KERO Utaratibu wa uzoaji Taka Jiji la Mbeya ni shida, zimezagaa mitaani licha ya Wananchi kulipa ili zizolewe

KERO Utaratibu wa uzoaji Taka Jiji la Mbeya ni shida, zimezagaa mitaani licha ya Wananchi kulipa ili zizolewe

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mwanongwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2023
Posts
611
Reaction score
567
DSC_0324.JPG
Hili Jiji la Mbeya sasa kila kona ya Mtaa limegeuka kuwa kama Dampo maana siyo kwa kutapakaa kwa takataka kiasi kingi, licha ya kutokea kwa ugonjwa wa Kipindupindu katika baadhi ya kata hivi karibuni lakini suala la usafi limebaki kitendawili.

Halmashauri ya Jiji hawa watu wenu wa Suma JKT wamefeli hili zoezi la kuzoa taka maana inavyoonekana Wanamagari machache, hivyo kusababisha kushindwa kupita karibia kila mtaa kwa wakati.

Ukipita mitaa ya Mwanjelwa, Soweto, Mwambene, Kabwe, Isanga, Uyole na mingine mingi utaona namna taka zilivyotapakaa mitaani.

Pamoja na hivyo, ukipita kwenye yale maeneo wanayoishi viongozi kila siku gari zinakwenda na kuzoa taka lakini huku kwetu Wakina ‘Uswazi’ gari linapita kwa wiki mara moja au mara mbili.

Mbaya zaidi wananchi wanaamua kwenda kuzirundika taka hizo pembezoni mwa Barabara na wengine wanazitupa kwenye mitaro ya maji.

Licha ya gari kusumbua kubeba taka hizo lakini wale ndugu zetu wa kukusanya fedha za taka wao kila mwezi lazima wafike na kudai fedha.

Utaratibu wa fedha ya taka ni kila mlango ni Shilingi 2,000, yaani kama nyumba moja ina wapangaji saba, basi kila mpangaji anatakiwa kutoa kiasi hicho.

Kwa wafanyabiashara wa maduka, wao wanatakiwa kutoa shilingi 5,000 kila mwezi, Lodge yenye bar na restaurant inatakiwa kulipa kiasi cha Shilingi 20,000/=, Lodge peke yake inalipa kiasi cha Shilingi 10,000/=.
DSC_0343.JPG

DSC_0360.JPG
Pesa zote hizo wanakusanya lakini ukiliona Jiji lilivyotapakaa uchafu unabaki unajiuliza hili Jiji lina Mkurugenzi kweli? Kama yupo ina maana haoni au anaona kisha anapuuzia hali hii?

Inafika kipindi huwa najiuliza ni vigezo gani walitumia mpaka waliamua kuipa Mbeya hadhi ya kuwa Jiji kama vitu vidogo tu hivi vya kukusanya taka vinawashinda.

Hali ni mbaya sana maeneo ya Kabwe Stand maana kuna takataka zinarundikwa pale na maeneo ya karibu na biashara za vyakula zinaendelea.

Nakumbusha Mamlaka zinazohusika zisiishie kuwafungia hao Mama Lishe na Baba Lishe pamoja na hivyo visima vya maji, bali maadamu mnakusanya pesa zetu za taka basi kumbukeni kuzoa hizo taka.
DSC_0355.JPG

DSC_0310.JPG

DSC_0221.JPG

Pia soma:
~
Mbeya: Wazazi tutoe elimu ya chakula kwa Watoto wetu kuanzia nyumbani ili iwe tahadhari ya kujilinda na Kipindipindu
~ Wagonjwa wa Kipindupindu wafikia 22 Mbeya, na Serikali imepiga kimya!
 

Attachments

  • DSC_0221.JPG
    DSC_0221.JPG
    1.1 MB · Views: 2
Halmashauri ya jiji la mbeya na watu wa mipango miji hata sielewagi wanafanyaga kazi gani.Jiji liko rafu kila sekta kuanzia mpangilio wa makazi ,mauchafu kuzagaa barabarani na mitaani ..yaani very local kwakweli.
 
