Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
KUMBUKIZI YA NYUMBA YA MWALIMU NYERERE NA PICHA ZA MWANZO WA NYAKATI ZAKE
Tukichagua picha za Mwalimu Nyerere
Watafiti wa Kumbukizi ya Nyumba ya Mwalimu Nyerere leo L' Asr walinitembelea tena kwa nia ya kupata picha adimu za Mwalimu Nyerere kwa ajili ya kuzionyesha katika nyumba aliyoishi Magomeni ambayo sasa ni sehemu ya kumbukumbu yake.
Tumekaa sote na tumesaidiana kuchagua picha moja baada ya jingine zaidi tukiongozwa na ''caption,'' za picha hizi.
Nyingi ya picha hizi nimeshazionyesha katika mitandao ya jamii lakini kwa maofisa hawa baadhi ni picha ngeni kwao.
Madhumuni yao ni kuweza kukusanya kila picha ya Mwalimu Nyerere na za washirika wake ili kukamilisha historia yake mwenyewe Baba wa Taifa katika picha ili kuonyesha uasilia wa hali ilivyokuwa katika miaka ya 1950 nyakati Baba wa Taifa alipofika Dar es Salaam na kupokewa na wenyeji wa mji na kuanza harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.
Picha ni nyingi na sina hakika kama tumeweza kuzipata zote lakini nimefarajika wataalamu hawa waliponiambia kuwa hii ni kazi endelevu na tutakuwa tunaifanya siku zote na wakati wote.
Naweka baadhi ya picha ambazo mimi hii leo nimewakung'utia watafiti hawa ili zikapambe nyumba ya Mwalimu zikiwa kama kumbukumbu yake na wale aliokuwanao katika kuikomboa Tanganyika kutoka makucha na minyororo ya ukoloni.
Baadhi ya picha ambazo zimepatikana kwa ajili ya kumbukizi ya Baba wa Taifa ni hizo hapo chini na hizi hapo chini na kila picha inaeleza maisha ya Mwalimu Nyerere na chama cha TANU.
Baadhi ya historia za wazalendo hawa katika kupigania uhuru wa Tanganyika zinaweza kusomwa hapo chini katika hizo link:
1. Sheikh Hassan bin Ameir 2. Salum Mpunga (Lindi) 3. Yusuf Chembera (Lindi) 4.Yusuf Olotu (Moshi) 5 Iddi Tosiri 6. Sharifa bint Mzee (Lindi) 7.Mwalimu Kihere (Tanga) 8. Abdul Sykes, Nyerere, Dossa Aziz na Lawi Sijaona 9.Abdallah Rashid Sembe (Tanga) 10. Makatta Mwinyi Mtwana na Sadiq Patwa (Tanga) 11. Bi. Titi Mohamed na wazee wa Dar es Salaam 12. Shariff Abdallah Attas 13. Bi. Mruguru bint Mussa (Mama Abdul) 14. Sheikh Hussein na Hassan Juma 15. Robert Makange 16. Paul Bomani (Mwanza) 16. Ali Migeyo (Bukoba) 17. Maulidi Kivuruga (Tabora) 18. Chief Kidaha Makwaia (Shinyanga) 19. Mwami Theresa Ntare (Kasulu) 20. Amir Jamal na Nyerere 21. Haidar Mwinyimvua...
Tukichagua picha za Mwalimu Nyerere
Watafiti wa Kumbukizi ya Nyumba ya Mwalimu Nyerere leo L' Asr walinitembelea tena kwa nia ya kupata picha adimu za Mwalimu Nyerere kwa ajili ya kuzionyesha katika nyumba aliyoishi Magomeni ambayo sasa ni sehemu ya kumbukumbu yake.
Tumekaa sote na tumesaidiana kuchagua picha moja baada ya jingine zaidi tukiongozwa na ''caption,'' za picha hizi.
Nyingi ya picha hizi nimeshazionyesha katika mitandao ya jamii lakini kwa maofisa hawa baadhi ni picha ngeni kwao.
Madhumuni yao ni kuweza kukusanya kila picha ya Mwalimu Nyerere na za washirika wake ili kukamilisha historia yake mwenyewe Baba wa Taifa katika picha ili kuonyesha uasilia wa hali ilivyokuwa katika miaka ya 1950 nyakati Baba wa Taifa alipofika Dar es Salaam na kupokewa na wenyeji wa mji na kuanza harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.
Picha ni nyingi na sina hakika kama tumeweza kuzipata zote lakini nimefarajika wataalamu hawa waliponiambia kuwa hii ni kazi endelevu na tutakuwa tunaifanya siku zote na wakati wote.
