Elections 2010 Utafiti wa Synovate wabadilishwa kuisaidia CCM?

hivi ndo vitu huwa vinanikera sana.... hujakamilisha udaku unaleta hapa!!! we dont need false expectations... enough with blah
 
It is no longer tetesi, but reality. The deal to witheld the results was reached between the affected party and the leaders of the synovate

Vesry sad, but optimistic for Slaa
 
Mwananchi laongoza kwa kutopendelea-Utafiti

Wednesday, 15 September 2010
Nora Damian


WAKATI kampeni za uchaguzi mkuu zikigonga vichwa vya habari vya vyombo mbalimbali vya habari nchini, gazeti la Mwananchi linaongoza kwa kuandika asilimia 97 ya habari za uchaguzi bila ya upendeleo, kwa mujibu wa utafiti wa Synovate.

Meneja wa huduma kwa wateja wa taasisi hiyo ya utafiti ya Synovate, Jane Meela alisema mchakato huo ulioanza kati ya Agosti mosi na 31 mwaka huu, uliangalia habari za uchaguzi zilizokuwa zikiandikwa kwenye vyombo vya habari tangu kuzinduliwa kwa kampeni hizo.


CCM ndiyo ilikuwa ya kwanza kuzindua kampeni zake Agosti 21, na kufuatiwa na CUF Agosti 27 na Chadema Agosti 28.

Utafiti huo wa Synovate, kwa mujibu wa Meela, unaonyesha kuwa Mwananchi limekuwa likiandika habari za uchaguzi bila ya kuipendelea Chadema kwa kiwango cha asilimia 97 na CCM asilimia asilimia 95.
Meneja huyo alifafanua kwamba, taasisi yake ilifanya utafiti wa kufuatilia vyombo vya habari jinsi vinavyoripoti uchaguzi mkuu na kuongeza kwamba, katika utafiti huo kulikuwa na timu maalumu.

"Tulibaini kuwa viko vyombo vya habari ambavyo vinalalia upande mmoja katika kuchapisha ama kutangaza habari za uchaguzi mkuu na tunadhani ipo haja ya kuliangalia suala hilo kwa kina zaidi," alitahadharisha Meela.


Kwa mujibu wa Meela, utafiti huo ulihusisha magazeti ya kila siku, ya wiki, redio na televisheni mbalimbali.


Utafiti huo ulihusisha magazeti 36, vituo 28 vya redio na vituo 10 vya televisheni na kuangalia habari katika makundi ya habari zilizoandikwa ama kutangazwa kwa upendeleo, bila upendeleo na zile ambazo hazikuegemea upande wowote.


Mbinu waliyotumia katika utafiti huo kwa magazeti ya kila siku na yale ya wiki ni kwa kuyasoma na redio na televisheni ilikuwa ni kusikiliza na kutazama, kufuatilia habari zote zinazohusiana na uchaguzi, kuandaa muhtasari wa muktadha wa kihabari na kuchambua habari kwa ubora na kwa idadi yake.


Katika matokeo hayo, meneja huyo alifafanua kwamba Mwananchi iliongoza kwa kuandika habari za uchaguzi ambazo ni sawa kwa sentimita 41,060, likifuatiwa na Tanzania Daima sentimita 40,393, Nipashe 38,951, Uhuru 33,413, Majira 28,267, Habari Leo 28,455, The Guardian 22,171, Daily News 19,654, The Citizen 19,460 na Rai sentimita 15,256.


Meela alisema magazeti mengine yaliandika habari hizo kwa sentimita 149, 407 wakati kwa upande wa televisheni, TBC 1 iliongoza kwa kutoa sekunde 79,035 ikifuatiwa na ITV 40,553, Star TV 37,096, Mlimani TV 34,190, Channel Ten 30,902, Tanga TV 8,880, Abood TV 4,320 na TVZ 4,260.

Meela alifafanua kuwa Radio One ilirusha kwa sekunde 42,990, ikifuatiwa na TBC Taifa 39,225, Times FM 15,855, Redio Free Africa 14,190, Magic FM 7,698 na redio nyingine zilitangaza habari hizo kwa sekunde 44,280.

Kwa upande wa mambo yaliyopewa kipaumbele baada ya uzinduzi wa kampeni mnamo Agosti , Meela aliyataja kuwa ni pamoja na amani asilimia 28, rushwa 21, uchumi 15, kilimo 7, afya 6, haki za binadamu 3, ajira na utalii 1 na mengineyo 6.


Hata hivyo, alisema katika utafiti huo hawakuangalia vyama ambavyo vilikuwa havijaanza kampeni na kwamba walichokuwa wanaangalia ni habari zinazohusiana na uchaguzi mkuu.

NCCR Mageuzi ni moja ya vyama ambavyo hadi mapema mwezi huu kilikuwa bado hakijaanza kampeni kutokana na kuamua kuanza harakati zake baada ya kumalizika kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Kwa upande wa chama kilichoongoza kupewa nafasi kubwa, Meela aliitaja CCM kuwa iliandikwa kwa wingi na kufuatiwa na Chadema.

Kwa mujibu wa matokeo hayo ya utafiti, chama hicho tawala kiliongoza kwa kupata asilimia 51, ikifuatiwa na Chadema 21, CUF 14, NCCR- Mageuzi 6, TLP 4, SAU 2 na DP 2.
Kwa upande wa televisheni, CCM bado iliongoza kwa asilimia 59, Chadema 19, Cuf 16, Nccr-Mageuzi 3, SAU 2 na TLP 2.

Kwa upande wa redio CCM, iliongoza kwa asilimia 55, Chadema 20, CUF 14, Nccr 5, SAU 4 na TLP 2.


Alifafanua kwamba, Chadema ilianza kuandikwa na kutangazwa kwa wingi baada ya kumtangaza Dk Willibrod Slaa kuwa mgombea wake wa urais. Slaa alikuwa mbunge wa Karatu na kwa sasa ni katibu mkuu wa Chadema.


"Katika utafiti wetu tumebaini kuwa televisheni nyingi zimekuwa haziegemei upande wowote katika kutangaza habari zinazohusiana na uchaguzi mkuu," alisema Meela.


Synovate ni taasisi ambayo imekuwa ikiheshimika nchini kutokana na tafiti zake mbalimbali katika mambo ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.
 
Greater thinker!!!!
nime-do ze needful kwenye post hii!!!.....Well said!~
 
ukwli ni kwamba hawa jamaa wanatumiwa na ccm lakini ccm na iwapo ccm itashinda wanataka kuhalalisha kwa atanzania kwamba hata utafiti ulionyesha hivyo, kumbe wanajiwekea mazingira ya wizi wa kura tu.
 
Aise kweli lakini ni media ndio inasikitisha aise. Nasikia clouds waliongea zaidi kuhusu chadema. :welcome:
 
Saaizi hawana jipya tena wanakwambia.............kikwete anaongoza kwa kuandikwa zaidi..........wapuuzi hawa.....yaani regardless anatamkwa kwa mambo gani wao wanasema tu anaongoza kwa kuandikwa zaidi..............kweli akili ni nywele
 
Tuwapuuzeni hawa...........wanasema
 
All in all guyz, kila mwenye kufikiri rationally ni dhahiri CCM imetaitiwa, maana miaka yote tayari ngonjera za synovate na Redet zingekuwa zimeshasikika na kibwagizo kudakiwa na Makamba. I just can't believe the same pple waliokuwa wanatuambia namna gani Jk anakubalika some few months ago, sasa hivi wananyuti! Kweli mwenye macho haambiwi tazama....
 

