Usiniache kilimo!!

xfactor

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2014
Posts
1,511
Reaction score
1,289
Heshima zenu nyingi sana wakuu

Kwanza nianze kwa kumshukuru Mungu aliyeniongoza mpaka nikajiunga JF hasahasa hili jukwaa letu tukufu maana nimejifunza mengi japo mengi yamenipita sababu wadau mmeshaweka hadi kempu za kilimo,nahisi kupitwa sana.Pili niwashukuru wote wenye moyo wa kutoa taarifa ili wengine wajifunze.

Nije kwenye mada yangu.Baada ya takribani mwezi sasa wa kupitia threads mbalimbali za kilimo humu ndani nimehamasika na kudhamiria kuingia kwenye kilimo,taarifa ni nyingi sana ambazo zimetolewa hivyo imeniwia vigumu kufanya maamuzi ya zao gani nianze nalo,matarajio ya huu uzi kuleta harmonization ya taarifa hizi ili watu wapate mwanga wa kilimo gani cha kuanza nacho.

Baada ya kusoma maoni nikajifunza kuwa kuna factor kuu zifuatazo ambazo natakiwa kuzingatia kabla sijachagua zao la kuanza nalo,mtanikosoa kama nitakuwa sipo sahihi:
1. kufanya kilimo sehemu ambayo nitaweza kufika mara kwa mara,kwa maana iwe karibu na dar mfano: chalinze,kibaha,mkuranga,mlandizi,Ruvu,bagomoyo ili iwe rahisi kusimamia sababu naishi Dar

2. Kufanya kilimo ambacho hakihitaji maji sana maana mvua haziaminiki au kama kitakuwa cha kuhitaji maji basi eneo liwe na mto au water table iwe karibu kwa ajili ya visima

3. Upatikanaji wa masoko

Kama nilivyosema awali taarifa ni nyingi mno humu maana kila mtu analima kitu tofauti,Hivyo lengo langu ni kutaka msaada wa yafuatayo
1. kulingana na factors zangu mbili hapo juu, je ni zao gani ambalo lina soko na limaweza kustawi maeneo hayo na wapi naweza kupata taarifa kamili kuhusu zao hili? Kwa maana ya kuandaa shamba,mahitaji ya utunzaji shamba na masoko
2. Mtaji wa kilimo cha hilo zao ni kiasi gani roughly achilia mbali gharama za kununua ardhi
3. Wapi specifically miongoni mwa hayo maeneo naweza kupata eneo ambalo lipo karibu na mto au water table ipo karibu,na bei zinaendaje?

Naamini huu uzi utawasaidia na wengine kama mimi ambao wamekuwa wakiwaza waanze na kilimo kipi.


Natanguliza shukurani wakuu
"Shika elimu ila usimuache kilimo aende zake"
 
1.unapozungumzia convenience ya kufika shamba nadhani inategemea whether unatumia public transport au personal.shambani kwangu 160km along morogoro road nafika mapema zaidi kuliko shamba lingine kisarawe 100km.pia naweza panda basi na nikatembea kwenda shamba. Pia kumbuka prices the mashamba zinategemea umbali kutoka dar
2.maeneo uliyotaja zao linaloweza kulimwa na likakupa manufaa ya haraka ni tikiti maji.waweza lina ufuta pia kwa maeneo mengine.pia passion zinastawi vizuri.zijui gharama za uzalishaji za hayo mazao mengine ila tikiti kama unalima kwa tractor gharama zote ikiwa ni pamoja na dawa,kupanda na kupalilia ni about 120k,that is kama unategemea mvua.kwa umwagiliaji sina uzoefu ila tikiti huhitaji maji mengi week za mwanzo.soko generally lipo dar lakini wanunuzi huja shamba kutegemea ni rahisi kiasi gani kufika huko.
 
Nashukuru mkuu kwa response yako,naomba nikusumbue tena kwa swali
Huko kwako bado maeneo yanapatikana na gharama zikoje?

