The redemeer
JF-Expert Member
- Jan 28, 2025
- 1,497
- 2,681
.
Karibu binti na mwana wa mama Afrika.
Ili kumuelewa Mungu wa Biblia ni lazima kwanza kuielewa Biblia, chanzo na asili yake.
Wengi wananiuliza binafsi naamini nini kuhusu Biblia na mahusiano yake na Mungu.
Kwa wanaofuatilia post zangu, sijawahi sema Biblia na Quran si vitabu vya Mungu, Mnielewe hapo.
Kawaida post zangu huwa zina hoja mbili kuu kuhusu Biblia na Quran.
Hoja ya kwanza ni kuwa Biblia na Quran si vitabu vya Wazungu na waarabu bali ni maandiko ya waafrika weusi.
Kwa nini waliamua kutumia maandiko yetu ili kututawala.
Sababu kuu toka zama mtu mweusi ndiye anamjua Mungu na alikuwa na mahusiano naye kwa usahihi, hivyo hata akipoteza mahusiano naye huwa anamtafuta kwa bidii.
Huo ni udhaifu wa asili wa mtu mweusi, ndiyo maana, sehemu ambayo unaweza kumdhuru mtu mweusi na asilalamike ni katika jambo linalohusishwa Mungu.
Na kwa kujua hilo mkoloni Kawekeza sana katika dini ili kutugawa na kututawala kirahisi.
Kwa namna ileile ya kuigawa Afrika vipande vipande ili aitawale kirahisi, ndiyo anatumia dini kutugawa ili atutawale kirahisi.
Uliza wenye kujua, hati za mkataba wa Berlin wa kuigawa Afrika vipandevipande upo wapi kama si Vartican.
Kwa nini zimehifadhiwa huko, kaulize Polisi.
Ndiyo maana nikakwambia Quran na Biblia ni kitabu kimoja ila walikigawa na kukipanga vibaya, Ili unabii utimie.
Nyuma ya pazia upangaji mbovu ndiyo maana ya kubadili siku na nyakati.
Nyakati ni zama, Zenye umri wa kati ya miaka 2000 hadi 4000.
Siku ni hizi za kutoka na kuzama jua.
Uliza utofauti kati ya siku za kalenda ya kiislamu na kalenda hii tunayotumia ya kikatoliki.
Kubadili nyakati kuna athari za mzunguko wa zama na historia ya kimungu sababu Maandiko ni ramani ya matukio ya kidunia.
Katika hili wanaofuata kisahihi ili kujua matukio ni wanajimu, usiulize wanajuaje, baada ya matukio fulani yatafuata matukio fulani.
Hivyo wanajimu hawatumii uchawi kama tunavyodhani bali wanafuata mzunguko asili wa kalenda ya kimungu.
Biblia na Qurani ni kati ya kitabu cha kiutabiri( kinabii), kinachowezesha mtu kujua mzunguko wa matukio yake binafsi na matukio ya kidunia na dunia.
Kama Biblia ingepangwa vizuri tungejua hiki ni kizazi Cha ngapi na kinaisha lini kisha kitafuata kizazi gani na kitaisha lini.
Na kila kizazi kina tabia yake, na matukio yake.
Sambamba na kujua wewe ni nani katika hii dunia, utakubwa na matukio gani na kwa nini, mbali na kujua kila kitakachofuata toka kilichopo, itajua poa mwisho wako ni upi katika hii dunia.
Njia hiyo ndiyo walitumia manabii wa maandiko kujua vizazi, matukio, yaliyopita na yajayo, kutia ndani mwisho wa kila kitu, kutia ndani wao.
Ukiona kalenda ya kinajimu ina nyota 12 sawa na biblia ina nyota 12 sawa na makabila(vizazi) 12, sawa na kalenda hii ya kikatoliki ina miezi 12. Kwa wanaojua kuhesabu au kutamka namba kwa kilatini utaona hesabu za miezi zipo kinyume mfano Dechem (desemba ) sio 12 ni 9.
Kubadili siku kuna athari za kimaumbile, miili kushindwa kupokea, taarifa sahihi za kimungu, ikiwa ni pamoja na kufanya ibada fulani, Kutoa sadaka, kufanya mambo, nje ya siku za kimungu.
Ukumbuke siku zinatokana na mzunguko wa mwezi.
Kila hatua moja ya mwezi inaathari katika mwili wa viumbe hai wa dunia.
Kila mwezi unapokuwa na siku fulani kuna jambo inatakiwa ufanye ili kufanikiwa kimwili na kimaisha.
