Usongo wangu na kiswanglishi : Watanzania hatujakomaa kilugha- 1

Usongo wangu na kiswanglishi : Watanzania hatujakomaa kilugha- 1

Dingswayo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
4,019
Reaction score
2,925
Ni juzijuzi hapa ambapo tumeshudia Rais wa China akiongea kwa lugha yake, wakati Rais wetu anaongea Kiingereza. Hotuba hizo zilifaa wananchi wote wazielewe kupitia lugha yao ya Kiswahili. Viongozi wengi wanachanganya Kiswahili na Kiingereza wakiongea na wananchi, na vile vile televisheni zetu pia zinarusha habari watu wanaongea Kiingereza bila kuweka maneno ya kutafsiri. Mitaani kwetu napo limekuwa jambo la sifa kusikika mtu anachanganya lugha hizo, eti ni kuonekana kuwa ameendelea au amesoma! Tatizo ni kuwa wengi ambao wanaochanganya lugha hizo hawazijui zote vizuri. Ili uweze kuwa mjuzi wa lugha fulani inabidi uweze kuongea lugha kwa ufasaha.

Mwandishi Freddy Macha naye pia ana usongo kama wangu. Soma zaidi hapa:

MAKALA ZANGU: USONGO WANGU NA KISWANGLISHI : WATANZANIA HATUJAKOMAA KILUGHA- 1
 
[B said:
Freddy Macha[/B]] "....Nimetathmini sera hiyo ya Waingereza ili kuongelea suala la Ki-Swanglish ambacho kinaendelea kuzaa chawa Tanzania"....

Hii imejieleza vizuri siona hata cha kuongeza hapa, Ahsante kaka Macha
 
Back
Top Bottom