 
Heshima kwako mkuu xfactor
kama umeamua kuzama katika kilimo, factor ya umbali iweke kwanza kando isipokuwa tu-kikubwa ni uhakika wa kutoa mazao yako hadi sokoni kiurahisi.
Kuna mdau mkuu humu anaitwa Malila natumai umemsoma vzr ktk pitapita zako kwenye jukwaa hili pendwa! Huyu jamaa amezunguka almost all over the country kutafta maeneo mazuri kwa kilimo na ufugaji.
Ningekushauri tuwasiliane ili nikuuzie shamba zuri ambalo hutajutia kutoa hela yako.
Karibu sana.
 
Last edited by a moderator:
Mdau Malila nampata vilivyo sana na natumaini atauona huu uzi naye anipe maoni kama malafyale hapo juu.Utaipata PM yangu soon,natumaini wewe sio mtu wa kati

 
Last edited by a moderator:
Mdau Malila nampata vilivyo sana na natumaini atauona huu uzi naye anipe maoni kama malafyale hapo juu.Utaipata PM yangu soon,natumaini wewe sio mtu wa kati

Asante wadau,

Zao la kuanza nalo linategemea plan zako na uchumi wako, kwa sababu huwezi kuanza na minazi wakati hutavuna kesho wakati huo huo huna kipato kingine. Lakini waweza kuotesha minazi kama una plan ya kuja kufanya kilimo kingine ktk shamba hilo miaka kumi ijayo( hii ni case yangu niliyofanya), pengine kwa sasa una shughuli nyingine.

Kama unataka kujenga mtaji kwa kutumia kilimo, basi anza na mazao ya muda mfupi yenye soko la uhakika kama matunda,mboga na mifugo, kisha muda wa kati. Wakati unafanya haya ya muda mfupi, anza kuwekeza ktk mazao ya muda mrefu, huku ukiangalia uwezekano wa kufungua kiwanda cha kusindika mazao.

Mkuu, kama uko Dar, basi tafuta eneo zuri kubwa, anza bustani ya mboga mboga, na ufanye kisayansi. Nimeshauri mboga mboga kwa sababu soko linaanzia kwa mlalahoi mpaka kwa mafisadi, cha msingi ubora wa mboga zako tu.
 
A kilimo bila pesa ni sawa na kujamba ktk Maji ya bahari .mm nimekodi na kununua ardhi mpaka Leo hela ya kulimia nimeshindwa kupata .bank naogopa kukopa maana kilimo hakina uhakika naona hivi pesa zangu zimepotea nilikuwa na lengo la kupanda Ufuta na mahindi na muhogo nipeni ushauri wadau
 
Nimekupata mkuu,nafikiri kuanza kidogo kwanza ndio jambo la msingi sana ili nipate na uzoefu wa namna ya kusimamia shamba.Nafikiri nitaanza na mbogamboga na matunda huku nikiwa na lengo la kufanya mazao ambayo nimeshauriwa na mkuu Malafyale in future

 

Kilimo ni kazi kama kazi nyingine na ni biashara kama biashara nyingine yeyote sasa huwezi anza kazi bila elimu au biashara bila ya mtaji!!!!!!!

Weka details zaid utapata mawazo ila suala la mtaji katika kilimo lipo tu kutegemea unataka kilimo cha aina gani na ukubwa wa ardhi unayofanyia kazi!!!!!!

Kama una muda pitia mashamba ya wengine ujifunze kwa kuona!!!!!!
 
Mdau xfactor nasubiri mlejesho wako kule PM.
Hapa kinachotakiwa ni umakini katika kuchagua ni zao litakupa tija katika kipindi kipi na uhitaji wake kwenye soko. Binafsi simshauri mtu abase kwenye biashara ya mbogamboga japo ni kweli haibagui wahtaji wake, ila madhara yapo hasa kwenye supply baada ya kuanza mavuno utajikuta unapambana na watu wa chini ambao ni wengi sana na wamelishikilia soko na ukisema kuwa upambane nao utaumia hawaogopi hasara wale! Hapa nina maana kuwa ogopa kujihusisha kwenye biashara ambayo mpinzani wako ktk soko anaifanya ili kukidhi mahtaji yake ya kila siku i.e watoto wapate mlo wa siku!
Ningewashauri wakulima- wajasiriamali mwaka huu walime kwa wingi mazao kama FIWI NYEUSI,DENGU,UFUTA,ALIZETI,KUNDE,CHOROKO,KARANGA na mazao yote jamii ya mikunde yatakuwa na soko zuri sana. Hii ni kwasababu mnunuzi mkubwa ni WAHINDI na WAARABU, watahtaji wanunue kwa wingi ili wawe na stock kubwa kuhofia uchaguzi wa 2015 ambapo kama kwaida yao hubana hela mwaka wa uchaguzi.
 
