UTAFITI KUHUSU UKATILI WA KIJINSIA.

Man Middo tz

Senior Member
Joined
Sep 9, 2020
Posts
182
Reaction score
279
UTAFITI: Asilimia 70 ya vifo vya wanawake duniani vinatokanana ukatili wa majumbani.

Usaliti katika mapenz fedha, chakula na hamu ya mapenzi vimetajwa kuwa miongoni mwa sababu za kuwepo kwa ongezeko la matukio ya ukatili wa majumbani barani Afrika, Huku vyombo vya habari vikinyoshewa vidole kutozipa kipaumbele taarifa za matukio haya.

Hayo yametajwa tarehe 26/07/2019 na Dkt. Dorothy Njoroge katka mkutano wanawake wanaofanya kazi katka vyombo vya habari wa bara la Afrika jijini Nairobi Kenya.

Imeelezwa kuwa asilimia 70 ya vifo vya wanawake barani Afrika vinatoka ukatili majumbani huku ukisababisha vifo, ulemavu sanjari na kutengana kwa watoto, imeelezwa kuwa ni asilimia 6 tu ya wanaume wanaoathirika na ukatili wa majumbani.
_______________________________
Wanawake wengine mnavumilia haya bila kutoa taarifa kwa kuogopa aibu katika mambo haya acheni kufumbia hayo paza sauti yako uokoe wenzako pamoja na familia yako, Sio kila kitu ni cha kuvumilia jamani.

man Middo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…