Utalii wa ndani (Isimila-Iringa)

Utalii wa ndani (Isimila-Iringa)

Full 8

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2010
Posts
313
Reaction score
271
Nimepata wasaa wa kutembelea Isimila kujionea malikale. Ni sehemu nzuri ya kuvutia na si mbali toka mjini Iringa, gharama ni nafuu kabisa na mapokezi yanaridhisha sana. Napendekeza upate wasaa pia wa kufika Isimila. Tazama picha zifuatazo.
IMG_20180304_130922.jpg
IMG_20180304_130937.jpg
IMG_20180304_142215.jpg
IMG_20180304_143034.jpg
IMG_20180304_142222.jpg
 
Kuna mengi ya kujifunza pale binafsi nimesoma shule jiran na hapo yenye jina hilo miaka 17 iliyopita nikiwa kidato cha kwanza tulienda hapo
 
Soma zaidi hapa Isimila - Wikipedia, kamusi elezo huru

Isimila ni eneo la kihistoria lililopo mkoani Iringa nchini Tanzania, katika kijiji cha Ugwachanya kwenye kata ya Mseke kilichopo kilomita 20 kutoka Iringa mjini karibu na barabara kuu ya A 104 kuelekea Mbeya. Njia ya kuingia si rahisi kuikuta iko kabla ya kufika kwenye kijiji cha Tanagozi ukitoka Iringa na kuingia upande wa kushoto.

Eneo hili ni kivutio kimojawapo kinachoupamba mkoa wa Iringa.

Bonde la Isimila lilikaliwa na watu tangu Zama za Mawe za Kale. Ni katika eneo hili ndipo zana za mawe za kale na nguzo za asili za Isimila zilipogunduliwa hapo tangu mwaka 1951.

Pia ndani ya eneo hili mafuvu na mifupa mingi ilionekana kati yao ilipatikana mifupa ambayo ilifanana na twiga wa hivi sasa, ila tofauti ni kwamba, mifupa hiyo iliashiria kuwa twiga hao walikuwa na shingo fupi, ambapo pia kulikuwa na aina tofauti ya viboko.

Zana hizo zinasadikiwa kuwa zilikuwepo tangu miaka laki tatu hadi nne kabla ya Kristo. Miongoni mwa zana zilizopo katika korongo la Isimila, ambalo lina mikondo miwili, ni pamoja na mikuki iliyotumika kwa ajili ya kujihami na pia mawe ya kombeo kwa ajili ya uwindaji.

Pia vifaa kama nyundo zilizokuwa zikitumika kwa ajili ya kutengenezea zana nyingine na shoka zilizotumika kwa kazi ya kuvunja mifupa, nyembe na visu.

Marejeo
Viungo vya nje

 
Nimefika iringa Mara nyingi hebu elekeza vzr unafikaje hapo,
Unapanda magari yanayoenda Ifunda, nauli ni 1000/= tu, unashuka kituo cha Isimila utaona bango na mshale unakuelekeza yalipo makumbusho mkuu.
 
Soma zaidi hapa Isimila - Wikipedia, kamusi elezo huru

Isimila ni eneo la kihistoria lililopo mkoani Iringa nchini Tanzania, katika kijiji cha Ugwachanya kwenye kata ya Mseke kilichopo kilomita 20 kutoka Iringa mjini karibu na barabara kuu ya A 104 kuelekea Mbeya. Njia ya kuingia si rahisi kuikuta iko kabla ya kufika kwenye kijiji cha Tanagozi ukitoka Iringa na kuingia upande wa kushoto.

Eneo hili ni kivutio kimojawapo kinachoupamba mkoa wa Iringa.

Bonde la Isimila lilikaliwa na watu tangu Zama za Mawe za Kale. Ni katika eneo hili ndipo zana za mawe za kale na nguzo za asili za Isimila zilipogunduliwa hapo tangu mwaka 1951.

Pia ndani ya eneo hili mafuvu na mifupa mingi ilionekana kati yao ilipatikana mifupa ambayo ilifanana na twiga wa hivi sasa, ila tofauti ni kwamba, mifupa hiyo iliashiria kuwa twiga hao walikuwa na shingo fupi, ambapo pia kulikuwa na aina tofauti ya viboko.

Zana hizo zinasadikiwa kuwa zilikuwepo tangu miaka laki tatu hadi nne kabla ya Kristo. Miongoni mwa zana zilizopo katika korongo la Isimila, ambalo lina mikondo miwili, ni pamoja na mikuki iliyotumika kwa ajili ya kujihami na pia mawe ya kombeo kwa ajili ya uwindaji.

Pia vifaa kama nyundo zilizokuwa zikitumika kwa ajili ya kutengenezea zana nyingine na shoka zilizotumika kwa kazi ya kuvunja mifupa, nyembe na visu.

Marejeo
Viungo vya nje

Umeweka nondo za kutosha mkuu, Heko.
 
nilishawahi kupita hapo 1993
ni pazuri kujifunzia historia ya zama za mawe
 
Back
Top Bottom