Fuatilia kwa nini mwezi fulani kuna hali fulani ambayo huleta magonjwa fulani.
Na hata hali ya afya ya Dunia huwa ina badirika, upepo, baridi nk.
Ukienda kinyume kuna madhara ya kiafya kutia ndani saikolojia, kwa maana utapoteza hata uwezo wa kufikilia.
Ukitaka uamini hili.
Jenga utaratibu wa kulala vizuri mchana alafu afya yako na mawazo yako, uoanishe na mtu anayelala usiku na kuamka mapema kama agizo la maandiko yanavyosema.
Mfano hai fuatilia afya na saikolojia ya wakristo, waislamu na wafanya kazi wenye utaratibu wa kulala mapema na kuamka kuanzia saa 11 mpaka saa 12 asubuhi.
Wanaofuata siku kisahihi ni Freemason, baadhi ya waislamu, baadhi ya wakristo bila kujua na wanajimu.
Baadhi ya Wakristo na waislamu wengi hawajui nguvu ya saa inapotakiwa kulia hadhana au kengere.
Mida ya hadhana na kengere imetegwa kwa sababu za kiroho na kisaikolojia.
Ndiyo maana adhana au kengere visiposikika ndani ya Muda aviruhusiwi kufanywa kabla au baadaye.
Hoja ya pili Ni kuwa, kile kinachomaanishwa katika Maandiko si maana ile tunayofundishwa.
Tunafundishwa mambo yanayosukuma akili zetu kuwa chini ya wengine, ili kuona mambo kwa namna anayoitaka mkoloni, ndiyo maana, Wakristo wa mapema hawakuruhusiwa kumiliki Biblia Wala kujaribu kutafakari.
Lengo wasitafakari nje ya mawazo ya wakoloni, na hata ukifanya hivyo peke yako, utafungwa na dhambi ya kukufuru.
Yaani kumtafakari Mungu vibaya, Hata ukiwa sahihi.
Siku za hivi karibuni kanisa Katoliki limeanza kuruhusu watu kutafakari lakini bado wamewekewa mipaka kwa kuweka kitabu cha namna ya kutafakari ambayo nayo haitoi haki ya kutafakari mwenyewe bali utafakari kwa kuoanisha na tafakari iliyowekwa.
Tuwe pamoja.
Karibu binti na mwana wa mama Afrika.
Ili kumuelewa Mungu wa Biblia ni lazima kwanza kuielewa Biblia, chanzo na asili yake.
Wengi wananiuliza binafsi naamini nini kuhusu Biblia na mahusiano yake na Mungu.
Kwa wanaofuatilia post zangu, sijawahi sema Biblia na Quran si vitabu vya Mungu, Mnielewe hapo.
Kawaida post zangu huwa zina hoja mbili kuu kuhusu Biblia na Quran.
Hoja ya kwanza ni kuwa Biblia na Quran si vitabu vya Wazungu na waarabu bali ni maandiko ya waafrika weusi.
Kwa nini waliamua kutumia maandiko yetu ili kututawala.
Sababu kuu toka zama mtu mweusi ndiye anamjua Mungu na alikuwa na mahusiano naye kwa usahihi, hivyo hata akipoteza mahusiano naye huwa anamtafuta kwa bidii.
Huo ni udhaifu wa asili wa mtu mweusi, ndiyo maana, sehemu ambayo unaweza kumdhuru mtu mweusi na asilalamike ni katika jambo linalohusishwa Mungu.
Na kwa kujua hilo mkoloni Kawekeza sana katika dini ili kutugawa na kututawala kirahisi.
Kwa namna ileile ya kuigawa Afrika vipande vipande ili aitawale kirahisi, ndiyo anatumia dini kutugawa ili atutawale kirahisi.
Uliza wenye kujua, hati za mkataba wa Berlin wa kuigawa Afrika vipandevipande upo wapi kama si Vartican.
Kwa nini zimehifadhiwa huko, kaulize Polisi.
Ndiyo maana nikakwambia Quran na Biblia ni kitabu kimoja ila walikigawa na kukipanga vibaya, Ili unabii utimie.
Nyuma ya pazia upangaji mbovu ndiyo maana ya kubadili siku na nyakati.
Nyakati ni zama, Zenye umri wa kati ya miaka 2000 hadi 4000.
Siku ni hizi za kutoka na kuzama jua.
Uliza utofauti kati ya siku za kalenda ya kiislamu na kalenda hii tunayotumia ya kikatoliki.
