Utafiti unaonyesha kuwa wanawake hubakwa na waume zao

Michael Amon

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2008
Posts
8,768
Reaction score
3,622
Tafiti zilizofanywa na wataalama wa masuala ya afya na jamii zinadai kuwa baadhi ya wanawake waliomo katika ndoa hukumbana na kadhia ya kubakwa na wanaume zao na pia hudhalilishwa. Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali ambalo hujishughulisha na Afya na Maendeleo ya Mtoto-(KIWOHEDE), Justa Mwaituka amesema kuwa wanawake wengi walio kwenye ndoa wananyanyaswa na waume zao kwa kuwa wanalazimishwa kufanya mapenzi kinyume na maumbile pamoja na kufanya kwa njia ya mdomo.

"Iringa tumekutana na wanawake ambao wamezikimbia ndoa zao kutokana na kuingiliwa kinyume na waume zao pamoja na kulazimishwa kufanya ngono kwa njia ya MDOMO" anasema Mwaituka.
 
hiyo ndiyo dunia na mambo yake.......... lol
 
Inauma SANA lakini ndio ukweli huo. wanaume wengi hawajui kua kumlazimisha mkeo kushiriki tendo la ndoa wakati hataki ni kumbaka. Kwa njia yoyote ile, hata zile zinazoonekana kua za kawaida.
 
Inauma SANA lakini ndio ukweli huo. wanaume wengi hawajui kua kumlazimisha mkeo kushiriki tendo la ndoa wakati hataki ni kumbaka. Kwa njia yoyote ile, hata zile zinazoonekana kua za kawaida.

Kuna mmoja alikua anamshauri mwenzake afanye hivyo hapa hapa.
 
Afanyeje Lizzy? amlazimishe mke wake?

Yeahhh.
Jamaa alikua analalamika mke wake anasumbua sana hataki kuexplore mambo,hataki mune aridhike (eti wafanye kwa kiasi. . .LOL. . . kiasi chenyewe mara moja) mwenzake akamshauri amshike kwa nguvu eti atazoea na.kujifunza taratibu.
 
ndo itamchosha mara 600.
Bora atumie nyama ya ulimi(maneno)

Yeahhh.
Jamaa alikua analalamika mke wake anasumbua sana hataki kuexplore mambo,hataki mune aridhike (eti wafanye kwa kiasi. . .LOL. . . kiasi chenyewe mara moja) mwenzake akamshauri amshike kwa nguvu eti atazoea na.kujifunza taratibu.
 
ndio faida ya 'kuwowa' wanasheria hiyo, kila kitu kinachambuliwa from a legal perspective - kama unaamini mumeo anakubaka, peleka mahakamani apigwe miaka 30
 
ndio faida ya 'kuwowa' wanasheria hiyo, kila kitu kinachambuliwa from a legal perspective - kama unaamini mumeo anakubaka, peleka mahakamani apigwe miaka 30

Habari ndio hiyoo!!! Akinilazimisha kortini...akininyima kortini pia....
 

Huo ni ukweli usiopingika, lakini tatizo nadhani linatokana na uelewa mdogo wa wahusika wengi katika masuala ya mahusiano unajua kuna haja ya wanaume pia kukalishwa chini na kufundishwa kama wanavyofundishwa wanawake kabla ya kufunga ndoa ila walau akapewa baadhi ya taratibu muhimu za ndani ya ndoa, hii nadharia kwamba wanaume wanajua kila kitu si kweli. DOs and DONTs ni muhimu kwa pande zote na hasa huko vijijini ndio balaa kabisa.
 
Yeahhh.
Jamaa alikua analalamika mke wake anasumbua sana hataki kuexplore mambo,hataki mune aridhike (eti wafanye kwa kiasi. . .LOL. . . kiasi chenyewe mara moja) mwenzake akamshauri amshike kwa nguvu eti atazoea na.kujifunza taratibu.
That's bullsh*t! Watu kama hao ndio wanaaribu jamii. :ballchain:
 
ndio faida ya 'kuwowa' wanasheria hiyo, kila kitu kinachambuliwa from a legal perspective - kama unaamini mumeo anakubaka, peleka mahakamani apigwe miaka 30

umenena mkubwa
 
Inauma SANA lakini ndio ukweli huo. wanaume wengi hawajui kua kumlazimisha mkeo kushiriki tendo la ndoa wakati hataki ni kumbaka. Kwa njia yoyote ile, hata zile zinazoonekana kua za kawaida.

Kwa dunia hii ya sasa nadhani wengi wetu tunafahamu ila wanaamua kutumia mabavu ili kukidhi tamaa na haja ya miili yao. Wanaume jamani tubadilike.
 
Kuna mmoja alikua anamshauri mwenzake afanye hivyo hapa hapa.

nani huyo alikuwa anamshawishi? Embu niwekee link nije kumpasha ili ajifunze na ajue nini mwanamke anachotaka.
 
Yeahhh.
Jamaa alikua analalamika mke wake anasumbua sana hataki kuexplore mambo,hataki mune aridhike (eti wafanye kwa kiasi. . .LOL. . . kiasi chenyewe mara moja) mwenzake akamshauri amshike kwa nguvu eti atazoea na.kujifunza taratibu.

lakini akili ni nywele kila mtu ana zake. Ila kwa upande wangu mimi siwezi kufikiria kitu kama hicho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…