MAFILILI
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 2,377
- 1,197
Mimi ni mdau wa benki husika ambaye nimeanza kufuatilia mkopo wa biashara kulingana na matangazo yao kuwa wameboresha huduma zao pia muda wa kuomba mkopo umepungua hadi wiki 2 iwapo utakidhi vigezo walivyojiwekea.
Matangazo yao yalinivutia na kuamua kuwasiliana nao kupitia tawi mojawapo jijini Dar Es Salaam. Maajabu baada ya kuwasilisha viambatanisho vilivyohitajika na kutembelewa nyumbani kwangu na sehemu ya biashara, tangia wiki ya mwisho ya Julai 2018 imekuwa ni nenda rudi, hadi nimechoka sijapata mkopo wala OFFER.
Kwa kweli kitengo cha mikopo ACB jijini Dar Es Salaam, wilayani Temeke ni bangua kichwa, maofisa mikopo kwa ujumla hawana ushirikiano kwa wateja wao, pia hawana kauli za kutia moyo na hawapo wazi.
Nawasilisha kwa wadau wenzangu mnipe uzoefu kwa benki zingine ili niachane na ACB!
Matangazo yao yalinivutia na kuamua kuwasiliana nao kupitia tawi mojawapo jijini Dar Es Salaam. Maajabu baada ya kuwasilisha viambatanisho vilivyohitajika na kutembelewa nyumbani kwangu na sehemu ya biashara, tangia wiki ya mwisho ya Julai 2018 imekuwa ni nenda rudi, hadi nimechoka sijapata mkopo wala OFFER.
Kwa kweli kitengo cha mikopo ACB jijini Dar Es Salaam, wilayani Temeke ni bangua kichwa, maofisa mikopo kwa ujumla hawana ushirikiano kwa wateja wao, pia hawana kauli za kutia moyo na hawapo wazi.
Nawasilisha kwa wadau wenzangu mnipe uzoefu kwa benki zingine ili niachane na ACB!