Ili mtu aweze kutuma maombi ya kujiunga na vyuo vya afya serikali katika ngazi ya cheti na stashahada anatakiwa kulipia sh 15,000/= ambazo hazirudishwi hata kama akikosa.Wakati nchi inakabiliwa na tatizo la wataalamu wa afya serikali yetu inazidi kuweka vikwazo vya kujiunga na vyuo vyake.Lakini mbona wizara nyingine za serikali hawana utaratibu huu ,mfano wizara ya elimu.Hii ni njia mojawapo ya kuwakandamiza watoto wa maskini kupata nafasi hizi na kuendeleza kukuza tatizo la upungufu wa wataalamu wa afya katika hosipitali za serikali.Kwangu mimi hiki siyo chanzo sahihi cha mapato ,serikali jraibuni kutengeneza vyanzo vingine vya mapato.