Naweka baadhi ya picha ambazo mimi hii leo nimewakung'utia watafiti hawa ili zikapambe nyumba ya Mwalimu zikiwa kama kumbukumbu yake na wale aliokuwanao katika kuikomboa Tanganyika kutoka makucha na minyororo ya ukoloni.
Baadhi ya picha ambazo zimepatikana kwa ajili ya kumbukizi ya Baba wa Taifa ni hizo hapo chini na hizi hapo chini na kila picha inaeleza maisha ya Mwalimu Nyerere na chama cha TANU.
Baadhi ya historia za wazalendo hawa katika kupigania uhuru wa Tanganyika zinaweza kusomwa hapo chini katika hizo link:
-
BI SHARIFFA BINT MZEE MUASISI WA TANU LINDI 1955
Bi. Shariffa bint Mzee Katika Ujana Wake Wakati wa Kupigania Uhuru wa Tanganyika ''Realising the importance of having educated leader...mohamedsaidsalum.blogspot.com
-
HAIDAR MWINYIMVUA (1905 - 1987) ALIUZA NYUMBA KUIKOMBOA TANGANYIKA NA ALHAJ ABDALLAH TAMBAZA
SHAJARA YA MWANA MZIZIMA: MZEE HAIDAR MWINYIMVUA (1905 - 1987) ALIUZA NYUMBA KUIKOMBOA TANGANYIKA Alhaji Abdallah Tambaza Hidar...mohamedsaidsalum.blogspot.com
-
MUFTI SHEIKH HASSAN BIN AMEIR (1880 - 1979)
Seminar on The Role of Educated Youth to Muslim Society 27 th February – 4 th March 2004 ORGANISED BY ZANZIBAR UNIVERS...mohamedsaidsalum.blogspot.com
-
YUSUF OLOTU 1927 - 1997: SHUJAA WA KURA TATU, 1958
YUSUF OLOTU 1927 - 1997 SHUJAA WA KURA TATU Utangulizi Nilikwenda kumuona Mzee Yusuf Olotu nyumbani kwake Moshi nyakati za jion...mohamedsaidsalum.blogspot.com
-
Sheikh Abdallah Rashid Sembe (1912-1999) Shujaa wa Azimio la Tabora la mwaka 1958
Sheikh Abdallah Rashid Sembe KIFO cha Abdallah Rashid Sembe kilitokea Hospitali ya Bombo, Tanga tarehe 22 Mei, 1999. Siku ya pili yak...mohamedsaidsalum.blogspot.com
-
BWANA MKUBWA BWANA WA MABWANA: MAKATTA MWINYI MTWANA
Utangulizi Makatta Mwinyi Mtwana Sifa za utajiri wa Makatta Mwinyi Mtwana bado zinahdithiwa Tanga hata baada ya zaidi ya nusu kar...mohamedsaidsalum.blogspot.com
-
Ali Migeyo: Ushapata Kumsikia Shujaa Huyu Aliyepigania Uhuru wa Tanganyika?
Ali Migeyo Shujaa Kutoka Bukoba Ali Migeyo Ali Migeyo alipigwa mabomu ya machozi na Waingereza Kamachumu mwaka 1953 wakati akida...mohamedsaidsalum.blogspot.com
-
KUTOKA JF: MAMA DAISY NA HISTORIA YA CHIEF DAVID KIDAHA MAKWAIA
Pasco said: ↑ Huyu mama ndiye aliyempokea Dar es Salaam Mama Maria. .. Pasco, Huyo Bi. Mkubwa ni Mama Daisy . Huyu mi...mohamedsaidsalum.blogspot.com
-
MCHANGO WA BAADHI YA MACHIFU KATIKA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA SEHEMU YA KWANZA
Mchango wa Baadhi ya Machifu Wazalendo katika Harakati za Kudai Uhuru wa Tanganyika Mwami Theresa Ntare (1922 - 1999) ''Chach...mohamedsaidsalum.blogspot.com
-
SALUM MPUNGA NA YUSUF CHEMBERA MARAFIKI WAASISI WA TANU LINDI
Salum Mpunga Yusuf Chembera Akiwa Mayor wa Lindi Town Council SHUKRANI Ninatoa shukrani kwa waasisi wa walioleta mabad...mohamedsaidsalum.blogspot.com
- https://mohamedsaidsalum.blogspot.com/2013/12/bibi-titi-mohamed-1926-2000-shujaa-wa.html