the ultimatum
JF-Expert Member
- Dec 16, 2012
- 403
- 116
Wapendwa nawasalimu,
Naomba awali ya yote nieleweke kuwa sababu ya kuandika uzi huu siyo ya kuharibia kampuni ya M-BET kibiashara bali ni kueleza suala lililotokea kwangu na labda kwa wengine pia ambao ni watumiaji wa michezo ya kubahatisha ya mpira wa miguu kupitia kampuni ya M-BET.
Kitendo cha M-BET kupunguza ODDS za ticket iliyokwishachezwa ni cha kitapeli na hakina tafsiri nyingine. Ukiachilia mbali odds zilizokosea kwa mfano ikiwa Barcelona anacheza na Huesca halafu ukakuta Barcelona amepewa odds 13 na Huesca akapewa odds 1.15 hapo moja kwa moja kunamakosa ya kimaandishi ambayo hutokea kwani uwezo wa Barcelona ni mkubwa mno kimantiki alipaswa apewe odds za Huesca Na kinyume chake. Kwa hiyo hapo ni wazi kabisa odds placing zilikosewa kwa huyu kupewa za mwenzake na kinyume chake.
Lakini kuna swala pia lifahamike Odds zinatabia ya kuongezeka au kupungua kwa kadili muda unavyokwenda na hili huwa halihusishi odds zilizokosewa bali ni utaratibu wa kawaida wa kupungua na kupanda kwa odds kulingana na muda na sababu nyingine za kimichezo. Ifahamike kuwa mabadiliko yanayotokea katika muktadha huu hayazihusu tiketi zilizokwishachezwa.
Inapotokea tiketi imechezwa na ikapunguzwa odds zake baadae au kuongezwa huu ni utapeli wa kimichezo ambao unakatazwa kwamujibu wa sheria za michezo ya kubahatisha.
Ninachokizungumza hapa kimenitokea, mkeka huu nilioweka hapa nimeucheza siku mbili nyuma ulisoma takribani 2,300,000 za kitanzania lakini leo pesa imepungua kufikia 1,700,000 za kitanzania. Huu ni utapeli na haukubaliki. Naomba mamlaka za nchi zichunguze swala hili, haya makampuni yanatupiga sana wakati mwengine, na huwa tunatumia pesa nyingi sana haipendezi tunatumia pesa zetu lakinini tunafanyiwa uhuni. Lakini pia huu ni mtego mwingine wa kukwepa kodi au kulipa kodi pungufu kwa mujibu wa sheria. Kampuni ya M-BET nadhani na makampuni mengine yanatozwa kodi 20% ya tiketi zote zinazoshinda, kwa kupunguza kwa makusudi kiasi cha pesa kwenye tiketi ni kupunguza kodi kampuni iliyopaswa kulipwa kama tiketi ingeshinda.
NB: Team M-BET tuungane pamoja kupinga huu upuuzi
===============================================
Naomba awali ya yote nieleweke kuwa sababu ya kuandika uzi huu siyo ya kuharibia kampuni ya M-BET kibiashara bali ni kueleza suala lililotokea kwangu na labda kwa wengine pia ambao ni watumiaji wa michezo ya kubahatisha ya mpira wa miguu kupitia kampuni ya M-BET.
Kitendo cha M-BET kupunguza ODDS za ticket iliyokwishachezwa ni cha kitapeli na hakina tafsiri nyingine. Ukiachilia mbali odds zilizokosea kwa mfano ikiwa Barcelona anacheza na Huesca halafu ukakuta Barcelona amepewa odds 13 na Huesca akapewa odds 1.15 hapo moja kwa moja kunamakosa ya kimaandishi ambayo hutokea kwani uwezo wa Barcelona ni mkubwa mno kimantiki alipaswa apewe odds za Huesca Na kinyume chake. Kwa hiyo hapo ni wazi kabisa odds placing zilikosewa kwa huyu kupewa za mwenzake na kinyume chake.
Lakini kuna swala pia lifahamike Odds zinatabia ya kuongezeka au kupungua kwa kadili muda unavyokwenda na hili huwa halihusishi odds zilizokosewa bali ni utaratibu wa kawaida wa kupungua na kupanda kwa odds kulingana na muda na sababu nyingine za kimichezo. Ifahamike kuwa mabadiliko yanayotokea katika muktadha huu hayazihusu tiketi zilizokwishachezwa.
Inapotokea tiketi imechezwa na ikapunguzwa odds zake baadae au kuongezwa huu ni utapeli wa kimichezo ambao unakatazwa kwamujibu wa sheria za michezo ya kubahatisha.
Ninachokizungumza hapa kimenitokea, mkeka huu nilioweka hapa nimeucheza siku mbili nyuma ulisoma takribani 2,300,000 za kitanzania lakini leo pesa imepungua kufikia 1,700,000 za kitanzania. Huu ni utapeli na haukubaliki. Naomba mamlaka za nchi zichunguze swala hili, haya makampuni yanatupiga sana wakati mwengine, na huwa tunatumia pesa nyingi sana haipendezi tunatumia pesa zetu lakinini tunafanyiwa uhuni. Lakini pia huu ni mtego mwingine wa kukwepa kodi au kulipa kodi pungufu kwa mujibu wa sheria. Kampuni ya M-BET nadhani na makampuni mengine yanatozwa kodi 20% ya tiketi zote zinazoshinda, kwa kupunguza kwa makusudi kiasi cha pesa kwenye tiketi ni kupunguza kodi kampuni iliyopaswa kulipwa kama tiketi ingeshinda.
NB: Team M-BET tuungane pamoja kupinga huu upuuzi
===============================================
Nilizungumza nao kwa simu jana wakaniambia kwenye system yao pesa inaonyesha kama ilivyokuwa ya awali hivyo wamenihakikishia nitalipwa kama ilivyokuwa yaani 2,345,000 badala ya 1,700,000. Niliwakumbusha tu kuhusu mabadiliko ya odds kutozigusa tickets zilizolipwa tayari. Picha hii hapa wamenitumia wao kuonyesha kiasi kinachosoma kwenye system yao