Usugu malaria ni janga la wasomi feki

Usugu malaria ni janga la wasomi feki

kibaravumba

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
6,634
Reaction score
7,015
Wengi mnaofanya kazi za tiba,mtakubaliana nami kuwa Malaria imekuwa sugu kwa dawa zilizopendekezwa na wizara ya Afya Tanzania.Pamoja na ukweli huu kujulikana,hakuna tafiti za maana kuhusu tiba ya dawa nyingine inayoweza kutumika hapa nchini.Wasomi wetu wanasubiri Makampuni ya wazungu wakishirikiana na wahindi waje na pendekezo jipya kwa ajili ya majaribio ndipo utawaona jopo la wale wanaoitwa madaktari na wafamasia wakiwa channel ten asubuhi wakijidai kuelezea dawa hizo za majaribio kama kwanba walikuwepo wakati zinaandaliwa!Kwanini ninyi hamfanyi tafiti bali mnamwachia Ndodi na wenzake?Halafu baadae mnakuja kuwaponda akina Babu wa Loliondo!Hivi hili ni jukumu la nani kati yenu madaktari na wafamasia?Mmebaki kuuza dawa kwenye maduka yenu tu bila kujua kuwa sisi raia tunasumbuka sana na usugu wa malaria.Tuambieni mnafanya utafiti au tufanye wenyewe?

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
kibaravumba

- Una uhakika hakuna Tafiti zenye manufaa kuhusu ugonjwa wa Malaria zilizokwisha fanywa hapa na zinazoendelea kufanywa hapa Nchini?
-Kwa ushahidi/sababu zipi unaweza kututhibitishia kuwa hakuna tafiti na Wataalamu wa Afya husubiri "wazungu na wahindi" tu kwa tafiti?
- Ni wangapi hufuatilia matokeo ya Tafiti zinazofanyia (achilia mbali zinapotangazwa, kuhamasishwa kupitia vituo vya Afya hadi hospitali?)

Endapo hata hutambui kuna tafiti zilishafanyika, utaanzaje kufanya utafiti?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom