Mh..nini tena WL jamani, tuwekee hapa tujue na upande wa ...mmh!
mwanzo ahadi huwa nyingi smtyms huambatana na machozi,,,,baadae ukikumbushia inasaidia kwa wiki 1 then mambo yanakuwa yaleyale,,naona iko very seasonal though it can work out,,thx
Naomba niwape uzoefu wangu kidogo.
Nakumbuka nilikutana na Mpenzi wangu maeneo ya bustani ya Nyerere (Nyerere Square) nikiwa kwenye mapumziko yangu ya jioni. Hapa ndipo nilipotoboa "Ozone Layer" na kumwambia yaliyojaa moyoni mwangu
Nakumbuka nilimwambia nampenda sana na hakuna mwanamke alieuvutia moyo wangu kama yeye na kama akikubali ombi langu sitavutika na mwanamke mwingine zaidi yake.
Nilimwambia nitamfanya kuwa mwenye furaha kila siku na sitakoma kumpenda. Nilimwambia nitampa nafasi ya kumsikiliza katika tofauti zetu
Tulipanga mipango yetu ya maisha.
Tunavyotumia mwanzo wetu: Kila siku lazima anikumbushe tuliyoongea mwanzo. Nami namkumbusha tuliyoongea mwanzo.
Kama ikitokea kuna jambo seroius na halifai kuzungumza home, huwa namchukua tunakaa kwenye kiti kile kile ambacho tulikutana siku hiyo (wakazi wa Dom ni kiti karibu na mtende unaotazamana na CRDB Bank) kisha tunaongea na kukumbushana ahadi zetu na umuhimu wake.
Ni mahali pa muhimu kwetu na hata yeye mwenyewe amekuwa akijua umuhimu wake.
Kila tukikutana hapa huwa kama vile ndio tunaanza moja!! Pana historia ya muhimu sana kwenye penzi letu kuliko maeneo ya historia ya Tanzania wala maeneo mengine makubwa na maarufu. Kila mara tunapatamani hapa kuliko hata mbuga za serengeti wala kubembea Jamaika
dah mi nilikutana na wangu kwnye daladala mwenge/mbagala (nilikua nashuka ilala) hlf daladala ilikua shazi km kawaida y dcm za huko.wote 2likua 2mecmama mzee mzima nikatema sumu palepale.na mimi cku nikimpeleka 2lipokutana c itakua balaa
Wewe ChweChwe wewe, mbona hii ya kwako balaa?
Ila pamoja na kukutana kwenye daladala nauhakika kuna mahali baada ya hapo mlikutana as your first meeting point na kujadiliana juu ya mahusiano yenu kwa undani zaidi. That is the place...hii ya kwenye daladala hii mmhmhhhh!!
Mkuu huo mtende naufahamu. Nilishakaa pale kusubiri foleni ya ATM