Utajiri wa Magofu ya Rapta

Hivyo basi kumuona fatemeh katika muonekano ule wa kujistili haikua bahati mbaya, hiyo Ndio ilikua tamaduni ya wasichana au wamama wa nchi hiyo ya Iran.

Na nilijithibitishia hilo baada ya kuingia ndani ya mji huo japo ilikua ni safari ya siku nzima kuanzia usiku ule mnene tulipotoka kwenye hotel ile.

Tukiwa ndani ya ndege ile wengi wa abiria walionekana kufahamiana au kujuana na Fatemeh. At least tulivyoingia kwenye ndege ubize wa fatemeh ulipungua kidogo sio kama ilivyokuwa hapo awali.

Kwa jinsi fatemeh alivyokua amekaa kwenye siti yake isingekua rahisi kwa mtu yoyote kuamini kwamba mwanadada huyo alikua ni mjuzi wa mambo mengi hususani upande wa mapigano lakini pia upande wa udukuaji wa taarifa za kiusalama.

Kwa taarifa fupi tu ni kwamba mwanadada huyo alikua ni mwiba pia kwa shirika la kijasusi la Israel maarufu kama Mossad.

Kwani mara kadhaa alihusika kwenye kufuatilia na kudukua taarifa muhimu zilizohusu majasusi wa Mossad na shughuli zao Ndani ya nchi hiyo ya Iran.

Umahili wa fatemeh uliwahi pia kuonekana katika moja ya misheni kubwa za kijasusi zilizowahi kufanywa na Mossad ndani ya nchi ya Iran.

Misheni hiyo ilikua ni ile iliyohusu vijana au watu wasiojulikana kwenda kuvunja ghala lililopo pembeni mwa mji wa Tehran (eneo la viwandani).

Baada ya watu hao kuvunja na kuondoka na nyaraka zilizohusu mikataba ya utengenezaji wa siraha za nyuklia, mikataba hiyo hapo baadae ilikutwa ndani ya jiji la Tel Aviv.

Wakati wa tukio hili kuna makamanda wengi wa Iran walituhumiwa kutumika na shirika la mossad kwenye misheni hiyo ambayo ilipingwa vikali na nchi ya Iran.

Asilimia kubwa ya watuhumiwa ambao waliitwa ni wasaliti kutokana na wao kutumika na shirika la upande wa pili yaani Mossad walihifadhiwa ndani ya jela iliyojulikana kama Evin Ndani ya mji huo.


Hapa nilikua najaribu kuelezea baadhi ya matukio yaliyomfanya fatemeh kuonekana bora zaidi kwenye tasnia hiyo, kwani tukio la vijana hao kuvunja ghala lilitokea miaka ya hivi karibuni yaan mwanzoni kabisa mwa mwaka wa 2017.

Kwa kutokea kwa tukio hili nadhani tunaendelea kupata picha ya kile tunachoita vita ya kijasusi inayoendelea baina ya nchi hizi mbili yaani Iran na Israel.

Hivyo basi watu wa MOIS wanajitahidi sana kuhakikisha hakuna uhusika wa namna yoyote ile ya shirika la mossad kwenye misheni zao. Kwani mara kadhaa hawa Mossad wamekua wakiwatumia maafisa wa Ndani wa Iran ili kufanikisha misheni zao.

Safari hii ilikua ndefu na ilituchukua mpaka masaa kumi na sita (16) mpaka kufika kwenye airport iliyojulikana kama Imam Khomeini International Airport.

Airport hii ilikua bize sana Wakati tunafika hapo, ni wazi kwa upande wetu wakati tunafika hapo tulipata treatment ya tofauti. Niliona kabisa tumekua treated katika namna ya ki V.I.P ukilinganisha na ndege nyingine zilizofia eneo hilo.


Ulinzi uliimarishwa katika kila angle na maafisa ambao walijulikana kama au maarufu kama sepah jina lingine la maafisa wanaosimamia ulinzi eneo hili waliitwa (Islamic Revolutionary Guards Corps) yaani IRGC.

Muda wote nilikua pembeni ya fatemeh kwa kila hatua anayopiga sikutaka aniache hata hatua moja, nadhani pia kuna baadhi ya watu walishangazwa na kwa namna tulivyoongozana.