Kama kweli hawa watafiti wa SYNOVATE hii ilikuwa ni taarifa ya kwamba CHADEMA inaoongoza kuliko CCM halafu wao wakapewa maelekezo kuficha ukweli. Kama mtu ana taarifa ya awali angetupa ili tuisambaze katika vyombo vya habari vya nchii vyenye mapenzi mema na nchii hii ambao watatoa taarifa yao wakiwaumbua kwa kuficha ukweli; mtafiti anapaswa kuwa mkweli ili aweze kuaminika.

Wasijaribu kuisukuma nchi yetu kwenye uwanja wa maangamizi kwa sababu ya taarifa yao wapuuzi sana waliojaa tamaa mbaya
 
Kwa kweli tuwe tunaongea kwa uhakika humu ndani, ninavyofahamu synovate ilikuwa ikidhaniwa kukibeba chama tawala hii ni SAWA.

Synovate imepata kazi kutoka shirika la kimataifa kufuatilia vyombo vya habari vinavyoripoti uchaguzi hii pia sawa

Waandishi wa habari wakaanza kulalamika kwa nini synovate wanachelewa kutoa matokeo hayo ya election media monitoring

Hatimaye juzi likawekwa tangazo pale habari maelezo kwamba watatoa report hiyo ya jinsi media inavyoripoti habari za uchaguzi kama ni fairly or not, na jana wakatoa habari hiyo na kusema wazi kuwa vyombo vingi vya habari vimeipendelea CCM hasa vyombo vya umma kwa kuipa muda mwingi tofauti na vyama vingine na wakaweka wazi kuwa hiyo ni kinyume na maadili ya uandishi pale habari maelezo.

Nashindwa kuelewa kama kweli wanapendelea CCM Wangetoaje ripoti kama hiyo inayoonyesha wazi CCM WAMEPENDELEWA.

Ndugu zangu wapenda maendeleo tuache kuipigia kelelele Synovate tunapoteza muda wa kampeni, na tuvipigie kelele vyombo vya habari vya umaa vinavyopendelea chama kimoja viache mara moja kwani viko hapo kwa ajili ya kodi zetu, Synovate wamefanya kazi yao ipasavyo this time, tungoje matokeo yao ya utafiti wa kura ya maoni
 

Nami pia nina wazo kama lako. Ni vema sana kwa Chadema ku-capitalize kwenye hii 44% ili wananchi hasa wa vijjini uoga uwapungue kuhusu upinzani.
 
Kumbuka mambo yanaenda yakibadilika kila siku, miezi sita iliyopita CHADEMA kabla Dokta Slaa hajatambulishwa mgombea urais haikuwa CHADEMA ya leo, kila siku kuna mabadiliko makubwa watu wanazidi kujua mengi na wanabadilika pia kutokana na awareness.

Sipingi wala kukubali tafiti hizo bali nataka nikuambie kila siku kuna mabadiliko na usishangae matokeo yakiwa completely different today.
 
Haya ni matokeo:

1. Zaidi ya asilimia 50 ya habari kwenye media ni kuhusu CCM

2. Chadema inapata coverage ya kama 20%

3. Vyama vilivyobaki, CUF, NCCR, TLP, etc vinagawana asilimia iliyobaki.

Magazeti yanayoandika habari za CCM kwa asilimia 50, mengi hayanunuliwi kabisa, na hizo taarifa hakuna anayezipata, magazeti haya kesho yake yanakuwa vifungashio vya maandazi mitaani.

Asilimia 20 ya habari za CHADEMA zinaandikwa kwenye magazeti makini kama Mwananchi, Tanzania Daima, Raia Mwema, na Mwanahalisi, nakala zinazochapishwa ni mara mbili au tatu ya magazeti ya serikali na mengineyo, na yote hununuliwa kwa kugombewa.
 

ukweli mtupu
 
Huyu jamaa kasema kweli. Utafiti ni tofauti na monitoring. WAKE UP!!! Alafu hawa majamaa wamesema kwamba ni bora waandishi wawe wanaandika bila upendeleo. Mi sijui watu wanaelewa vipi hio statement.:confused2:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…