Usilete mbwembwe kwenye Harusi; utalia

Usilete mbwembwe kwenye Harusi; utalia

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
USILETE MBWEMBWE KWENYE HARUSI, UTALIA.

Na, Robert Heriel

Leo Taikon sitakuwa na maneno mengi maana kuna wadau wangu hupenda ndizi kisukari, hupenda fupi fupi.

Haya, usilete mbwembwe kwenye Harusi tadhani wewe ndio mtu wa Kwanza kufanya Harusi, utalia.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa mahari ulitoa Kwa mbinde😜😜 Kama ulibargain na Wakwe usije ukaleta mbwembwe zako za kipuuzi.
Tutakuwa tunakuchora tuu Sisi Wakwe zako. Utalia baadaye.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa Harusi yenyewe umekamua watu na tumichango ya kushikana mashati. Utalia.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa Bibi Harusi uliyemuoa hujaikuta bikra. Ex za mke wako tunakudere tuu unavyoshongondoka. Utalia baadaye, utake usitake.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa unajua kabisa bila mundende ganzi mujarabu huwezi kumridhisha Bibi Harusi wetu. Utachapiwa, wewe jichekeleshe na suti yako.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa unajua kabisa huna maajabu ya viuno feni, mwanamke hujafundwa ukafundika hujui A wala Ba za chinua Achebe kwenye sebene la seremala. Utaletewa mke mdogo.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi wakati Harusi yenyewe imefungwa Kwa mbinde, mtu mpaka umegombana na rafiki kisa kukuchangia.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa unajijua Una Mkono wa birika, hujui kumhudumia Mkeo. Wadhamini waliokudhamini Harusi yako ndio hao hao watakaokusaidia majukumu ya ndoa.

Ukifika kwenye ukumbi wa sherehe ya Harusi yako.

Cheza Kwa staha, usiruke ruke Kama njeree ya makaa, Kama ni Bibi Harusi cheza Kwa maringo ya staha, macho yako yawe ya aibu muda mwingi yawe chini sio ung'aze macho huku na huko Kama Askari anayetafuta washukiwa wa dawa za kulevya.

Kama ni Bwana Harusi, cheza ki-gentlemeni. Usirushe rushe miguu, wala usikate mauno Kama mwehu.
Usilete mbwembwe, utagongewa, ulie Kama Mbuzi meee baadaye.

Muda wa kula, Kula Kwa adabu, usichote lisahani likajaa machakula mengi Kama mlafi. Kula chakula huku ukitafakari michango ya wote waliokuja ukumbini. Tafuna huku ukisema; mchango! Mchango! Mchango! Kimoyo moyo.

Sio unatafuna Kwa sifa mbele ya watoa michango, watu wanakudere, wanasubiri sherehe iishe.

Harusi haihitaji mbwembwe, Harusi inahitaji utulivu, burudani zenye staha.

Sio upigie watu kelele na mbwembwe zisizo na maana, nakuhakikishia kadiri unavyoleta mbwembwe ndivyo utakavyolia Kama Mbuzi.

Anyway nilisema sitaandika pakubwa. Niishie hapa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
 
Ulete mbwembwe au usilete mbwembwe kama niku chapiwa utachapiwa tu. Kitu chochote kinachokupa furaha kwa wakati husika usisite kukifanya .life is too short na hakuna formular ya kufanikiwa kimahusiano au kwenye ndoa
 
Ulete mbwembwe au usilete mbwembwe kama niku chapiwa utachapiwa tu. Kitu chochote kinachokupa furaha kwa wakati husika usisite kukifanya .life is too short na hakuna formular ya kufanikiwa kimahusiano au kwenye ndoa

Zingatia usilete mbwembwe.
Ukikaidi sawa
 
Nimeipenda na Amini uandish wako ht hip-hop unaweza andika mistari
 
Niliwahi hudhuria harusi Bwana harusi kajaza sahani ya Ubwabwa balaaah, Basi wakati wa kula anapiga tonge mpaka anajifuta jasho Tena kwa mkono. Kanzu yote na Jamvi vimeloa Jasho.
 
Nimependa hapo cheza kwa staha mana kuna maharusi sijui ndo furaha sana ama vipi?

Niliwahi ona video Bibi na Bwana harusi wamepagawa mpaka wanataka wafanye ya chumbani pale ukumbini mana si kwa mpapasano na mabusu yale na hapo ilikuwa ni kucheza muziki tu. Lol.
 
Niliwahi hudhuria harusi Bwana harusi kajaza sahani ya Ubwabwa balaaah, Basi wakati wa kula anapiga tonge mpaka anajifuta jasho Tena kwa mkono. Kanzu yote na Jamvi vimeloa Jasho.

😂😂😂😂😂
 
Nimependa hapo cheza kwa staha mana kuna maharusi sijui ndo furaha sana ama vipi?