Njia zote tulizopita zilikua ni v.i.p kiasi kwamba hakukua na muingiliano mkubwa wa watu kuzunguka maeneo yote tuliyokua tunapita mimi na fatemeh.

Baada ya kutoka ndani ya uwanja tulizunguka nyuma ya uwanja huo ambapo tulikuta gari nyeusi aina ya Toyota hiace.

Gari hiyo ilionekana kuwepo pale ikitusubiri sisi, na tulipoikaribia tu fatemeh alifungua mlango kiasi kwamba alikua ameshajua kama gari hiyo ilikua pale kwa ajili yetu.

Ila tulipoingia ndani ya gari hiyo hakukua na mawasiliano yoyote na derava. Kwa lugha rahisi hatukuweza kuonana na dereva wa gari hiyo kutokana na namna ilivyoundwa kwa kutengenisha sehemu hizi za passenger na driver.

Safari haikua ya kitoto kwani na hapa tena tulitembea na gari hiyo kwa zaidi ya saa nzima kwa makadirio mpaka tulipofika sehemu iliyoitwa Pasdaran.

Hakika mji huu wa Tehran ulikua mgumu sana kwa kuungalia tu mtu anaweza gundua hilo.


Ulikua mji mgumu kwa wale vijana wa ovyo kwani nikikumbuka mji wa Lima jinsi wadada walivyojiachia ilikua tofauti kabisa na mji huu wa Tehran.

Mfano tu pale Lima kuna beach moja ni open beach inaitwa Ancon, aisee ukifika pale hatakama haukua na mawazo ya kutoka na mchumba yaani utabadiki tu mawazo yako.


Kuna watoto sijui niseme wana laana kwa mavazi yao ambayo hakuna namna utaweza kuepuka vishawishi vyao.

Binafsi nilivutiwa sana na maumbo yao mazuri pamoja na nywele ndefu za kuvutia. Wadada wa kiperu au Peruvian kama wanavyoitwa wengi wana asili kama ya ki-asia ukiwatizama kwa haraka.


Mji huu ukibahatika sana kumuona binti basi umeona sura au mikono tena ni kwa mabinti wachache sana Kwan wengi wao wamefunika sehemu kubwa ya miili yao.

Lakini ukiongelea miji mirahisi kwa hali ya maisha basi jiji la Tehran ni miongoni mwa majiji hayo ambayo ni simple au rahisi sana kwa mtu mmoja mmoja kumudu gharama za maisha.

Fatemeh hakuonekana tofauti kabisa na wadada wa mji huo, kwani mavazi alivyovaa yeye yalifanana kabisa na wanawake wengine wa mji huo kimuonekano.

Kiukweli fatemeh alikua miongoni mwa wadada wachache ambao hawakufunika sura zao zaidi ya kichwa na kuvaa magauni marefu yaliyofunika miguu yao.

Hapa sasa urembo wa fatemeh haukuonekana tena, hivyo binafsi nilikua miongoni mwa wanaume wachache wa mji huo tuliowahi kumuona fatemeh akiwa hana hizo hijab kama wanavyoita wenyewe.

Kuna muda nilimwangalia fatemeh nikaishia kutabasamu tu, na yeye alijua ni kitu gani kilinifanya nitabasamu baada ya kumuangalia.


FATEMEH: you still need a bitch to sleep with?
( Bado tu unahitaji binti wa kulala nae)

Nilijua kwanini aliuliza swali lile, kwa mazingira yale ya Tehran haikua kazi rahisi kununua ngono kama ilivyokua kwa peru na miji mingine ya America ya kusini.

Hivyo aliuliza vile kama tu namna ya kunistua kwamba sina ujanja tena kwani mji huo hakuna namna naweza kula tunda kimasihala zaidi ya kuoa.

Kiukweli kuna muda nilimuogopa sana fatemeh ila kuna muda kama nilimzoea na kutokuonyesha kama namuogopa.

Zile nyakati ambazo anakua serious sana ndizo nyakati ambazo alinitisha sana kiasi kwamba nilishindwa ata kumuongelesha hivyo tulikaa kimya mda mwingi.