Kubadili nyakati kuna athari za mzunguko wa zama na historia ya kimungu sababu Maandiko ni ramani ya matukio ya kidunia.
Katika hili wanaofuata kisahihi ili kujua matukio ni wanajimu, usiulize wanajuaje, baada ya matukio fulani yatafuata matukio fulani.
Hivyo wanajimu hawatumii uchawi kama tunavyodhani bali wanafuata mzunguko asili wa kalenda ya kimungu.
Biblia na Qurani ni kati ya kitabu cha kiutabiri( kinabii), kinachowezesha mtu kujua mzunguko wa matukio yake binafsi na matukio ya kidunia na dunia.
Kama Biblia ingepangwa vizuri tungejua hiki ni kizazi Cha ngapi na kinaisha lini kisha kitafuata kizazi gani na kitaisha lini.
Na kila kizazi kina tabia yake, na matukio yake.
Sambamba na kujua wewe ni nani katika hii dunia, utakubwa na matukio gani na kwa nini, mbali na kujua kila kitakachofuata toka kilichopo, itajua poa mwisho wako ni upi katika hii dunia.
Njia hiyo ndiyo walitumia manabii wa maandiko kujua vizazi, matukio, yaliyopita na yajayo, kutia ndani mwisho wa kila kitu, kutia ndani wao.
Ukiona kalenda ya kinajimu ina nyota 12 sawa na biblia ina nyota 12 sawa na makabila(vizazi) 12, sawa na kalenda hii ya kikatoliki ina miezi 12. Kwa wanaojua kuhesabu au kutamka namba kwa kilatini utaona hesabu za miezi zipo kinyume mfano Dechem (desemba ) sio 12 ni 9.
Kubadili siku kuna athari za kimaumbile, miili kushindwa kupokea, taarifa sahihi za kimungu, ikiwa ni pamoja na kufanya ibada fulani, Kutoa sadaka, kufanya mambo, nje ya siku za kimungu.
Ukumbuke siku zinatokana na mzunguko wa mwezi.
Kila hatua moja ya mwezi inaathari katika mwili wa viumbe hai wa dunia.
Kila mwezi unapokuwa na siku fulani kuna jambo inatakiwa ufanye ili kufanikiwa kimwili na kimaisha.
Fuatilia kwa nini mwezi fulani kuna hali fulani ambayo huleta magonjwa fulani.
Na hata hali ya afya ya Dunia huwa ina badirika, upepo, baridi nk.
Ukienda kinyume kuna madhara ya kiafya kutia ndani saikolojia, kwa maana utapoteza hata uwezo wa kufikilia.
Ukitaka uamini hili.
Jenga utaratibu wa kulala vizuri mchana alafu afya yako na mawazo yako, uoanishe na mtu anayelala usiku na kuamka mapema kama agizo la maandiko yanavyosema.
Mfano hai fuatilia afya na saikolojia ya wakristo, waislamu na wafanya kazi wenye utaratibu wa kulala mapema na kuamka kuanzia saa 11 mpaka saa 12 asubuhi.
Wanaofuata siku kisahihi ni Freemason, baadhi ya waislamu, baadhi ya wakristo bila kujua na wanajimu.
Baadhi ya Wakristo na waislamu wengi hawajui nguvu ya saa inapotakiwa kulia hadhana au kengere.
Mida ya hadhana na kengere imetegwa kwa sababu za kiroho na kisaikolojia.
Ndiyo maana adhana au kengere visiposikika ndani ya Muda aviruhusiwi kufanywa kabla au baadaye.
Hoja ya pili Ni kuwa, kile kinachomaanishwa katika Maandiko si maana ile tunayofundishwa.
Tunafundishwa mambo yanayosukuma akili zetu kuwa chini ya wengine, ili kuona mambo kwa namna anayoitaka mkoloni, ndiyo maana, Wakristo wa mapema hawakuruhusiwa kumiliki Biblia Wala kujaribu kutafakari.
Lengo wasitafakari nje ya mawazo ya wakoloni, na hata ukifanya hivyo peke yako, utafungwa na dhambi ya kukufuru.
Yaani kumtafakari Mungu vibaya, Hata ukiwa sahihi.
Siku za hivi karibuni kanisa Katoliki limeanza kuruhusu watu kutafakari lakini bado wamewekewa mipaka kwa kuweka kitabu cha namna ya kutafakari ambayo nayo haitoi haki ya kutafakari mwenyewe bali utafakari kwa kuoanisha na tafakari iliyowekwa.
Tuwe pamoja.