Usikate simu mapema...

Snipes

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2013
Posts
9,165
Reaction score
16,791
pale unapomaliza kuongea na simu usipende kuwa wa kwanza kukata simu kwa sababu kuna matusi ambayo unatukanwa ila kwa kiherehere chako unawahi kukata, unakuta mtu anakuambia, huyu fala kakosa watu wa kuwapigia, huyu mjinga anamalizia dk zake kwangu, mijitu mingine ovyo, acha kimbele mbele

[HASHTAG]#WapostPumba[/HASHTAG]
 
umenikumbusha kuna msichana jirani yangu akiongea na cm. ile inaita tu
utasikia huyu mbwa anampigia nani. akipokea sasa anavyoongea, laiti ningekuwa ndo mimi ningempigia nahisi na Number ningefuta siku hiyo hiyo. akikata ndo anamtusi balaa.
 
Ngoja basi niwe na kinyumenyume..kimbelembele nakiacha leo
 
Huwa nakata simu nikipiga ila nikipigiwa huwa sina mchezo huo.
 
umenikumbusha kuna msichana jirani yangu akiongea na cm. ile inaita tu
utasikia huyu mbwa anampigia nani. akipokea sasa anavyoongea, laiti ningekuwa ndo mimi ningempigia nahisi na Number ningefuta siku hiyo hiyo. akikata ndo anamtusi balaa.
Dah!!umenikumbusha kuna siku nilimupigia demu wangu fulani hivi.

Sasa wakati tunaongea maongezi yetu yalikuwa poa sana tu.

Ile tunaangana hivi sikukata simu muda ule yeye akajua kuwa simu nimeikata.

Uwiiiii!!kwanza nilisikio bonge la tusi na msonyo juu.
 
ulichukua hatua gani??
 
Mi mwenyewe ni mmoja kati ya watu wanaomaliza kupokea simu kwa matusi, yaani simu ya mtu yeyote lazima nimalize na tusi kama "huyu jamaa ms***e, mambo ya kis***e au sitaki mambo ya kis***e mimi" isipokuwa labda watu wa home tu[emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…