MIMI: I don't need a girl anymore
( Sina haja ya msichana tena)

FATEMEH: That's what I wanted to hear from you
( Hicho ndicho nilitaka kusikia kutoka kwako)
Fatemeh alisisitiza kama ni kweli sihitaji tena msichana wakati huo basi tutaanza kuelewana na Mambo yataenda sawia kabisa.

Kuna muda aliniuliza kama nimeshamsahau merry, nilishangaa alimjuaje merry lakini nilipokumbuka kama wanamjua mpaka brother basi niliamini kumjua Merry ilikua simple kwani kama walifuatilia nilitokaje sengerema basi ni wazi walimjua pia na Merry.

Majibu yangu yalikua ni kama sijamsahau na sidhani kama nitaweza kumsahau kirahisi hivyo. Fatemeh alisema ni kweli na amethibitisha hilo kwakua mpaka wakati huo nilitunza hereni za mrembo huyo.

Licha ya kutunza nilizithamini pia kwani sikua tayari kuzipoteza kwa namna yoyote. Fatemeh alitibitisha hilo toka siku ile pale mgodini wakati nabadili nguo kwani alijua nimecha hereni hizo ila hakutaka kunikumbusha.

Na baada ya mimi kukumbuka hereni hizo ndipo alithibisha kuwa bado nina mkumbuka sana, japo alishangaa sana ni kwanini bado natamani ngono na wasichana wengine ilihali nimetoka kumpoteza merry siku si nyingi.

Hapa fatemeh aliongea kauli moja nzuri japo nilishindwa kuihusianisha au kujua ilihusiana vipi na maongezi yetu,



Alisema: wanaume wa kiafrika tunahitaji ngono ili tuonyeshe mapenzi kwa mwanamke, wakati huo wanawake wetu wanahitaji mapenzi ili watupatie ngono (miili yao).

Nilimjibu kuwa sijamuelewa kauli hiyo alimaanisha Nini, lakini aliniambia nitamuelewa siku nikikutana na mwanamke ambaye atakua na mapenzi Lakini hayupo tayari kingono.


Tuliingia Ndani ya jengo moja refu sana na moja kwa moja tulielekea kwenye lifti, tukiwa ndani ya lift fatemeh aliniomba nimtajie majina kamili ya yule jamaa aliyejulikana kwa jina la Shahzad.

Kiukweli nilichemka kabisa, nilimwambia kulingana na taarifa zilizo tokea kwa javier bwana huyo alimtaja kwa jina moja tu la shahzad.

Hapa fatemeh aliniangalia kisha akasema ndani ya mji huo jina shahzad ni la kawaida sana yaani kila mtaa ni kawaida kukutana na mtu anatumia jina hilo. Hivyo nilipaswa kuuliza vizuri kuhusu majina hayo.

Lakini mpaka wakati huo hatukua na namna ya kuuliza majina hayo kwani tulishakua mbali na bwana Javier ambae ndio alionekana kuwa na taarifa za Shahzad.


FATEMEH: Don't worry, I know what to do.
( Usijali nitajua cha kufanya)

Na mimi niliamini hivyo, kwani kama aliweza kunijua mimi na familia yangu yote basi isngekua kazi ngumu kumtambua bwana huyo alijulikana kama Shahzad.

0623329512 Whatsapp mzigo unashuka kila siku. Na tupo mbele zaidi

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
 
Shukrani kwa aliyekuwa anatafuta huu uzi, hatimaye amenifikisha hapa, nami naweka kambi rasmi
 
Wadau mtu mmoja anisaidie kutafuta episode namba15C
 
story isha andaliwa mkuu shida anataka wote twende whatsapp hapana kwa kweli
Jamaa anataka kutununua hili kusoma kama vile mikataba ya waarabu kwa bandari hii Hapana kwa kweli Bora tukomae humu
 
Ghorofa ile ilikua na zaidi ya floors 24, kwani mimi na fatemeh tulishuka au tuliishia flow hiyo ya 24 lakini bado kulikua na floor nyingine kwenda juu zaidi. Na Ndani ya floor hiyo ndipo kulipokua na apartment aliyokua akiishi fatemeh.

Tulipofika ndani ya apartment hiyo fatemeh aliniambia hapo ni kwake hivyo naweza kumpumzika kwa amani kabisa kwani nipo sehemu salama.

