Ustaarabu wabongo bado?

Ustaarabu wabongo bado?

Mundu

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2008
Posts
2,707
Reaction score
642
Nimekuwa mkazi wa Dar kwa muda mrefu na nimekuwa nikishuhudia vipindi mbalimbali vya maisha ya wakazi wake kwa namna ya pekee. Tabia za wananchi hawa au wakazi wa Dar hazitabiliki kiasi cha kushindwa kujua mkazi huyu ata'behave' vipi katika matukio mbalimbali.

Kwa mfano, utaona mkazi huyo akifika kwenye mashine ya kuchukua fedha yaani ATM, atapanga foleni na zamu yake ikifika anaingiza kadi yake na kuendelea na shughuli yake pale. Hapa amekuwa mstaarabu kamili. Lakini huyu huyu mkazi akiwa anaendesha gari na kama kuna kafoleni kadogo basi utamwona anachepuka na kuanza kula service road ili yeye awahi, kana kwamba wale wote aliowakuta kwenye foleni hawana haraka labda au hawajui kutumia magari yao vizuri. Na kwa kitendo chake hicho anaweza akasababisha foleni kubwa zaidi. Hapa ustaarabu wote aliouonyesha kwenye ATM anauvua kabisa. Mkazi huyo huyo atanunua chungwa, akimaliza asitafute sehemu ya kutupia takataka, atatupa ganda la chungwa barabarani, tena sehemu ambayo ni wazi, imesafishwa na wafanya kazi ambao hulipwa kwa ajili hiyo ili kuweka mji, hususani barabara zetu katika hali ya usafi. kwanini ustaarabu wa mkazi huyu hautabiriki? Hapa ana'behave' hivi, pale anakuwa tofauti kabisa kiasi cha kuleta usumbufu kwa wengine??
 
usitupakazie, sisi hatujawa wakenya. si rahisi hapa bongo mtu kudandia foleni bank au kwenye ATM. labda, hapo kwenye atm au bank, ungesema kuwa, mtu anajifanya kamwekea mwenzie foleni, yeye anasimama afu anakuja amechelewa anamwambia mtu aliyeko mbele achukua kadi yake akamchukulie hela, labda ni kaka yake au dada yake, sasa pale anakuwa anadandia foleni kimtindo.
 
mundu...ustaarabu kwa wabongo bado sana.Idd pili hapa mwanza nilikwenda Beach moja safi sana sehemu ya Nyegezi nikiwa na mama yangu ,mke wangu na majirani zangu.Tulikuta ile resort imejaa wabongo wanaogida pombe na wengine wakitoleana maneno ya matusi ya nguoni hadi kufikia kurushiana makonde.Kwa kawaida mtu kuingia pale unahitaji kibali cha mwenye ile resort kwa sababu bado haijakuwa fully opened for business.

Mara ghafula likaja gari limesheheni mapolisi na wakaanza kuwaondoa wote amabo hawakufuata taratibu za kuingia kwa ruksa.

Bwana weee...tulikutana na matusi makubwa mno ya kibaguzi kwa kuwa wengine tume mix uarabu na uswahili.Wacha tutukanwe...na wakorofi hao.Kitu ambacho hawakujua pale nilikuwa na wajomba zangu na mama na wale majirani wote walikuwa Watanzania wenye ngozi nyeusi.

Tulipumua baada ya wakorofi hao kuondolewa na kusema kweli wale waliobaki beach walikuwa wengi ni ngozi nyeusi ukiondoa wachache ambao walikuwa na uhindi na uarabu.

Sasa hii ni nini? Ustaarabu hakuna.watu wengine wanadhani ukija beach starehe ni kunywa pombe na kufanya ubabe.

niliwaambia wenzangu kuwa Dar afadhali wamestaarabika ukienda beach hakuna mambo kama yaliyotusibu huko Nyegezi beach.

Kumbe nako bado!!!
 
Labda tunahitaji darasa la ustaarabu toka kwa wazungu. Maana hata viongozi wetu wanaoukumbatia ufisadi ni kielelezo cha kukosa ustaarabu. Iweje mtu mmoja ajilimbikizie mali nyingi kwa jasho la watanzania wakati wananchi wengi wako katika lindi la umaskini mkubwa? Ni kukosa ustaarabu nako.
 
kwanza waaangalie hao viongozi wetu wanato yafanya tarime na kwengineko ambao wao ndio kioo chetu sasa baba hivyo jee mtoo jee?
 
kwanza waaangalie hao viongozi wetu wanato yafanya tarime na kwengineko ambao wao ndio kioo chetu sasa baba hivyo jee mtoo jee?

kuna mengi, kama kuchokonoa pua hadharani au ndani ya bunge letu, kukojoa hovyo barabarani n.k. Bongo bado sana!
 
Back
Top Bottom