Utajuaje kama Watu fulani wanaandamana, Tafsiri hasa ya neno Maandamano ni ipi?

Utajuaje kama Watu fulani wanaandamana, Tafsiri hasa ya neno Maandamano ni ipi?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Kwa Mjini kama Dar es Salaam na kwingineko si jambo la ajabu kukuta makundi ya watu mabarabarani wakitembea kuelekea huku na kule , wengine masokoni , wengine kwenye viwanja vya soka , wengine wakitafuta Bar nzuri za kunywea pombe zao baada ya uchovu wa hapa na pale , wako pia wengjne wanaokwenda Mahakamani kusikiliza kesi za ndugu zao , na wengine wakiwa na barua za utambulisho wa serikali za mitaa na hati za mali zao ili kuwawekea dhamana wapendwa wao.

Sasa watu wa namna hii nao huwa wako kwenye maandamano au wanatafsiriwa wako kwenye mwendo upi ? Maandamano ni nini hasa ? Je wakivaa sare za namna fulani ndio huitwa wanaandamana? Tandika Mwembe Yanga haipiti siku bila kuona akina mama wakiwa kwa umati wametinga Sare za Vijola kwenda kumsuta mtu ama kwenda kwenye ndoa ya mkeka au ya halali , huku kigoma cha Uruguay kikiongoza njia , Je watu kama hawa tutaita wanaandamana?

Ni nini hasa maana halisi ya Maandamano?
 
Nimekumbuka yule jamaa wa Uamsho kule zanzbar miaka flani alihotubia watu uwanjani Kisha akasema "baada ya kukaa hapa kwa muda mrefu Sasa Mimi na marafiki zangu tutaenda kunyoosha miguu kidogo maana tumechoka, hatuandamani, tunanyoosha miguu tu"... Mara kundi lote likaamka wakaanza kuzurula mtaani huku police wakitazama tu.
 
Kwa Mjini kama Dar es Salaam na kwingineko si jambo la ajabu kukuta makundi ya watu mabarabarani wakitembea kuelekea huku na kule , wengine masokoni , wengine kwenye viwanja vya soka , wengine wakitafuta Bar nzuri za kunywea pombe zao baada ya uchovu wa hapa na pale , wako pia wengjne wanaokwenda Mahakamani kusikiliza kesi za ndugu zao , na wengine wakiwa na barua za utambulisho wa serikali za mitaa na hati za mali zao ili kuwawekea dhamana wapendwa wao.

Sasa watu wa namna hii nao huwa wako kwenye maandamano au wanatafsiriwa wako kwenye mwendo upi ? Maandamano ni nini hasa ? Je wakivaa sare za namna fulani ndio huitwa wanaandamana? Tandika Mwembe Yanga haipiti siku bila kuona akina mama wakiwa kwa umati wametinga Sare za Vijola kwenda kumsuta mtu ama kwenda kwenye ndoa ya mkeka au ya halali , huku kigoma cha Uruguay kikiongoza njia , Je watu kama hawa tutaita wanaandamana?

Ni nini hasa maana halisi ya Maandamano?
IGP Sirro atakufundisha maana yake tarehe 5 Agosti ukijaribu kuweka miguu
 
Back
Top Bottom