Mandhari ya apartment hiyo ilinivutia sana kiukweli kwani palikua pametulia mno hakukua na kelele wala movements za watu za hapa na pale.

Ukiwa ndani ya apartment hiyo unaweza kuuangalia mji wote na shughuli zote zilizokua zikiendelea mjini hapo. Fatemeh alinionyesha chumba ambacho nitalala siku zote nikiwa hapo kabla ya kurudi bongo na alisema ameagiza aletewa kila kitu cha msingi kiichotakiwa kuwepo ndani hivyo ikitokea yeye hayupo nitaweza kupata kila kitu ndani na sitakuwa na haja ya kutoka ndani umo.

MIMI: Why do you live on your own without siblings?
( Kwanini unaishi mwenyewe hauna ndugu?)

FATEMEH: you should be my brother, how do you think
( Tufanye uwe kaka yangu basi, unaonaje)

Kwa majibu yale niligundua hakua na ndugu kabisa ndio maana alikua pale akiishi peke yake.

MIMI: you can't be my sister
( Hahahahah huwezi kuwa dada yangu)


FATEMEH: why
( Kwanini)

MIMI: you already sucked my dick
( Unakuaje dada yangu wakati tayari umeshanyonya ****)

Jibu langu lilimfanya awe na ki aibu cha kike na kilimpelekea kupoteza utulivu kabisa.

FATEMEH: now.....!!!! who can we be if not brother and sister
( Sasa tunaweza kuwa nani kama sio kaka na dada)

MIMI: lovers
( Wapenzi)


Fatemeh hakujibu chochote zaidi aliniangalia tu na kusimama kuelekea kwenye chumba chake. Mpaka hapo niligundua fatemeh na ujanja wake hakuwahi kuwa na interaction na wanaume.

Wale wanaume alio interact nao ni wale waliohusisha mambo ya kazi pekee lakini mbali na hapo kuna uwezekano mkubwa hakua ata na rafiki wa kiume.

Hivyo apo nilitamani sana kujua story ya maisha yake huko nyuma, yaani alisoma vipi na alikulia wapi na kuzaliwa wapi.

Kutokujiamini kwake niligundua tulipokua ndani kwani hakua na utulivu kabisa ata kuniangalia usoni hakuweza kabisa. Jambo hilo ndio lililo nipelekea nazidi kujua weakness yake na mimi kumkazia sana usoni tunapokua kwenye maongezi hali iliyomfanya kukosa utulivu kabisa.
Baada ya kuona mwenzangu amenikimbia pale sitting room kutokana na maneno yangu ambayo yalimkosesha amani. Na mimi nilielekea kwenye room ambayo niliambiwa ndio nitaitumia siku zote nitakapo kuwa eneo hilo.

Cha kwanza kabisa ilikua ni kuoga, wakati nipo bafuni niliskia kama kengele ya mlangoni ina bisha hapo nilijua kuna mgeni amefika eneo hilo.

Wakati naendelea na kuoga na mlango wa chumba changu ulifunguliwa japo sikujua ni nani ameingia mi niliendelea na shughuli zangu chooni.

Nilipotoka kuoga nilikuta mfuko mkubwa wa plastic ukiwa kitandani, ndani ya mfuko ule kulikua na nguo mbali mbali zikiwemo na kanzu pia. Hapo niligundua aliyekua anapiga hodi ya kengele ndiye aliyekua amekuja na mzigo huo wa nguo.

Kwenye zile nguo zote zilizokuwepo eneo lile niliona ngoja nivae kanzu kwani kwenye maisha yangu sikuwahi kuvaa vazi hilo kabisa hivyo niliona wakati huo ni wakati sahihi kabisa kujaribu vazi hilo.

Baada ya kutupia kanzu yangu ambayo ilionekana ni ghali sana mjini pale, nilijisogeza mpaka sitting room ambapo nilimkuta fatemeh akibeba baadhi ya mizigo iliyoletwa hapo akiipeleka jikoni na stores.

FATEMEH: mashaallah!!!.... You look amazing today
( Mashaallah, umependeza sana)

Pia aliuliza kwanini nimechagua kuvaa kanzu wakati zilikuwepo nguo za kibrazamen mfano t-shirt na jinsi na kadet pia. Jibu langu liikua ni lilelile sikuwahi kuvaa kanzu hivyo basi nilitaka kujua ninaonekana vipi.


