USILE NYAMA SIKU YA IJUMAA KUU, WANGAPI TUMEKUNYWA SUPU ASUBUHI??

USILE NYAMA SIKU YA IJUMAA KUU, WANGAPI TUMEKUNYWA SUPU ASUBUHI??

Mgeni wa Jiji

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2017
Posts
9,758
Reaction score
18,431
Ndio nakumbuka leo ni Ijumaa ile tunayoiita Ijumaa kuu yenye amri, Usile nyama siku ya Ijumaa kuu.

Just imagine ndio uko na mning'inio wa ziada 'hangover' na umeambiwa usile tu nyama siku zote kama ya leo Ijumaa kuuView attachment 729110
 
Ndio nakumbuka leo ni Ijumaa ile tunayoiita Ijumaa kuu yenye amri, Usile nyama siku ya Ijumaa kuu.

Just imagine ndio uko na mning'inio wa ziada 'hangover' na umeambiwa usile tu nyama siku zote kama ya leo Ijumaa kuu
C&P
Habari za leo wapendwa wangu katika Kristo.
Kuna kitu kinaitwa mapokeo katika madhehebu yetu. Madhehebu yetu huwa yana mapokeo. Sina maelezo mazuri sana kueleza nini maana ya mapokeo. Lakini kwa maelezo marahisi mapokeo ni taratibu za ibada na namna ya kuenenda katika kanisa. Mapokeo ni desturi za madhehebu. Kila dhehebu huwa lina desturi na taratibu zake. Taratibu hizi pamoja na imani ndizo zinazotofautisha madhehebu duniani.
Ndo maana kuna madhehebu mengine hawali baadhi ya vyakula si tu katika pasaka bali wakati wowote. Au hawanywi baadhi ya vinywaji fulani wakati wowote. Lakini si kwamba wale wanaokula vyakula hivyo watenda dhambi au hao wasiokula ni wadhaifu katika imani. La hasha. "Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato....Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani, Msishike, msionje, msiguse; (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu? Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili" - Kol 3:16-20
Kwa hiyo wapendwa tusiwakwaze wale wasiokula au wale wanaokula nyama katika Ijumaa kuu ya sikukuu ya pasaka au siku iwayo yote.
Nami siko tayari ndugu yangu aingie huzuni kwa sababu ya chakula, nitakuwa nimeacha kwenda katika upendo. Kwa chakula changu sitaki nimharibu mtu yule ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake pale msalabani.
Kwa ajili ya chakula sitaki niiharibu kazi ya Mungu. Maana vyote ni safi; bali ni vibaya kwa mtu alaye na kujikwaza. Ni vyema kutokula nyama wala kunywa divai wala kutenda neno lo lote ambalo kwa hilo ndugu yangu hukwazwa. Ile imani niliyo nayo nafsini mwangu mbele za Mungu. Paulo asema "Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali. Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi" - Rum 14:22,23
Amani ya Kristo na iwe nawe
10155335_631894333552654_613698806508049189_n.jpg
 
Dah....nyama siyo chakula chenye maana sana kwenye mwili wa mwanadamu..... Kisayansi gramu 40 zinamtosha MTU kwa siku 7....yaani kilo 1 iliwe na watu 25 kwa wiki ...yaani ukiwa na wageni 100 wakakaa kwako kwa siku 7 bas kilo 4 tu za nyama zinawatosha kabisa[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Nani kasema watu wasile nyama?
Nini msingi wa katazo hilo?

Kama mtu hajala nyama toka mwaka huu uanze, basi leo ndio siku nzuri zaidi ya kutafuna nyama kisawa sawa.
 
Mkuu hangover yangu lazima niitoe kwa supu....kwa hyo supu kwangu ni kama dawa,ndio naelekea toroka uje kupata supu ya utumbo na ndiz za kuchemsha
 
Ndio nakumbuka leo ni Ijumaa ile tunayoiita Ijumaa kuu yenye amri, Usile nyama siku ya Ijumaa kuu.

Just imagine ndio uko na mning'inio wa ziada 'hangover' na umeambiwa usile tu nyama siku zote kama ya leo Ijumaa kuuView attachment 729110

Ukila nyama inakuwaje? Mbona Ijumaa nyingine ninakula nyama. Kwanza Ijumaa zenyewe zinahamahama, hivyo Ijumaa kuu ya mwaka jana ikawa Ijumaa ya kawaida ya mwaka huu kwa kuzingatia kalenda, ingawaje utofauti ni ukuu.
 
Ukila nyama inakuwaje? Mbona Ijumaa nyingine ninakula nyama. Kwanza Ijumaa zenyewe zinahamahama, hivyo Ijumaa kuu ya mwaka jana ikawa Ijumaa ya kawaida ya mwaka huu kwa kuzingatia kalenda, ingawaje utofauti ni ukuu.
Mkuu, waambie tu waelewe, mtu alhamisi anapiga mecgi za ugenini na mchepuko, af ijumaa kuu ndo anaanza swaga za kutokula nyama. 😝
Ttz ukamilifu hatuutafuti kwa kufanya yaliyosemwa ktk biblia, ila kwa yale yaliyosemwa na kanisa ndo tunajidai kuyaelewaaaa! 😝 😝 😝
 
Mimi nyama nakula kama kawa wapeleke huko UJINGA wao.
Hapa nimetoka kupata supu safiii na chapati mbili
 
Back
Top Bottom