Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363
Daktari mmoja aitwaye Abuu aliingia hospital kwa
haraka baada ya kupigiwa simu kuwa alitakiwa
kwa
ajili ya operesheni ya haraka sana.Moja kwa moja
bila kupoteza muda Dr Abuu aliingia katika
chumba
cha
upasuaji.Akamwona baba wa kijana aliyetakiwa
kufanyiwa upasuaji akiwa katika chumba cha
kusubiria. Baada ya kumwona Dr Abuu baba wa
kijana alipiga kelele huku akimfuata na
kumwambia:
Kwa nini umechukua muda mrefu kuja? Haujui
kuwa mtoto
wangu angeweza kufa? Una chembe ya
ubinadamu wewe au kwako vifo ni ufahari?
Abuu alitabasamu na kumwambia Yule baba:
Sikuwa hapa hospital ila baada ya kupigiwa simu
nimekuja haraka kama nilivyoweza Nakuomba
samahani na uwe mpole nifanye kazi mara moja
Niwe mpole?! Ungekuwa wewe ndio mimi na
mototo wako anataka kufa na daktari anakuambia
uwe mpole ungekuwa mpole? Aliongea baba Yule
akiwa na hasira za kutisha.
Daktari Abuu alitabasamu tena na kumjibu mzee
yule: Nitasema maneno yaliyopo kwenye kitabu
kitakatifu Tuliumbwa kwa mavumbi na tutarudi
mavumbini, Jina la bwana libarikiwe. Daktari
hawezi
kurudisha Maisha ya mtu bali kwa neema zake
bwana. Mwanao atapona kwa jina la bwana.
Huwezi kunipa ushauri wakati wewe sio
mwajibikaji
hivyo huna maana Aliongea baba kwa hasira
Upasuaji ulichukua masaa kadhaa na baadae
daktari
Abuu akafungua mlango na kutoka akiwa na uso
wenye furaha na kumwambia baba Ashukuriwe
Mungu mtoto wako kapona na bila kupoteza
muda
Abuu akaondoka kabla ya Yule mzee hajadadisi
zaidi.
Mbona huyu daktari mkorofi sana, yaani hata
kabla
sijamaliza kuuliza kaondoka? Aliuliza yule mzee
kwa
nesi aliyekuwa pembeni yake.
Nesi akamjibu huku machozi yakimtoka: Mtoto
wa
daktari huyu alipata ajali na kufa jana, Alikuwa
nyumbani akijiandaa kwenda kumzika,Na kwa
kuwa hakuna daktari wa tatizo hilo zaidi yake basi
tukampigia ndio akaja mara moja na sasa
anawahi
kwenda kumzika mwanae.
Funzo :
Usiwe mwepesi wa kuhukumu .. kwa sababu
huwezi jua wenzako ni kwa nini wako na hali
unazoziona zikiwaandama au watu wanapitia
Maisha
ya namna gani wakijitahidi kukufanya wewe uwe
na
furaha na amani.
haraka baada ya kupigiwa simu kuwa alitakiwa
kwa
ajili ya operesheni ya haraka sana.Moja kwa moja
bila kupoteza muda Dr Abuu aliingia katika
chumba
cha
upasuaji.Akamwona baba wa kijana aliyetakiwa
kufanyiwa upasuaji akiwa katika chumba cha
kusubiria. Baada ya kumwona Dr Abuu baba wa
kijana alipiga kelele huku akimfuata na
kumwambia:
Kwa nini umechukua muda mrefu kuja? Haujui
kuwa mtoto
wangu angeweza kufa? Una chembe ya
ubinadamu wewe au kwako vifo ni ufahari?
Abuu alitabasamu na kumwambia Yule baba:
Sikuwa hapa hospital ila baada ya kupigiwa simu
nimekuja haraka kama nilivyoweza Nakuomba
samahani na uwe mpole nifanye kazi mara moja
Niwe mpole?! Ungekuwa wewe ndio mimi na
mototo wako anataka kufa na daktari anakuambia
uwe mpole ungekuwa mpole? Aliongea baba Yule
akiwa na hasira za kutisha.
Daktari Abuu alitabasamu tena na kumjibu mzee
yule: Nitasema maneno yaliyopo kwenye kitabu
kitakatifu Tuliumbwa kwa mavumbi na tutarudi
mavumbini, Jina la bwana libarikiwe. Daktari
hawezi
kurudisha Maisha ya mtu bali kwa neema zake
bwana. Mwanao atapona kwa jina la bwana.
Huwezi kunipa ushauri wakati wewe sio
mwajibikaji
hivyo huna maana Aliongea baba kwa hasira
Upasuaji ulichukua masaa kadhaa na baadae
daktari
Abuu akafungua mlango na kutoka akiwa na uso
wenye furaha na kumwambia baba Ashukuriwe
Mungu mtoto wako kapona na bila kupoteza
muda
Abuu akaondoka kabla ya Yule mzee hajadadisi
zaidi.
Mbona huyu daktari mkorofi sana, yaani hata
kabla
sijamaliza kuuliza kaondoka? Aliuliza yule mzee
kwa
nesi aliyekuwa pembeni yake.
Nesi akamjibu huku machozi yakimtoka: Mtoto
wa
daktari huyu alipata ajali na kufa jana, Alikuwa
nyumbani akijiandaa kwenda kumzika,Na kwa
kuwa hakuna daktari wa tatizo hilo zaidi yake basi
tukampigia ndio akaja mara moja na sasa
anawahi
kwenda kumzika mwanae.
Funzo :
Usiwe mwepesi wa kuhukumu .. kwa sababu
huwezi jua wenzako ni kwa nini wako na hali
unazoziona zikiwaandama au watu wanapitia
Maisha
ya namna gani wakijitahidi kukufanya wewe uwe
na
furaha na amani.