Utapeli wa kupatiwa dawa jiji la arusha

LUMBAKALA

Senior Member
Joined
Dec 29, 2010
Posts
148
Reaction score
20
Kuna jamaa wamezuka jijini Arusha wakidai wao wanawapa dawa wananchi za kuongeza nguvu za kiume,kutibu kisukari,nk.Jamaa hawa wamediriki kusema eti hata fanta na cocacola haifai kwa matumizi ya binadamu,kwasababu eti ukienda pale Bonite huwezi kukuta magari yameleta machungwa kwa ajili ya kutengenezea fanta orange.Hivi kweli nchi hii serikali itakubali iwanyweshe wananchi wake vinywaji vyenye madhara kwa wananchi wake,serikali iwe macho kwa hawa madokta njaa,mi nawaita njaa sababu wanajiita madokta wakipotosha taaluma kubwa kama hii
 
hao watu imani yao ya dini inasimamia wapi!!isije kuwa wana masalia!
 

too much drinking of soda is harmful ukweli ndio huo utake usitake.....kwani ni kweli umeona magari ya matunda kiwandani..? mbona hajajibu hiyo hoja we unakimbilia kulaumu tuuu
 
Ndo maana mi deal na TBL tu.
 
haa haaaa, yaani wameona Fanta Orange wakajiimanisha inatengenezwa na machungwa, hizi ni flovoured beverages

pia hivi vinywaji sio vizuri sana kutumia mara kwa mara kwani vinatengezwa na sukari za labaratory au industrial sugar
 
Hao jamaa wako sahihi kabisa, SODA haifai na mimi nashuru mungu sasa ni miaka miwili tangia niachane na kitu Soda, Watalamu wanakuambia Soda ni mbaya kuliko hata Sigara ila najua watu watabisha,
 
Hivi kweli nchi hii serikali itakubali iwanyweshe wananchi wake vinywaji vyenye madhara kwa wananchi wake?
Hujawahi kusikia inagawa ARVs feki kwa waathirika? wanaume wanaota matiti mahips na wowowo la kufa mtu.
 
Hao jamaa wako sahihi kabisa, SODA haifai na mimi nashuru mungu sasa ni miaka miwili tangia niachane na kitu Soda, Watalamu wanakuambia Soda ni mbaya kuliko hata Sigara ila najua watu watabisha,

Uko sahihi mkuu hasa zile za Cola ni hatari sana zinaharibu mifupa, na pia zina tabia ya kuharibu digestion ndio maana ni hatari kuzitumia baada au wakati wa msosi! Ukimudu kunywa lita 4 ndani ya saa moja unakufa! Anayebisha aje nimuelezee ki-biologia kinachotokea ili afe!
 
SODA si nzuri kwa afya, hao wako sahihi katika hilo, hamna utapeli hapo. Cocacola ina vijiko visivyopungua 8 vya sukari, kiasi cha sukari ambacho hata kwenye chai huwezi weka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…