Utaratibu wa timu kuanzia round ya awali halafu zingine zinasubiri round ya pili ni wa hovyoo sana

Utaratibu wa timu kuanzia round ya awali halafu zingine zinasubiri round ya pili ni wa hovyoo sana

CAF wana mambo mengi mno ya kizamani, kama hayo kila siku timu fulani kuanzia ugenenini ni ushamba, Away goal ni ushamba, mambo ya huyu anaanza hatua ya awali huyu ya mbele ni ushamba na ushamba ukubwa zaidi wa kutumia ubora wa miaka 7 nyuma kupima timu kwa wakati wa sasa, kwa mambo haya ndio maana ni ndoto kwa africa kubeba Wedi Cap
 
Nadhani CAF inatakiwa kufanya review katika baadhi ya mambo yake . Hii ni taswira ya kibaguzi. Pia na suala la timu kubwa kuanzia ugenini nao huu ni utaratibu wa hovyoo sana.
Kabla ya kulaumu kwanza ulipaswa kujua kwanini inatokea timu zingine kuanzia raundi ya pili.

Tatizo lipo kwa aina ya wanachama wa CAF, CAF ina wanachama zaidi ya 50 lakini wanachama wengi ni kapuku hawana uwezo kiuchumi na CAF wameweka mfumo wa wazi kuwa kila mwanachama anaweza kushiriki katika mashindano ya CAF ngazi ya vilabu kama unaona timu zako zinaweza kumudu gharama za mashindano.

Sasa nini kinachopelekea timu zingine zianzie hatua inayofuata?

Mashindano ya CAF ngazi ya vilabu wameweka mfumo wa knock out stage kwanzia hatua ya awali ambapo zinatakiwa zikichezwa mechi zibakie timu 32 zitakazocheza raundi ya pili. Idadi ya timu zinazotakiwa kushiriki hatua ya awali ni timu 64 lakini kutokana na changamoto za kiuchumi, kuna baadhi ya wanachama wa CAF hawatoi wawakilishi kwenye mashindano hivyo hupelekea timu kuwa pungufu ya 64.
Na ukiangalia ushiriki wa vilabu kila msimu hubadilika na hupelekea kubadilika badilika kwa idadi ya timu zinazoanzia hatua ya pili.

Mfano msimu uliopita wa 2023/2024 ni wanachama 42 pekee ndio walitoa wawakilishi kwenye klabu bingwa. Katika wanachama 42, wanachama 12 hutoa timu mbili klabu bingwa hivyo wanachama 30 watatoa timu moja moja hivyo inafanya kuwe na timu 54 zilizoshiriki klabu bingwa. Hapo unaona kuna upungufu wa timu 10 ili kufikia idadi ya timu 64, hapo sasa ndipo unapopata idadi ya timu inayopaswa kuanzia hatua ya pili. Ile idadi inayopelea kufika 64 ndio idadi ya timu inayopelekea kuanzia raundi ya pili, lengo ni kufanya timu ziwe 32 kwenye raundi ya pili. Msimu uliopita timu 10 zilianzia raundi ya pili, na msimu huu timu zilizoshiriki klabu bingwa ni timu 59 kutoka kwa wanachama 47 wa CAF. Ukiangalia hapo kwenye 59 kuna pengo la timu 5 kufika timu 64 na ndio maana unaona msimu huu timu 5 zikapaswa zianzie raundi ya pili. Siku ikitokea wanachama 52 wametoa wawakilishi, hautoona timu yeyote ile itakayoanzia raundi ya pili.
 
CAF wana mambo mengi mno ya kizamani, kama hayo kila siku timu fulani kuanzia ugenenini ni ushamba, Away goal ni ushamba, mambo ya huyu anaanza hatua ya awali huyu ya mbele ni ushamba na ushamba ukubwa zaidi wa kutumia ubora wa miaka 7 nyuma kupima timu kwa wakati wa sasa, kwa mambo haya ndio maana ni ndoto kwa africa kubeba Wedi Cap
Yaani pale CAF ni sawa na TifuaTifua ya Karai tu.
 
Kabla ya kulaumu kwanza ulipaswa kujua kwanini inatokea timu zingine kuanzia raundi ya pili.

Tatizo lipo kwa aina ya wanachama wa CAF, CAF ina wanachama zaidi ya 50 lakini wanachama wengi ni kapuku hawana uwezo kiuchumi na CAF wameweka mfumo wa wazi kuwa kila mwanachama anaweza kushiriki katika mashindano ya CAF ngazi ya vilabu kama unaona timu zako zinaweza kumudu gharama za mashindano.

