAomba uingeze nyama ktk maelezo yko uliosema kuwa iyo bond inaweza kuwa dhamana ya kukopea

Si unajua utaratibu wa taasisi nyingi za kifedha unapenda kukopa LAZIMA uwe na amana au Mali ya kuweka inaweza kuwa nyumba,Ardhi na nk

Ili utakaposhindwa kulipa waiuze

Kwa hiyo ukiwa na HATIFUNGANI/BOND inakuwa ni dhamana yako

Utasubmit taarifa zako unakopeshwa Hadi asilimia 80% ya pesa yako iliyopo bond

FAIDA nyingine ni wepesi wa kupata mkopo unaweza pata mkopo Kwa wiki moja Hadi mbili

Wakati kama unaweka nyumba ni zaidi ya mwezi,

Bila shaka no mekujibu mkuu
 
Je interest ambayo inapatikana kila mwezi naweza kuichukua?
 
Je interest ambayo inapatikana kila mwezi naweza kuichukua?
Kwa mwaka unapewa mara 2 ikiwa na maana Kama ni 10000 interest baada ya miezi 6 unapewa 5000p

Na mwisho wa mwezi wa 6 Tena unapewa 50000
 
HATIFUNGANI/BOND/AMANA

Ni aina ya dhamana inayotolewa na serikali au kampuni kwa lengo la kukopa fedha. Mkopaji anaweza kuwa serikali au kampuni na anaekopesha ni mwekezaji.

Mwekezaji anaponunua hatifungani, anaikopesha serikali au kampuni fedha yake kwa kipindi flani cha makubaliano.

Serikali au kampuni humlipa mwekezaji riba (isiyobadilika) kila mwaka kwa kipindi chote cha mkopo.

Baada ya kipindi kufika ukomo, mwekezajI hurudishiwa hela aliyowekeza mwanzoni.

Kuna hatifungani za aina mbili; Hatifungani za serikali na Hatifungani za makampuni.

ILA TUTAANGAZIA HATIFUNGANI ZA SERIKALI

FAIDA ZA HATIFUNGANI ZA SERIKALI

1. Uhakika wa Mapato: Hatifungani za serikali zinajulikana kwa kuwa na uhakika wa mapato.

Riba inayotolewa na hatifungani hizi ni kiasi ambacho hakibadiliki na kinajulikana hivyo inafanya hatifungani za serikali kuwa chaguo kwa wawekezaji wanaotafuta mapato ya uhakika.

2. Usalama: Hatifungani za serikali mara nyingi zinachukuliwa kuwa na kiwango cha chini cha hatari kuliko uwekezaji wa hisa au hatifungani za makampuni.

Hii ni kwa sababu serikali ni ngumu sana kutokulipa fedha kwa wawekezaji.

3. Hatifungani za serikali zinaweza kuuzika na ukarudishiwa fedha yako kabla ya kipindi Kuisha

4. Hatifungani za serikali zinaweza kutumika kama dhamana kuchukulia mkopo kwenye taasisi za kifedha kama benki.

Hatari za hatifungani za serikali*

1. Mwekezaji anaweza asirudishiwe riba au kiasi chake cha uwekezaji endapo serikali itashindwa kulipa mkopo huo.

Hatari hii huwa ni ndogo sana na hutokea kwa nadra sana hasa kwenye nchi zilizojaa malimbikizo makubwa sana ya madeni au uchumi kuyumba kwa kasi sana.

Kwa Tanzania, serikali haijawahi kutokuwalipa wawekezaji wa hatifungani za serikali hata mara moja.

Kwa hiyo usiwe na shaka

JINSI YA KUSHIRIKI KWENYE MNADA WA HATIFUNGANI ZA SERIKALI*

1.Fungua akaunti ya uwekezaji (BOT CDS ): Ili kufungua akaunti hii mwekezaji anatakiwa aambatanishe vitu vifuatavyo.

a. Picha 3 za passport
b. Copy ya TIN certificate
c. Copy ya kitambulisho cha taifa

2. Baada ya kuhakikisha viambatanisho vinavyohitajika, mwekezaji anatakiwa Kujaza fomu ya kufungua akaunti ya uwekezaji.

3. Akaunti ikiwa imeshafunguliwa hatua inayofata, mwekezaji anabaini aina ya hatifungani anayotaka (miaka 2, 5, 7,10,15,20 na 25)

pamoja na tarehe ya mnada wa hatifungani iliyochaguliwa kupitia kalenda inayopatikana kwenye tovuti ya Benki kuu ya Tanzania (BOT)

4. Mwekezaji anatakiwa Kujaza bid application form ambayo ataiwasilisha ofisini Kwa wakala aliyemchagua kwenye soko la hisa na kusubiria matokeo ya mnada huo

5. Matokeo hutolewa jioni ya siku ya mnada ambayo hutokana na bei ambayo mwekezaji amejaza kwenye form.

Mwekezaji anapaswa kufanya malipo siku ya kazi inayofuata. Ambayo malipo hayo hufanywa kupitia benki anayotumia muwekezaji.

6. Kiwango cha chini cha kuwekeza ni TZS millioni 1.

*Ikiwa unataka kuuza hatifungani ulionunua kabla haijafika ukomo wake(maturity), wasiliana WAKALA uliye mchagua kwa msaada Zaidi.


Mfano wa jinsi unavyoweza kupata FAIDA

Mfano wa milioni arobaini 40,000,000
Ukiwekeza ambayo utapata interest ya 15%

Tupate asilimia 15% ya 40,000,000

40,000,000÷100=400,000 ni laki nne

Zidisha Kwa 15×400,000=6,000,000 milioni 6 Kwa mwaka

Hiyo milioni 6 zidisha mara miaka 20

6,000,000×20=120,000,000 milioni mia moja ishirini

Hiyo ni faida unakuwa umezalisha Kwa miaka 20 Kwa mtaji wa milioni 40

Siku Miaka 20 ikiisha unapewa milioni 40 yako kama ilivyo

Ukipata Hela kubwa usifanyie matumizi wekeza alafu tumia

Hizo uliyowekeza kama amana ya kukopea mkopo


Kwa hiyo faida ndo inalipa deni lako

Kwa masomo zaidi unaweza I save no yangu

(255744980339) Whatsap and normal
Asante sana kwa elimu nzuri juu ya uwekezaji. Haya mambo kwa Watanzania walio wengi ni mageni hivyo elimu bado inahitajija sana.
 
Back
Top Bottom