KERO Usumbufu kwa Wananchi wa Mbezi Beach-Jogoo Kwa Kerai (kwa mzee Temu) jijini Dar kutokana na baa inayopiga Muziki mkubwa usiku

KERO Usumbufu kwa Wananchi wa Mbezi Beach-Jogoo Kwa Kerai (kwa mzee Temu) jijini Dar kutokana na baa inayopiga Muziki mkubwa usiku

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
IMG-20240814-WA0015.jpg


Maelezo ya Tatizo:

Ndugu wanajamii, napenda kufichua tatizo kubwa linaloendelea hapa Mbezi Beach-Jogoo barabara ya Kerai (kwa Mzee Temu) ambapo baa moja imekuwa ikipiga muziki mkubwa mno usiku kucha, hali inayoathiri kwa kiasi kikubwa maisha ya wananchi wanaoishi karibu na eneo hilo.

Baa hiyo, ambayo iko karibu sana na makazi ya watu, inapiga muziki mkubwa mpaka usiku wa manane na wakati mwingine hukesha kabisa. Hali hii imekuwa kero kubwa kwa sisi wakazi wa eneo hili, hasa kwa watoto na wazee ambao wanahitaji kulala kwa utulivu ili waweze kuamka na nguvu siku inayofuata.

Hatua Zilizochukuliwa:

Tayari tumesharipoti tatizo hili kwa serikali za mitaa mara kadhaa, lakini hadi sasa hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa. Tunahisi kama haki zetu za msingi za kupumzika na kuishi kwa amani zinapuuzwa.

Athari:

Tatizo hili linaathiri kwa kiasi kikubwa afya zetu na uwezo wetu wa kufanya kazi kwa ufanisi. Kutolala usiku kunasababisha uchovu, msongo wa mawazo, na kushusha viwango vya uzalishaji.

Wito Wangu:

Naomba msaada kwenu JamiiForums kuibua suala hili ili mamlaka husika zichukue hatua stahiki. Ni muhimu kwa baa kama hii kuheshimu sheria na haki za wananchi kwa kupunguza kelele au kuweka sauti kwa kiwango kinachokubalika.
 
Hio baa imeanzishwa mwaka huu kama sikosei na iko mita chache tu kutoka ofisi ya serikali za mtaa
 
View attachment 3070245

Maelezo ya Tatizo:

Ndugu wanajamii, napenda kufichua tatizo kubwa linaloendelea hapa Mbezi Beach-Jogoo barabara ya Kerai (kwa Mzee Temu) ambapo baa moja imekuwa ikipiga muziki mkubwa mno usiku kucha, hali inayoathiri kwa kiasi kikubwa maisha ya wananchi wanaoishi karibu na eneo hilo.

Baa hiyo, ambayo iko karibu sana na makazi ya watu, inapiga muziki mkubwa mpaka usiku wa manane na wakati mwingine hukesha kabisa. Hali hii imekuwa kero kubwa kwa sisi wakazi wa eneo hili, hasa kwa watoto na wazee ambao wanahitaji kulala kwa utulivu ili waweze kuamka na nguvu siku inayofuata.

Hatua Zilizochukuliwa:

Tayari tumesharipoti tatizo hili kwa serikali za mitaa mara kadhaa, lakini hadi sasa hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa. Tunahisi kama haki zetu za msingi za kupumzika na kuishi kwa amani zinapuuzwa.

Athari:

Tatizo hili linaathiri kwa kiasi kikubwa afya zetu na uwezo wetu wa kufanya kazi kwa ufanisi. Kutolala usiku kunasababisha uchovu, msongo wa mawazo, na kushusha viwango vya uzalishaji.

Wito Wangu:

Naomba msaada kwenu JamiiForums kuibua suala hili ili mamlaka husika zichukue hatua stahiki. Ni muhimu kwa baa kama hii kuheshimu sheria na haki za wananchi kwa kupunguza kelele au kuweka sauti kwa kiwango kinachokubalika.
Mziki hauleti msongo wa mawazo sema kwa wanafunzi hawezi kusoma na wazee pia kero cha kukusaidia Uza hapo kanunue MLANDIZI KIWANJA CHA MILLIONI 6 UJENGE HAPO SIO RAFIKI KWAKO pashachangamka
 
Hili swala la ujengaji holela wa open bar kwenye maeneo ya karibu na makazi ya watu limekuwa kero ya kudumu mpaka imefika mahali tunaona ni jambo la kawaida, bar za wazi hazipaswi kupiga mziki kama night club, na zinapaswa kuwa na muda maalumu wa kufunga (haipaswi kuwa kero kwa watu wengine) lakini Sisi binadamu wa ulimwengu wa tatu swala la ustaarabu na kuheshimu privacy za watu wengine sio shida zetu kabisa.

Mamlaka zipo kimya na zinajionea sawa tu, nchi za wenzetu hata ikitokea jirani yako anapiga mziki mkubwa wa kukera wengine unaruhusiwa kupiga 911.


Ngoja tuone kama mamlaka husika itafanya jambo katika hilo, poleni.
 
Mziki hauleti msongo wa mawazo sema kwa wanafunzi hawezi kusoma na wazee pia kero cha kukusaidia Uza hapo kanunue MLANDIZI KIWANJA CHA MILLIONI 6 UJENGE HAPO SIO RAFIKI KWAKO pashachangamka
Na huko Mlandizi pakichangamka?
 
Mziki hauleti msongo wa mawazo sema kwa wanafunzi hawezi kusoma na wazee pia kero cha kukusaidia Uza hapo kanunue MLANDIZI KIWANJA CHA MILLIONI 6 UJENGE HAPO SIO RAFIKI KWAKO pashachangamka
Hapo unaona umemshauri vizuri kweli
 
Tanzania nchi ya kipumbavu sana. Mtu anaamini anakaa sehemu nzuri makazi bora na ya gharama ila inakuja siku panafunguliwa bar/club jirani yake halafu anashindwa kulala na mamlaka hakuna kitu zinaweza kufanya.
Yaani mtu anaishi Masaki au Mbezi Beach lakini usiku anapigiwa kelele za Amapiano kuliko sisi wa Mbagala!
 
Mziki hauleti msongo wa mawazo sema kwa wanafunzi hawezi kusoma na wazee pia kero cha kukusaidia Uza hapo kanunue MLANDIZI KIWANJA CHA MILLIONI 6 UJENGE HAPO SIO RAFIKI KWAKO pashachangamka
Akili hizi ndio unakuta ndio mwenyekiti wa serikali za mitaa.
 
Tanzania nchi ya kipumbavu sana. Mtu anaamini anakaa sehemu nzuri makazi bora na ya gharama ila inakuja siku panafunguliwa bar/club jirani yake halafu anashindwa kulala na mamlaka hakuna kitu zinaweza kufanya.
Yaani mtu anaishi Masaki au Mbezi Beach lakini usiku anapigiwa kelele za Amapiano kuliko sisi wa Mbagala!
Mkuu kazi ya NEMC ni ipi hasa?
 
Hahahahaha biashara inafuata watu ,tegemea biashara kuongezeka na serikali kupata kodi
 
Back
Top Bottom