Sasa nini kinachopelekea timu zingine zianzie hatua inayofuata?

Mashindano ya CAF ngazi ya vilabu wameweka mfumo wa knock out stage kwanzia hatua ya awali ambapo zinatakiwa zikichezwa mechi zibakie timu 32 zitakazocheza raundi ya pili. Idadi ya timu zinazotakiwa kushiriki hatua ya aeali ni timu 64 lakini kutokana na changamoto za kiuchumi, kuna baadhi ya wanachama wa CAF hawatoi wawakilishi kwenye mashindano hivyo hupelekea timu kuwa pungufu ya 64.
Na ukiangalia ushiriki wa vilabu kila msimu hubadilika na hupelekea kubadilika badilika kwa idadi ya timu zinaanzia hatua ya pili.

Mfano msimu uliopita wa 2023/2024 ni wanachama 42 pekee ndio walitoa wawakilishi kwenye klabu bingwa. Katika wanachama 42, wanachama 12 hutoa timu mbili klabu bingwa hivyo wanachama 30 watatoa timu moja moja hivyo inafanya kuwe na timu 54 zilizoshiriki klabu bingwa. Hapo unaona kuna upungufu wa timu 10 ili kufikia idadi ya timu 64, hapo sasa ndipo unapopata idadi ya timu inayopaswa kuanzia hatua ya pili. Ile idadi inayopelea kufika 64 ndio idadi ya timu inapelekwa kuanzia raundi ya pili, lengo ni kufanya timu ziwe 32 kwenye raundi ya pili. Msimu uliopita timu 10 zilianzia raundi ya pili, na msimu huu timu zilizoshiriki klabu bingwa ni timu 59 kutoka kwa wanachama 47 wa CAF. Ukiangalia hapo kwenye 59 kuna pengo la timu 5 kufika timu 64 na ndio maana unaona msimu huu timu 5 zikapaswa zianzie raundi ya pili. Siku ikitokea wanachama 52 wametoa wawakilishi, hautoona timu yeyote ile itakayoanzia raundi ya pili.
Hahah. Natumaini hii post yako ni joke unamkejeli mleta mada. Sitaki kuamini upo siriasi
 
CAF wana mambo mengi mno ya kizamani, kama hayo kila siku timu fulani kuanzia ugenenini ni ushamba, Away goal ni ushamba, mambo ya huyu anaanza hatua ya awali huyu ya mbele ni ushamba na ushamba ukubwa zaidi wa kutumia ubora wa miaka 7 nyuma kupima timu kwa wakati wa sasa, kwa mambo haya ndio maana ni ndoto kwa africa kubeba Wedi Cap

Kwenye swala la away goal nakubaliana na wewe, na inawezekana tunaishangaa Africa kwenye hili kwasasa kwavile ulaya wameshafuta.

Kwenye kubagua timu kuanza hatua ya awali na nyingine hatua ya pili nimelitolea ufafanuzi juu kwanini inatokea hilo.

Kutumia ubora wa miaka 7 sio kweli, bali hutumika misimu mitano, na hilo sio swala la Africa peke yake kama ni mfuatiliaji wa UEFA champions league utaona kuwa hata UEFA wanafanya kitu hicho hicho labda kwavile watu mnashindwa kujua kwavile tu kule hawa post post ranking kama CAF lakini mfumo wa ranking ipo sawasawa na hiyo ranking ndio inayofanya seeding kwenye draw ( kutengeneza pots na kujua yupi apate favour ya kuanzia ugenini)


IMG_20240819_123540.jpg
 
Unakua shabiki wa mpira afu hata haujui unashabikia nini. Mkuu jaribu kushabikia vitu vingine, mpira umeshafeli.
 
Nadhani CAF inatakiwa kufanya review katika baadhi ya mambo yake . Hii ni taswira ya kibaguzi. Pia na suala la timu kubwa kuanzia ugenini nao huu ni utaratibu wa hovyoo sana.
Mimi naona wapo sahihi.... Japo ni Shabiki wa Yanga.
 
Duh! Kweli kazi ipo
Kama hauna hoja sio lazima u comment, unakosoa kuwa sipo siriazi na nilichoandika halafu usemi ni kipi ambacho sio sahihi katika kilichoandikwa. Humu ni sehemu ya maarifa watu kujifunza na kueleweshana. Wewe bado upo kwenye hali kama ya utoto fulani hivi. Kosoa hoja sio mipasho na dhihaka, uwezi kaa kimya wachie wanaojua kufanya mijadala kisomi.
 
Back
Top Bottom