Last edited by a moderator:

Ndg ndo umeandika nn sasa! Kabla hujafanya kitu chochote jipe muda wakutafakari kwa umakini cz ht kz yakuajiriwa ucpotulia unafukuzwa so Lazima kujipanga!
 
Ndg maestro naona umeshindwa kabla hujaanza! Kilimo ni km kz yakuajiriwa ucpoifanya kwa umakini utafukuzwa! Unapojiingiza kwenye KILIMO lazima akili itulie hasa unapotaka kujua ni Zao gani unataka kulima! Pamoja na ushauri 2naopena japa lkn ni vyema ww mwenyewe ukajipa Homework yakutosha 7bu ww ndo utakuwa fld Tatizo nnalo liona wengi we2 tufanya mambo kwa kufuata mkumbo dat Y badae 2nalaumu!
 


Sio kweli, unaweza anza na nguvu zako mwenyewe, hata kwa kulima kwa jembe la mkono ni jitihada kubwa sana, Unaweza anza hata na Robo ya Robo heka, na baadae ukapanua, Kua na shamba tu kwamba umekosa pesa sio jitihada, jitihada ni wewe kuanza, ni sawa na wale wanao sema wana mawazo ila hawana pesa,

Anza na ulicho nacho hata Vitani watu huenda na mawe, wengine hubeba fimbo na wengine hubeba bunduki, ukikosa bunduki beba hata mawe, na unaweza vizia adui mwenye bunduki ukampa ya kichwa na kubeba bunduki yake na kusonga mbela, nazani umenielewa.
 

Ni kweli sana,nimeona watu wengi humu wanasukumwa kwa mkumbo sababu tu wanaambiwa na kuonyeshwa picha za mafanikio ya wale waliokwisha tangulia kwenye kilimo,ila wanasahau kuwa inahitajika tafakari kubwa.

Ila nakubaliana na Vaccum kwenye swala la masoko,hasa ya mbogamboga japo kuna kitu kimoja ambacho tunapaswa kujua,sidhani kwamba kuna zao ambalo halina changamoto ya masoko,na mbaya zaidi katika thread nyingi humu hili swala halizungumzwi kwa kina kwahiyo cha msingi ni kuingia mtaani mwenyewe na kujua namna ambavyo utapata soko baada ya kuchagua zao utakalo anza nalo

Mimi binafsi nimechagua mbogamboga na matunda kama zao la kuanzia sababu sina uzoefu na usimamizi kabla sijaenda kwenye kilimo kikubwa.kwa mantiki hii nimeshaanza kufikiria namna ya kupambana na hao wachuuzi wadogo wa mboga na matunda,na target yangu mimi itakuwa hoteli na migahawa(nauza wazo hapa bure),sinza ina hoteli nyingi na mjini posta kuna migahawa ya kutosha pia so nitadili na hao.

"Dawa ya changamoto ni kupambana nazo na si kuzikwepa maana utakutana nazo tena mbeleni"
 


Uko sahihi kabisa kaka hapo kwenye masoko ni suala la kuvamiana tu in real sense sababu huwezi pata soko lako peke yako na hata ukilipata watu wakigundua wata attempt kukutoa tu!!!!!

Cha maana ni kujua soko linataka nini na nini kipo sokoni na kina mapungufu au ubora gani then unafanyia kazi hayo mapungufu ya bidhaa zilizopo sokoni ili wewe uje na kitu tofauti!!!!
 
Km umeamua kushughulikia Mbogax2 na matunda ni wazo Jema cha muhimu kabla hujaanza Kulima anza kutafiti Soko ili ujue SOKO linataka nini Manake ma2nda yako aina nyingi pia Mboga so nimuhmu kujua B4 ili uckwame ni mbaya kuanza kulima kisha utafute Soko ndomana wengine wanatukana KILIMO!
 

Noted with thanks brother.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…