Usiruhusu ukaribu uliopitiliza kati ya mwenza wako na marafiki zako (mashemeji)

Usiruhusu ukaribu uliopitiliza kati ya mwenza wako na marafiki zako (mashemeji)

RIGHT MARKER

Senior Member
Joined
Apr 30, 2018
Posts
129
Reaction score
473
Mhadhara wa 27:
Ukaribu uliopitiliza kati ya Mwenza wako na marafiki zako ni hatari sana. Ukaribu wa marafiki zako kwa Mwenza wako ukipitiliza mambo huwa hivi.

1. Leo wanaitana "shemeji"

2. Kesho wataitana "shemu"

3. Keshokutwa wataitana "meji"

4. Mtondogoo wataitana "shemu darling"

5. Siku inayofuata wataitana "tunakulaga"

Kamwe usiruhusu ukaribu uliopitiliza kati ya Mwenza wako na marafiki zako (mashemeji zake). Wezi wengine huibuka kwa sababu ya mali iliyoachwa sehemu nyeupe. Hata kama nyumba yako ni imara hupaswi kuacha milango wazi, usimwache mwizi aibe mali yako kirahisi.

USIRUHUSU:
1. Usiruhusu Mwenza wako kusafiri mara kwa mara umbali mrefu na rafiki yako.

2. Usiruhusu Mwenza wako kwenda Lunch na rafiki yako mara kwa mara bila uwepo wako.

3. Usiruhusu mawasiliano ya karibu ya simu kati ya rafiki yako na mwenza wako (wanachati mpaka simu inakuwa ya moto).

4. Usiruhusu rafiki yako awe hakimu wa kudumu wa kusuluhisha kesi za wewe na Mwenza wako. Pia rafiki yako asiwe daktari wa kutibu upweke wake.

5. Usiruhusu Mwenza wako ajue kuwa kila unapokwama kifedha, sponsor wako mkubwa ni rafiki yako.

Je, ni kitu gani kingine kisiruhusiwe?

Right Marker
Dar es salaam
Oktoba 1, 2024
 
Haya Mambo ya kulana ni kawaida sana sema tu sijui kwanini hamzoei hadharani...wakati gizani mwaweza kula hadi binamu zenu
Popote alipo mwanamke na nwanaume hasa katika mazingira ya peke yao pia shetani yupo kati yao anachochea vishawishi vya zinaa.

Haya ulioandika ni kweli kabisa. Marafiki waishie kukuona ukumbini tu Tena bila kuonana na mkeo.
 
Unafiki unawasumbua. Lol
cocastic mpenz....the way gays wanavyotupiwa mawe hadharani....huwezi amini % ya wanaume kamili na gays Tanzania huenda ni 50/50 aisee....Tena wavaa suti,wenye misuli, gentlemen,wafanya ibada,wameoa,wanaaminika katika jamii....dunia imekuwa uwanja wa hovyo sana aisee
 
Michepuko ya mwenzio ni ndugu zake wa karibu sana ama marafiki zako wa karibu sana
 
Haya Mambo ya kulana ni kawaida sana sema tu sijui kwanini hamzoei hadharani, wakati gizani mwaweza kula hadi binamu zenu.
Mwanaume kuchapiwa ni maumivu makali sana na hii ni kwa kiasi kikubwa inatokana na tofauti ya uwekezaji baina ya mwanamke na mwanaume katika mahusiano.

Mwanaume ndie anaingia gharama za ku-maintain mahusiano, na anafanya ivyo akiwa na matarajio ya kupewa utiifu na uaminifu in return.

Tafuta kijana mmoja wa kiume mhudumie kila kitu kuanzia chakula, mavazi, makazi, bata ndogo ndogo n.k halafu siku uje kugundua anaku-cheat uone kama utakua na mtazamo huo huo kwamba kulana ni kawaida.
 
Back
Top Bottom