Uchaguzi 2020 Utaratibu wa muda wa kufunguliwa na kufungwa kwa kituo cha kupigia kura

Uchaguzi 2020 Utaratibu wa muda wa kufunguliwa na kufungwa kwa kituo cha kupigia kura

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
Infographic Instagram.png

Kwa mujibu wa kifungu cha 68 na 69 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 na kifungu cha 69 na 70 cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292, kituo cha kupigia kura kitafunguliwa saa moja kamili (1:00) asubuhi na kufungwa saa kumi kamili (10:00) jioni

Itakapofika saa 10:00 jioni:
(i) Endapo kutakuwa na wapiga kura kwenye mstari muda huo, mlinzi wa kituo atasimama nyuma ya mpiga kura wa mwisho ili mpiga kura mwingine yeyote aliyechelewa asiweze kuja na kupanga foleni mara baada ya muda wa kufunga kituo kufika. Wapiga kura walio kwenye mstari waruhusiwe kupiga kura hadi watakapokamilisha upigaji kura

(ii) Wapiga kura watakaofika kwenye kituo cha kupigia kura baada ya saa kumi kamili (10:00) jioni watakuwa wamechelewa na hawataruhusiwa kupiga kura
 
Upvote 0
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom