Usimchukie mumeo kwa kuwa hajaokoka!

Huyo mwanamke anafanya makosa, yeye anachotakiwa ni kumwombea mumewe na kuonesha tabia na matendo mema huyo mwanamume ataokoka mwenyewe bila kupigiwa kelele. Nimeona wanawake ambao wameokoka na waume zao hawajaokoka lakini wanaishi kwa amani na mwishoe mwanaume anaamua kuokoka. Mimi naamini kua kuokoka ni neema toka kwa MUNGU si jambo la kumlazimisha ni mpaka nuru ya Bwana imwangazie si kwa maneno ya ukali.
 
Mie hawezi kunibalasa coz huwa namwazima flash ya gospal songs na leo nimepata nyimbo mpya ndio gia ya kuingilia hiyo kwa vile ndio ugonjwa wake atanasa tu,
Yani ni aibu tupu kwa mumewe,na wale wapendwa wenzie ndio wamemshawishi ahame chumba kwan etu kuna maandiko yanawaagiza kujitenga na mataifa,yani hata wakiwa wanakuja pale kwake jamaa anatafuta pa kwenda kuepusha maneno ya ajabu kutoka kwa waumin wenzie na mkewe.
Na sio siri huko tuendako na hii kasi ya makanisa ya kilokole yanayoota km uyoga ukilinganisha na hayo mafundisho yao sijui nn kitatokea.
 

Naomba muelewe kua hapo awali huu uamsho ulipoanza ulokole ulionekana kama namna fulani ya kujitenga sana hasa pale biblia inaposema "tokeni kati yao mkatengwe nao" watu walipokea vibaya andiko hili kwani mtu alipookoka alitamani kuhama nyumbani kwao, waliokuwa shuleni walitamani kuacha shule kwa mtazamo ambao si mzuri...
Kwako wewe unayekwenda kuongea na mwanandoa huyu inabidi usiongee nae kwa jazba bali muelimishe kuwa hata biblia inasema "Na, kama mwanamke Mkristo anaye mume asiyeamini, na huyo mwanamume akakubali kuendelea kuishi naye, basi, asimpe talaka mumewe." - 1 Wakorintho 7:13
Kwa ushauri zaidi sikilizeni Wapo Radio Fm (98.0) kila jumapili kuanzia saa nne kamili hadi saa tano kamili usiku na jumatatu saa sita kamili hadi saa saba kamili mchana

Ubarikiwe
 
Asante sana mpendwa,
Hakika hapa umenirahisishia kazi yangu kwa mhusika huyu,
Nakushukuru sana,ubarikiwe pia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…