Utafiti: Je, wajua kuosha mdomo ni dawa ya kisonono?

Utafiti: Je, wajua kuosha mdomo ni dawa ya kisonono?

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363

Dawa inayotumiwa kuosha mdomo

Maelezo ya picha,Dawa inayotumiwa kuosha mdomo

Kuosha mdomo kunasaidia kupunguza maambukizi ya kisonono,watafiti wanaamini.
Utafiti wa hivi majuzi umeonyesha kwamba binaadamu wanaweza kubeba magonjwa ya zinaa katika koo zao kwa mda wa wiki moja ama hata miezi bila ya kupata dalili zozote.
Na wanaweza kusambaza kwa wengine kupitia ngono isio salama ya mdomoni.
Wachunguzi wanajaribu kuona iwapo kuosha mdomo mara kwa mara kunaweza kusaidia kuzuia kuenea polepole na wataalam wanasema kuwa ni wazo ambalo linafaa kutumiwa.
Ndani ya koo ya mdomo ndio eneo ambalo bakteria wa kisonono hukaa

Maelezo ya picha,Ndani ya koo ya mdomo ndio eneo ambalo bakteria wa kisonono hukaa
Kisonono husababishwa na bakteria na kinaweza kuishi katika koo,katika uume na uke na husambazwa kupitia ngono ya mdomoni pamoja na ile ya katika uke.
Ugonjwa huo uliokuwa mwingi miaka ya 1950 umepungua baada ya dawa kugunduliwa. chanzo.BBC
 
Back
Top Bottom