Niliwahi ona video Bibi na Bwana harusi wamepagawa mpaka wanataka wafanye ya chumbani pale ukumbini mana si kwa mpapasano na mabusu yale na hapo ilikuwa ni kucheza muziki tu. Lol.

😂😂😂

Wanaleta mbwembwe mbele za Wakwe na Ma-Ex
 
USILETE MBWEMBWE KWENYE HARUSI, UTALIA.

Na, Robert Heriel

Leo Taikon sitakuwa na maneno mengi maana kuna wadau wangu hupenda ndizi kisukari, hupenda fupi fupi.

Haya, usilete mbwembwe kwenye Harusi tadhani wewe ndio mtu wa Kwanza kufanya Harusi, utalia.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa mahari ulitoa Kwa mbinde[emoji12][emoji12] Kama ulibargain na Wakwe usije ukaleta mbwembwe zako za kipuuzi.
Tutakuwa tunakuchora tuu Sisi Wakwe zako. Utalia baadaye.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa Harusi yenyewe umekamua watu na tumichango ya kushikana mashati. Utalia.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa Bibi Harusi uliyemuoa hujaikuta bikra. Ex za mke wako tunakudere tuu unavyoshongondoka. Utalia baadaye, utake usitake.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa unajua kabisa bila mundende ganzi mujarabu huwezi kumridhisha Bibi Harusi wetu. Utachapiwa, wewe jichekeleshe na suti yako.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa unajua kabisa huna maajabu ya viuno feni, mwanamke hujafundwa ukafundika hujui A wala Ba za chinua Achebe kwenye sebene la seremala. Utaletewa mke mdogo.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi wakati Harusi yenyewe imefungwa Kwa mbinde, mtu mpaka umegombana na rafiki kisa kukuchangia.

Usilete mbwembwe kwenye Harusi ikiwa unajijua Una Mkono wa birika, hujui kumhudumia Mkeo. Wadhamini waliokudhamini Harusi yako ndio hao hao watakaokusaidia majukumu ya ndoa.

Ukifika kwenye ukumbi wa sherehe ya Harusi yako.

Cheza Kwa staha, usiruke ruke Kama njeree ya makaa, Kama ni Bibi Harusi cheza Kwa maringo ya staha, macho yako yawe ya aibu muda mwingi yawe chini sio ung'aze macho huku na huko Kama Askari anayetafuta washukiwa wa dawa za kulevya.

Kama ni Bwana Harusi, cheza ki-gentlemeni. Usirushe rushe miguu, wala usikate mauno Kama mwehu.
Usilete mbwembwe, utagongewa, ulie Kama Mbuzi meee baadaye.

Muda wa kula, Kula Kwa adabu, usichote lisahani likajaa machakula mengi Kama mlafi. Kula chakula huku ukitafakari michango ya wote waliokuja ukumbini. Tafuna huku ukisema; mchango! Mchango! Mchango! Kimoyo moyo.

Sio unatafuna Kwa sifa mbele ya watoa michango, watu wanakudere, wanasubiri sherehe iishe.

Harusi haihitaji mbwembwe, Harusi inahitaji utulivu, burudani zenye staha.

Sio upigie watu kelele na mbwembwe zisizo na maana, nakuhakikishia kadiri unavyoleta mbwembwe ndivyo utakavyolia Kama Mbuzi.

Anyway nilisema sitaandika pakubwa. Niishie hapa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
Sasa Mr. Robert, huoni kama itapoteza ladha? Yaani nisiruke kweli? Nisile nikashiba? Nisitafune kwa raha zangu kweli? Haaaaah!
 
Sasa Mr. Robert, huoni kama itapoteza ladha? Yaani nisiruke kweli? Nisile nikashiba? Nisitafune kwa raha zangu kweli? Haaaaah!

Kazi wedding maid ndio hiyo kunogesha sherehe,
Kazi ya MC ndio hiyo kuchangamsha Sherehe
Kazi ya Dj ndio hiyo kuburudisha ukumbi Kwa Muziki.

Maharusi mnasherehekea Kwa heshima kwani ninyi ndio wageni rasmi siku hiyo.

Harusi hupoteza ladha kama maharusi wakijigeuza washehereshaji badala ya washehereshwaji
 
Nimependa hapo cheza kwa staha mana kuna maharusi sijui ndo furaha sana ama vipi?

Niliwahi ona video Bibi na Bwana harusi wamepagawa mpaka wanataka wafanye ya chumbani pale ukumbini mana si kwa mpapasano na mabusu yale na hapo ilikuwa ni kucheza muziki tu. Lol.
Alafu najiulizaga...pale wakati wa harusi hivi bwana harusi anawezaje kutokudindisha wakati anajua kabisa leo naenda kisasambua mbususu
 
Alafu najiulizaga...pale wakati wa harusi hivi bwana harusi anawezaje kutokudindisha wakati anajua kabisa leo naenda kisasambua mbususu
Ni ma control tuu mzee wangu ...

Kikubwa usilete mbwembwe......
 
Back
Top Bottom