Una binti yako wa miaka 17 ambaye anasumbuliwa na ugonjwa wa kuvimba tumbo kwa muda mrefu hata shule ikabidi aache, umehangaika naye hospitali mbalimbali hadi India mmefika lakini ikashindikana.
Siku moja binti alibaki peke yake nyumbani akaja jirani yako ambaye ana mke na watoto,baada ya kuona binti yuko peke yake akapata tamaa na kumbaka, mara baada ya kitendo hicho ukatoka upepo kupitia sehemu za siri za yule binti na tumbo lake likarudi katika hali ya kawaida.
Mliporudi mkashangaa kumkuta binti kwenye hali ile na baada ya kumuuliza akawaeleza kilichotokea, kama we ndio mzazi wa binti utachukua hatua gani?