Venus Star
JF-Expert Member
- Dec 6, 2018
- 26,519
- 78,311
Utaratibu wa usafi wa Mazingira nao uwekwe kwenye katiba?
Nimekuwa nikitatizika sana na usafi wa mitaa yetu. Hakuna jitihada zozote zinazoongelewa kuhusu usafi wa mazingira yetu.
Inasikitisha sana kwamba tupo na ngazi za uongozi kutoka kwenye mitaa lakini hakuna utashi wa kuhimiza watu kusafisha mazingira.
Mitaa yote Dar es salaam haisafishwi kila wakati inatoa harufu mbaya. Utakuta Mwenyekiti wa mtaa yupo hawezi hata kuhimiza vijana wakachimbua hiyo mitaro na kusafisha mazingira.
Mfano: Dodoma maeneo ya Airport sehemu ambayo inamkusanyiko mkubwa wa watu Chako ni Chako mitaro inatoa harufu mbaya miezi yote 12.
Sababu za kutokea kwa jambo hilo
Hakuna political will Hapa naongelea utashi wa kisiasa. Hakuna viongozi wenye utashi wa kisiasa maana hakuna mwongozo wa kuwaelekeza kuhamasisha watu kufanya usafi. Matokeo yake imekuwa ni tabia na watu wanaona hilo ni jambo la kawaida. Lazima kuwepo na miongozo kikatiba itakayoweka misingi ya usafi wa mazingira. Hii itasababisha viongozi wa kisiasa waweze kuhimiza usafi wa mazingira.
Viongozi wa serikali za mitaa hawana ToR. Wanafanya kazi kwa kijitolea
Viongozi wa mitaa hakuna maelezo wala guidance iliyopo kuhusu usafi wa mazingira. Kwahiyo kunakuwa na ombwe la kutekeleza majukumu.
Hakuna taasisi inayohusika na usafi wa mazingira bali kunataasisi inayohusika na udhibiti
Tunakuwa tunakibilia katika kudhiti badala ya kuwa na taasisi ya kutatua changamoto. Mfano: National Environment Management Council (NEMC) Wamekuwa ni wadhiti tu badala ya wao kuwa watatuzi wa changamoto.
Mgongano wa Taasisi kiutendaji
Hapa kuna taasisi utitiri zinazojihusisha na mazingira. Kunakuwa hakuna mmoja nayekuwa responsible na usafi wa mazingira.
Utatuzi
Lazima katiba mpya iweke misingi ya usafi wa mwili na mazingira kwa kila raia wa Tanzania.
Katiba iweke takwa kwa viongozi kuhimiza usafi wa mazingira.
Mwenye maelezo mengine namkaribisha.
Nimekuwa nikitatizika sana na usafi wa mitaa yetu. Hakuna jitihada zozote zinazoongelewa kuhusu usafi wa mazingira yetu.
Inasikitisha sana kwamba tupo na ngazi za uongozi kutoka kwenye mitaa lakini hakuna utashi wa kuhimiza watu kusafisha mazingira.
Mitaa yote Dar es salaam haisafishwi kila wakati inatoa harufu mbaya. Utakuta Mwenyekiti wa mtaa yupo hawezi hata kuhimiza vijana wakachimbua hiyo mitaro na kusafisha mazingira.
Mfano: Dodoma maeneo ya Airport sehemu ambayo inamkusanyiko mkubwa wa watu Chako ni Chako mitaro inatoa harufu mbaya miezi yote 12.
Sababu za kutokea kwa jambo hilo
Hakuna political will Hapa naongelea utashi wa kisiasa. Hakuna viongozi wenye utashi wa kisiasa maana hakuna mwongozo wa kuwaelekeza kuhamasisha watu kufanya usafi. Matokeo yake imekuwa ni tabia na watu wanaona hilo ni jambo la kawaida. Lazima kuwepo na miongozo kikatiba itakayoweka misingi ya usafi wa mazingira. Hii itasababisha viongozi wa kisiasa waweze kuhimiza usafi wa mazingira.
Viongozi wa serikali za mitaa hawana ToR. Wanafanya kazi kwa kijitolea
Viongozi wa mitaa hakuna maelezo wala guidance iliyopo kuhusu usafi wa mazingira. Kwahiyo kunakuwa na ombwe la kutekeleza majukumu.
Hakuna taasisi inayohusika na usafi wa mazingira bali kunataasisi inayohusika na udhibiti
Tunakuwa tunakibilia katika kudhiti badala ya kuwa na taasisi ya kutatua changamoto. Mfano: National Environment Management Council (NEMC) Wamekuwa ni wadhiti tu badala ya wao kuwa watatuzi wa changamoto.
Mgongano wa Taasisi kiutendaji
Hapa kuna taasisi utitiri zinazojihusisha na mazingira. Kunakuwa hakuna mmoja nayekuwa responsible na usafi wa mazingira.
Utatuzi
Lazima katiba mpya iweke misingi ya usafi wa mwili na mazingira kwa kila raia wa Tanzania.
Katiba iweke takwa kwa viongozi kuhimiza usafi wa mazingira.
Mwenye maelezo mengine namkaribisha.