Nilianza kumsaidia fatemeh kubeba mizigo hiyo kupeleka store na jikoni, wakati tunaendelea na ubebaji niliuliza ni nani aliyekua akibisha hodi ya kengele.

Kwa majibu yake ni watu wa delivery na hao ndio watu pekee ambao hufika hapo kwani hakuna mtu mwingine yoyote ambaye anaweza kufika hapo ukizingatia hakuwahi kuwa na ndugu au kuwajua ndugu zake kabisa.

Hata hivyo fatemeh alionekana kufurahia uwepo wangu Ndani ya nyumba ile niligundua hilo baada ya kusikia kauli yake. Alisema kwa miaka kadhaa toka atoke kituo cha nursery imam Ali amekua akiishi peke yake ndani ya nyumba hiyo.

Lakini siku hiyo alikua ni mwenye faraja baada ya kuona tupo wawili tunabadilishana mawazo na kupiga stories mbalimbali japo kuna muda story zangu zinamkera.
Alidai nimeshindwa kumsoma yeye ni mtu wa aina gani kwani nimekuwa nikitanguliza tamaa ya ngono sana wakati yeye hakua na mawazo hayo.

Lakin pia alidai hakuwahi kuwa na mahusiano ya karibu na mwanaume wa aina yoyote mpaka kufikia umri huo. Hivyo basi kulingana na maisha aliyolelewa mpaka kufikia hapo mimi ndio mwanaume aliyewahi kuwa nae karibu mpaka kufikia hatua ya kushika maungo yangu.

Hivyo alitanguliza kusema sababu kubwa ya kunizoea mpaka kufikia hatua hiyo imesababishwa na namna tulivyoanza mazoea hayo tukiwa haullaga.

MIMI: ok....! that's why miss aparecida Said I'm very lucky man
( Ndio maana aparecida alisema nina bahati sana)


Since I very lucky man, i can get your virginity too

fatemeh alisema kwa tabia zangu hizi za kujifanya kidume mwenye uchu kumbe ni bora Javier angeniacha jamaa wanishughulikie.

Hapo niligundua anachukizwa na maneno yangu ya kufosi kula tunda kwani yeye hakuwa na mawazo hayo kabisa. Muda wote tukiwa ndani fatemeh alikua amefunika kichwa, sasa nilishangaa sana kwani hapo mwanzo tukiwa haullaga hakuwa vile kabisa.

MIMI: why you still covering yourself, you didn't do that when we were in haullaga.

( Mbona bado unajifunika wakati hukufanya hivyo tukiwa haullaga. Kama umeamua kujifunika jifunike tukiwa nje huku ndani niache nifurahie urembo wako)


Apa sasa fatemeh alijibu kwamba Kule haullaga alikua ni Manuela ila huku Tehran nipo na fatemeh binti wa ki-shia ambayo hapitwi na swala kabisa.

Hapa pia nilimuuliza kama yeye ni mtu wa swala ilikuaje akawa anatumia dawa za kulevya akiwa haullaga tena alikua teja kabisa.

Majibu ya fatemeh yalikua mepesi mno, alisema next time atanieleza ni nini kilikua kinafanyika pale ila ukweli ni kwamba kwenye maisha yake hakuna kilevi alichowahi kutumia mpaka anafikia umri huo.

Ni wazi fatemeh hakupenda kujibu maswali yaliyohusu taaluma yake ya ujasusi lakini pia taaluma yake ya udukuzi kwani maswali mengi aliyaacha na kusema ata nieleza kiundani hapo baadae kwani bado hakua ameniamini kiasi hicho licha ya kua na taarifa zangu za kutosha.
Muda huu tulishamaliza kuweka sawa mizigo yote kuanzia jikoni mpaka store hivyo tulikua wote tupo jikoni tukiendelea na mapishi. Mtoto wa kibongo sikua nyuma sana yaani yeye akishika nyanya mimi nashika kitunguu.

Yeye akishika mafuta mimi nashika mwiko au kijiko, yote hiyo niliifanya kuhakikisha naendelea kutengeneza ukaribu nae kwani Imani yangu ya kula tunda ilirudi upya kabisa.

