Utaratibu wa kuokoteza watumishi nje ya utumishi usitishwe ili kurejesha hadhi ya utumishi wa umma

Utaratibu wa kuokoteza watumishi nje ya utumishi usitishwe ili kurejesha hadhi ya utumishi wa umma

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad amesema watu wenye tabia ya kuunga mkono kila wakati ni wasaka fursa na hawana msaada wowote katika nchi.

Kipindi cha miaka mitano iliyopita tumeona tabia hii ya kusifia kila kitu ikikomaa na kufikia kiwango cha juu kabisa nchini. Hali hii ileletwa na utamaduni ambao haukwa mpya sana tofauti na awamu nyingine ila kwa kipindi hiki ulishika kasi zaidi. Utaratibu huo ni wa watu walio nje ya utumishi wa serikali au vyama vyao wengine wakiwa hawana sifa kabisa kuteuliwa katika nafasi za utumishi.

Matokeo yake tumekuwa na kundi kubwa la wasifiaji 'praise team' kuanzia kwa vijana wadogo kabisa wanaomaliza vyuo hadi wazee wanaotakiwa kucheza na wajukuu zao tu. Na hali ni kwa kila sekta nchini, iwe vyuoni, polisi, bungeni, makanisani, misikitini, vyombo vya habari hadi hapa JF!

Serikali mpya inatakiwa idhibiti hali hii ili taifa letu lisizidi kuwa la hovyo. Nafasi za juu na nyingine zozote katika utumishi wa umma zipatikane kwa watu kupanda madaraja katika taaluma, sekta na idara zao husika. Serikali na vyama vya siasa visitishe utaratibu wa kuokoteza watu kokote waliko na kuwapa majukumu ya kiutumishi. Nafasi za kiutumishi zipatikane kwa kupanda ngazi. Watumishi wapande ngazi kuanzia ya chini kabisa.
 
Utawala ndiyo unapenda kuweka watu wao bila kujali unyeti wa kazi wanazowapatia. Unawezaje kumchukua ndugu yako au mtia Mia wa Chama tu na ukampa cheo cha DED au RAS bila kujali hata kama umemtoa mtaani hajui hata ABCs za Utumishi wa Umma.

In fact hata katika Chama wanatakiwa ku lobby wapate kutoka kwa Watumishi wa Umma wenye uzoefu mnawaachisha kazi au wanapostaafu mnawatumia.

Chadema niliwahi kumpata mama mstaafu aliyekuwa Katibu Mkuu na aliwasaidia sana kuweka mambo sawa. Ujingaujinga wa kusema mwenzetu ndiyo unetufikisha hapa tulipo
 
Ili kuthibitisha kauli yako, kaangalie kwenye ripoti ya CAG 2019-2020. Zile halmashauri 53 zilizopata hati zisizoridhisha na 8 zilizopata adverse opinion 95% zinaongozwa na Wakurugenzi kutoka PRAISE team.

Hawa ni wale walioingizwa kwenye utumishi wa umma kutokea 'mtaani'.
 
Ukitaka kuamini Magufuli alikuwa Mshenzi aliwateua Hassan Ngoma na Hudson Kamoga kuwa ma DED na DAS just because walikuwa wanamsifu kwenye kile kipindi chao cha Clouds.

Magu alikuwa mshenzi sana Kwa kweli!
 
Kama wataendeleza huu utaratibu wa kuchukua watu wowote popote na kuwapa nafasi za juu za utumishi wa umma miaka mitano ijayo tutakwa zaidi ya banana republic.
Ili kuthibitisha kauli yako, kaangalie kwenye ripoti ya CAG 2019-2020. Zile halmashauri 53 zilizopata hati zisizoridhisha na 8 zilizopata adverse opinion 95% zinaongozwa na Wakurugenzi kutoka PRAISE team.
Hawa ni wale walioingizwa kwenye utumishi wa umma kutokea 'mtaani'.
 
Kwa sababu ni wateuliwa na hawakuchaguliwa na wananchi ndio maana inawabidi kuwa watu wa kujipendekeza sana ili wadumu vitini mwao.
Eti DC au RC analazimisha watumishi kuwa na ilani ya CCM.Pia mtumishi analazimishwa kusema CCM oyeeeee! Vitu vya kijinga kabisa!
 
Ati?
.... Wanaokotezwa wa majalalani na sio watu makini wanaovutia jicho la uteuzi!

... Nani kasema sisi tuliojiajiri tuko majalalani hadi tuokotezwe?

Mleta mada tengua kauli yako inayovunja hata maadili tuliyojiwekea jf!
🤮 🤮 🤮 💥
 
Hua wanaendaga kupata mafunzo ya utumishi wa Umma au wanaendesha nchi kama kituo cha mafuta? Yale mafundisho hayana maana tena.
 
Utumishi wa umma umenajisiwa sana awamu hizi. Fikiria Niki wa Pili anaenda kwenye baraza la madiwani kama mheshimiwa. Nchi inaendeshwa kama group la wasap.
 
Back
Top Bottom