Utajifunga: Polisi huenda wakaanza kusikiza mawasiliano yako ya simu

Utajifunga: Polisi huenda wakaanza kusikiza mawasiliano yako ya simu

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Polisi wataweza kuingia nyumbani ama afisini mwako kuweka vifaa vya kunasa mawasiliano yako
Mahakama itakubali ushahidi unaopatikana kwa njia hiyo

Polisi huenda wakapata idhini ya kusikiliza mawasiliano yako kwenye simu ya mkononi iwapo watakushuku kwa kujihusiaha na biashara ya dawa za kulevya endapo sheria inayopendekezwa itapitishwa .

Mswada huo unaopendekezwa na mbunge wa Kiambaa Paul Koinange utawaruhusu polisi kuingia nyumbani ama afisini mwako na kuweka vifaa vya kuweza kusikiliza mawasiliano yako ya simu .

Na kwa minajili ya kutafuta ushahidi korti inaweza kumruhusu afisa wa polisi mwenye chao juu ya Chief inspekta kuifanya oparesheni kama hiyo .

Polisi hata hivyo watajitajika kupata idhini ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma kabla ya kwenda kortini .

“ Korti itatoa agizo linalohitaji kampuni ya mawasiliano kunasa mawasiliano ynayaofanywa au yanayokaribia kutekelezwa’ sehemu ya mswada huo inasema

Koinange ndiye mwenyekiti wa kamati ya bunge kuhusu usalama . Korti pia itawaruhusu polisi kuchukua simu yako ya mkononi na vifaa vingine vinavyotumiwa kufanikisha biashara ya dawa za kulevya .

Mahakama hata hivyo zitaridhishwa kwanza kwamba mawasiliano yanayonaswa yanaweza kusababisha kutekelezwa kwa uhalifu chini ya sheria hiyo ya kupambana na mihadarati .

RadioJambo
 
Hivi ina maana polisi hawafanyi kwa sasa au, maana siku zote huwa nipo makini kila nikiongea kwa simu, hazina siri, huko kwenu Tanzania ile kesi ya Membe na wenzake kudukuliwa maongezi yao ya kwenye simu iliishaje.
 
Hivi ina maana polisi hawafanyi kwa sasa au, maana siku zote huwa nipo makini kila nikiongea kwa simu, hazina siri, huko kwenu Tanzania ile kesi ya Membe na wenzake kudukuliwa maongezi yao ya kwenye simu iliishaje.

ukiongea utumbo utasokotwa tu noway.

kwani nyinyi idara zenu za usalama zimelala bar??
 
Hivi ina maana polisi hawafanyi kwa sasa au, maana siku zote huwa nipo makini kila nikiongea kwa simu, hazina siri, huko kwenu Tanzania ile kesi ya Membe na wenzake kudukuliwa maongezi yao ya kwenye simu iliishaje.
Nilidhani kenya kuna uhuru na privacy inaheshimiwa...au ni kwa mdomo tuu ila kwa ground ni kama NKPR?🤣🤣
 
Tanzania ukichapisha jambo which goes against our mzee.. utajua hujui
 
Hivi ina maana polisi hawafanyi kwa sasa au, maana siku zote huwa nipo makini kila nikiongea kwa simu, hazina siri, huko kwenu Tanzania ile kesi ya Membe na wenzake kudukuliwa maongezi yao ya kwenye simu iliishaje.
Kila kitu TZ ukilala na njaa unajifariji hivyo hivyo hata TANZANIA watu wanalala na njaa [emoji205] we
 
"...Polisi wataweza kuingia nyumbani ama
afisini mwako kuweka vifaa vya
kunasa mawasiliano yako
Mahakama itakubali ushahidi
unaopatikana kwa njia hiyo..." Tatizo lipo wapi, 'Wire taps' ni jambo la kawaida duniani kote, mswada wa mbunge Paul Koinange unazungumzia 'targeted wire taps' kupitia mahakama, sio kusikizwa kwa mawasiliano yote kila wakati. Ushahidi mahakamani kupitia mawasiliano ya simu umekuwa ukitumika na mafanikio makubwa kufungua kesi na kuhukumu wahalifu kwenye nchi kama US, UK, France Germany n.k.
 
Back
Top Bottom