Kwa asilimia fulani nilifanikiwa kwani tukiwa jikoni tulikua close sana yaani ukaribu uliongezeka lakini pia alikua huru ukilinganisha na masaa machache yaliyopita.

Lakini pia niligundua ata yeye kuna vitu alikua anavitamani sana ila alishindwa kuweka wazi labda kutokana na msimamo wa dini yake au labda maadili ya kazi yake.
Wakati huo nikiwa na fatemeh pia niligundua kuwa ni mtu aliyewahi kuishi maisha ya upweke ulipitiliza hapo kabla. Kwani kitendo cha kutokua na wazazi wala ndugu basi ni dhahiri aliishi maisha ya upweke sana kuanzia utoto wake mpaka anafikia utu uzima huo.

Ni wazi kampani yangu ilimfanya kujiona sasa ni mtu mwenye rafiki wa karibu lakini pia alijiona wa thamani kwa kuwa na mtu wa kubadilishana nae mawazo.

Licha ya hivyo katabia kangu ka kufosi kula tunda kalimfanya na yeye ajione mwanamke ambaye anavutia mbele ya wanaume. Kwani ilionekana wazi watu anaofanya nao kazi wasingeweza kumchombeza kwa namna yoyote ile.

MIMI: can I see your childhood memories like photos?
( Naweza kuona kumbukumbu zako za utotoni kama picha na vingine, niliongezea hapo kwamba anaonekana enzi za utoto wake alikua very cute girl)

FATEMEH: Even my self wish I could see them
( Hata Mimi pia natamani ningeziona)

Kwa majibu hayo nilijua kabisa ni wazi ata yeye hakuwahi kuona picha zake za utoto.

Lakini pia niliwaza inawezekana fatemeh akawa na story ngumu sana inayohusu maisha yake. Hapo niimuomba anipe at least nusu ya story ya maisha yake mpaka anafika umri huo.

Sura ya fatemeh iliongezeka upole na majonzi kwa wakati mmoja, alibeba msosi ambao ulikua tayari na mimi nilibeba msosi pia tukaelekea mezani sehemu ya dinning table.

Tukiwa dinning fatemeh aliuliza kuwa nataka kusikia story ya maisha yake kuanzia wapi. Kwani yeye mwenyewe haujui mwanzo wake zaidi anachokumbuka ni maisha yake kuanzia kituo cha nursery imam Ali.

Nyuma ya hapo hakuna anachokumbuka, yaani hajui alizaliwa wapi? Baba yake ni nani, mama yake ni nani wala hajui ndugu lakini pia hajui alifikaje kituoni hapo.

Mlezi wake wa kwanza aliyempokea kituoni hapo alikufa kwa kuwekewa sumu aina ya Botulinum inayotokana na bakteria wanaofahamika kama anaerobic.

Lakini kwa upande wake ana amini kuuwawa kwa mlezi huyo kulisababishwa na yeye mwenyewe yaani fatemeh ndio aliyepelekea kuuwawa kwa mlezi huyo.


Fatemeh aliligundua hilo baada ya uchunguzi wake binafsi alioufanya baada ya kuwa ametoka kwenye kituo hicho. Na ni kupitia uchunguzi huo ndio aligundua kutumika kwa sumu hiyo kwenye mauaji ya mlezi huyo.

Ni taasisi au idara ya MOIS ndio iliyomtoa fatemeh kwenye kituo hicho na kumpeleka kwenye kituo kingine baada ya kugundua uwezo wake mkubwa wa darasani.

Wakati tunaendelea na story zile ilionekana wazi kama fatemeh hakuwahi kuulizwa swali lolote kuhusu maisha yake hapo nyuma. Lakini pia niligundua kuna siri kubwa iliyopo nyuma ya maisha yake, na kuna uwezekano mkubwa kuwa siri hiyo inafichwa na either serikali ya Iran au ata yeye mwenyewe.

0623329512 ( Whatsapp) kama ukihitaji kusogea mbele zaidi kwa kutumia PDF ( BUKU TATU TU!)

bandari haijauzwa mama yupo kazini,

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
 
Shusha vitu bro.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…