JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 685
- 1,124
Utaratibu wa Kupiga Kura
(i) Mpiga Kura atatakiwa kwenda na Kadi yake ya kupigia Kura Kituoni na kumpa Msimamizi Msaidizi Na. 1 wa Kituo;
(ii) Msimamizi Msaidizi Na. 1 wa Kituo atasoma kwa sauti jina la Mpiga Kura ili kuwawezesha Mawakala kuangalia taarifa za Mpiga Kura huyo katika Daftari la Kituo;
(iii) Msimamizi Msaidizi Na. 1 wa Kituo ana haki ya kumuuliza Mpiga Kura swali lolote linalohusiana na utambulisho wake iwapo ana shaka naye;
(iv) Msimamizi wa Kituo kabla ya kumkabidhi Mpiga Kura Karatasi za Kura atagonga Muhuri wa Kituo;
(v) Msimamizi wa Kituo atampatia Mpiga Kura Karatasi ya Kupigia Kura na kumuelekeza namna ya kuikunja Karatasi hiyo baada ya Kupiga Kura;
(vi) Mpiga Kura atatakiwa kwenda katika Kituturi na Kupiga Kura yake kwa siri;
(vii) Mpiga Kura atatakiwa kuweka alama ya vema (√) katika eneo la Mgombea ambaye anamtaka katika Karatasi ya Kupigia Kura;
(viii) Mara baada ya Kupiga Kura, Mpiga Kura atazikunja/ataikunja Karatasi yake ya Kura na kuitumbukiza katika Sanduku la Kura lililowekwa katika eneo la wazi la Kituo; na
(ix) Kabla Mpiga Kura hajaondoka Kituoni anatakiwa kupakwa Wino Maalum na Msimamizi Msaidizi Na. 2 wa Kituo katika Kidole Kidogo cha Mwisho cha Mkono wa Kushoto
Kuharibika kwa Kura
Karatasi ya Kura haitahesabiwa kuwa Kura Halali iwapo Kura hiyo:-
(i) Haina Muhuri wa Kituo;
(ii) Imepigwa kwa Mgombea zaidi ya mmoja;
(iii) Ina alama, au maandishi yanayoweza kumtambulisha mtu aliyepiga Kura;
(iv) Haina alama yoyote; na
(v) Amepigiwa Mgombea aliyejitoa.
(i) Mpiga Kura atatakiwa kwenda na Kadi yake ya kupigia Kura Kituoni na kumpa Msimamizi Msaidizi Na. 1 wa Kituo;
(ii) Msimamizi Msaidizi Na. 1 wa Kituo atasoma kwa sauti jina la Mpiga Kura ili kuwawezesha Mawakala kuangalia taarifa za Mpiga Kura huyo katika Daftari la Kituo;
(iii) Msimamizi Msaidizi Na. 1 wa Kituo ana haki ya kumuuliza Mpiga Kura swali lolote linalohusiana na utambulisho wake iwapo ana shaka naye;
(iv) Msimamizi wa Kituo kabla ya kumkabidhi Mpiga Kura Karatasi za Kura atagonga Muhuri wa Kituo;
(v) Msimamizi wa Kituo atampatia Mpiga Kura Karatasi ya Kupigia Kura na kumuelekeza namna ya kuikunja Karatasi hiyo baada ya Kupiga Kura;
(vi) Mpiga Kura atatakiwa kwenda katika Kituturi na Kupiga Kura yake kwa siri;
(vii) Mpiga Kura atatakiwa kuweka alama ya vema (√) katika eneo la Mgombea ambaye anamtaka katika Karatasi ya Kupigia Kura;
(viii) Mara baada ya Kupiga Kura, Mpiga Kura atazikunja/ataikunja Karatasi yake ya Kura na kuitumbukiza katika Sanduku la Kura lililowekwa katika eneo la wazi la Kituo; na
(ix) Kabla Mpiga Kura hajaondoka Kituoni anatakiwa kupakwa Wino Maalum na Msimamizi Msaidizi Na. 2 wa Kituo katika Kidole Kidogo cha Mwisho cha Mkono wa Kushoto
Kuharibika kwa Kura
Karatasi ya Kura haitahesabiwa kuwa Kura Halali iwapo Kura hiyo:-
(i) Haina Muhuri wa Kituo;
(ii) Imepigwa kwa Mgombea zaidi ya mmoja;
(iii) Ina alama, au maandishi yanayoweza kumtambulisha mtu aliyepiga Kura;
(iv) Haina alama yoyote; na
(v) Amepigiwa Mgombea aliyejitoa.
Upvote
0