Utafiti: Madaktari Kusini mwa Sahara huzidisha dawa kwa wagonjwa

Kurzweil

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
6,621
Reaction score
8,411
Utafiti unaonyesha kuwa madaktari wa nchi za kusini mwa Afrika wanatoa dawa nyingi zaidi ya zilizoagizwa na Shirika la Afya Duniani WHO.

Utafiti huo uliofanywa na Chuo kikuu cha London kwa ushirikiano na kituo cha Kutoa ushauri wa afya cha nchini Ghana,ikihusisha nchi kumi na moja za kusini mwa jangwa la Sahara zinaonyesha kuwa wagonjwa wanapewa takribani dawa tatu kila wanapotembelea hospitali, moja zaidi ya maelekezo ya WHO.

Inasemekana tatizo ni baya zaidi kwenye taasisi zinazotengeneza faida, na kuchochea kuuza dawa.

Tafiti zimeonya kuwa matumizi makubwa ya madawa yanasababishwa na kulazimishwa kutumia dawa, kuzidisha dozi na kuleta athari mbaya kwa mchanganyiko unaosababishwa na kuchanganya dawa mbalimbali.

Pia wamegundua wagonjwa wengi wamekuwa wakipewa dawa za kutuliza maumivu pasipo kufanyiwa vipimo, na kuongeza hatari ya maambukizo yanayosababisha na kupambana na dawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…