Utakombaje mboga ukiwa unakula na mgeni?

PAZIA 3

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2018
Posts
1,102
Reaction score
1,919
Huwa unafanyaje ukiwa unakula na mgeni ila anapenda kula kwa kukomba mboga?
 
Unaleta sufuria la mboga mezani, kama kuna watoto unawaambia, kwa sauti ili mgeni mkomba mboga naye asikie "nyie watoto msikombe mboga, si mnaona ndani ya sufuria zimeisha"
hapo lazima ajue hata yeye anaambiwa.
 
Inategemea na utaratibu wako wa chakula Mkuu..kwani mnakula ile ya kijamaa kwamba mnachovya sehemu moja?
 
Acha uchoyo. Akombe ikiisha mtapata maarifa mengine
 
Mfano,unaishi sehemu umepanga,ila jirani yako akaanza kumtongoza mke wako
 
Mfano,unaishi sehemu umepanga,ila jirani yako akaanza kumtongoza mke wako
We jamaa hueleweki, unataka upewe uzoefu wa 'Mgeni anayekomba mboga? au unataka uzoefu wa 'Jirani anaye mkomba mkeo?'
 
Tatizo mnapenda kusoma vitu direct-we endelea kuchambua mada,mkomba mboga anaweza kuwa kweli mkomba mboga,lakn pia ikawa mtu wa rafu!!Sijui mnanielewa new GT?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…