Uchaguzi 2020 Utafiti unaonyesha baadhi ya majimbo kura za maoni za CCM hazikuwa za siri tena, waliotoa rushwa waliwatisha wapiga kura endapo wasingewachagua

Uchaguzi 2020 Utafiti unaonyesha baadhi ya majimbo kura za maoni za CCM hazikuwa za siri tena, waliotoa rushwa waliwatisha wapiga kura endapo wasingewachagua

budagala

Member
Joined
Jun 11, 2015
Posts
75
Reaction score
137
Baadhi ya wana CCM wamekipaka matope sana chama chetu sababu ya ubinafsi wao. Kilichotokea kwa baadhi ya majimbo husuani Sengerema ni aibu. Mabepari na watoa rushwa hasa jimbo la Sengerema waliwahonga wapiga kura kila kata.

Masharti yalitolewa kwa makatibu kata na viongozi wengine wanapokwenda kupiga kura kwa pamoja sharti waangalie kila mtu kampigia nani kura. Hapakuwa na utaratibu wa siri kuwa mmoja mmoja anaingia kwenye chumba cha kupigia kura na kupiga kura kwa siri. Hii iliwafanya waliopokea rushwa kulazimika kuwaonyesha viongozi wao kura zao wamezipiga kwa nani kama ushahidi.

Inasemekana mwaka flani, bepari mmoja katika jimbo hilo, alitoa sana rushwa lakn hakushinda. Baada ya matokeo akawa anawafuata wote aliowapa pesa na kuwatishia na silaha warudishe pesa zake. Mwaka huu ndo ikabidi strategy ibadilike ya kuzichunga kura. Inasemekana bepari huyo alimfuata hadi Mkurugenzi wa uchaguzi kuomba mwongozo siku moja kabla ya kura kupigwa eti kwa nini CCM imezuia wagombea kusafirisha wapiga kura?

Kwa upeo wake mdogo huyo mgombea alisikika mara kadhaa hadharani akilalamika kwa Mkurugenzi kuwa kwa nini wanamzuia asisafirishe wapiga kura wake. Kwa upeo wake aliamini wapiga kura huko kwenye kata walikuwa mali yake. Alipoeleweshwa, alikataa na kumpigia K.MKUU na kumtumia
text kulalamika na K.MKUU naye akaforward message tena kwa Mkurugenzi wa wilaya kutaka maelezo ya huyo bepari. Ushauri wangu ni kwa vyombo ya usalama na maadili kufyeka wote waliopatikana kwa harufu ya rushwa.

Ninaamini ni wachache tu na siyo majimbo yote. Tusipodhibiti tamaa ya rushwa na madaraka, mwaka huu tutapata wagombea wa hovyo kabisa. Ikiwezekana hata mishahara ya wabunge ipunguzwe ili ku-discourage rushwa kubwa sana kwenye kura za maoni. Wachaguliwe wagombea safi waliotosheka na wasio na tamaa na wakubali mishahara na posho zao kupunguzwa ili zikatumike kujenga hospitali, mashule na miundombinu ya maji.

MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Njombe mjini agent wa mgombea alikuwa chooni.ukienda kukojoa unapewa msimbazi.kweli m/kiti wa ccm taifa anaichukia rushwa.shida anapambana na rushwa akiwatumia wala eushwa wakubwa.aliyeongoza viti maalum njombe.inasemekana alitumia zaidi ya 90milioni.njombe mjini ndo usiseme.rushwa ilitamalaki kama wingu la mvua.kifupi siasa na rushwa huwezi kuvitenganisha
 
Kwenye hizo chaguzi karibia wote wanatoa na kupokea Rushwa ila siyo wote wanagundulika
 
Malalamiko yanayoendelea humu ndani ya JF juu ya rushwa kwenye kura za maoni za CCM kwenye ubunge na udiwani kila jimbo, nashauri wote waliopata kuanzia namba 1 hadi 4 wakatwe! Next time hawatarudia, Na mkuu usiwape vyeo vungine maana hata kuho watataka kurudisha pesa yao - wapate hasara 100%
 
Malalamiko yanayoendelea humu ndani ya JF juu ya rushwa kwenye kura za maoni za CCM kwenye ubunge na udiwani kila jimbo, nashauri wote waliopata kuanzia namba 1 hadi 4 wakatwe! Next time hawatarudia, Na mkuu usiwape vyeo vungine maana hata kuho watataka kurudisha pesa yao - wapate hasara 100%
WEWE BONGE LA JINIAS ! HII IANZISHIE UZI KISHA U MTAG SLOW SLOW NA JIWE
 
Hata ile ya maigizo ya kumpitisha magufuli wajumbe walitishwa kuna namna waligawa kura ili ijulikane wabishi watatokea Kanda ipi......
Hii ccm ni chama cha kishetani wala rushwa wa nchi hii....
 
Rushwa ipo siku nyingi tu na haitaisha labda mbinguni.

Ili kuipunguza shida hii inabidi mshahara na marupurupu ya wabunge yawe laki tano tu. Na pasiwe na kiinua mgongo kabisa.


Watu wanamwaga pesa ya rushwa kwakuwa wanajua pesa itarudi kwa faida. Ila kama mshahara ukiwa mdogo hakuna atakaye mwaga hela. Hizo pesa zinazomwagwa zingetumika katika uwekezaji watu wengi sana tungepata ajira toka kwa hao mabosi wanaomwaga hela.
 
Back
Top Bottom