Hili Jiji la Mbeya sasa kila kona ya Mtaa limegeuka Dampo maana siyo kwa kutapakaa kwa takataka kiasi kingi, licha ya kutokea kwa ugonjwa wa Kipindupindu katika baadhi ya kata lakini suala la usafi limebaki kitendawili.

Mpaka kuna muda unajiuliza hivi hapa ndipo panaongozwa na Kiongozi wa Juu Serikalini?

Halmashauri ya Jiji hawa watu wenu wa Suma JKT wamefeli hili zoezi la kuzoa taka maana inavyoonekana Wanamagari machache, hivyo kusababisha kushindwa kupita karibia kila mtaa kwa wakati.

Ukipita mitaa ya Mwanjelwa, Soweto, Mwambene, Kabwe, Isanga, Uyole na mingine mingi utaona namna taka zilivyotapakaa mitaani.

Ila ukipita kwenye yale maeneo wanayoishi viongozi kila siku gari zinakwenda na kuzoa taka lakini huku kwetu Wakina ‘uswazi’ gari linapita kwa wiki mara moja au mara mbili.

Mbaya zaidi wananchi wanaamua kwenda kuzirundika taka hizo pembezoni mwa Barabara na wengine wanazitupa kwenye mitaro ya maji.

Licha ya gari kusumbua kubeba taka hizo lakini wale ndugu zetu wa kukusanya fedha za taka wao kila mwezi lazima wafike na kudai fedha.

Utaratibu wa fedha ya taka ni kila mlango ni Shilingi 2,000, yaani kama nyumba moja ina wapangaji saba, basi kila mpangaji anatakiwa kutoa kiasi hicho.

Kwa wafanyabiashara wa maduka, wao wanatakiwa kutoa shilingi 5,000 kila mwezi, Lodge yenye bar na restaurant inatakiwa kulipa kiasi cha Shilingi 20,000/=, Lodge peke yake inalipa kiasi cha Shilingi 10,000/=.

Pesa zote hizo wanakusanya lakini ukiliona Jiji lilivyotapakaa uchafu unabaki unajiuliza hili Jiji lina Mkurugenzi kweli? Kama yupo ina maana haoni au anaona kisha anapuuzia hali hii?

Inafika kipindi huwa najiuliza ni vigezo gani walitumia mpaka waliamua kuipa Mbeya hadhi ya kuwa Jiji kama vitu vidogo tu hivi vya kukusanya taka vinawashinda.

Hali ni mbaya sana maeneo ya Kabwe Stand maana kuna takataka zinarundikwa pale na maeneo ya karibu na biashara za vyakula zinaendelea.

Nakumbusha Mamlaka zinazohusika zisiishie kuwafungia hao Mama Lishe na Baba Lishe pamoja na hivyo visima vya maji, bali maadamu mnakusanya pesa zetu za taka basi kumbukeni kuzoa hizo taka.
Mbeya na tunduma nishida kwa uchafu
 
Nimeishi mbeya kwa miaka mitatu, na ulichokiandika ni kweli kbsaa.
Na mbeya pia inaongoza kua na vijana wadogo wadogo wengi Sana Ambao kazi yao hua ni kupita kwenye kaya za watu kwa ajiri ya kuzoa taka kwa Bei nafuu na kuzipeleka kusiko julikana mwisho wa siku tunakutana nazo zimesambaa ovyo tu. Na mbeya ni eneo ambalo mvua ikinyesha maji hua Yana tiririka Sana kitu ambachoni hatar Sana kwa afya zao, nadhani ndio sababu iliopelekea kutokea kwa kipindu pindu huko mbeya hivi karibuni.
 
Halmashauri ya jiji la mbeya na watu wa mipango miji hata sielewagi wanafanyaga kazi gani.Jiji liko rafu kila sekta kuanzia mpangilio wa makazi ,mauchafu kuzagaa barabarani na mitaani ..yaani very local kwakweli.
Ni hatari
 
Nimeishi mbeya kwa miaka mitatu, na ulichokiandika ni kweli kbsaa.
Na mbeya pia inaongoza kua na vijana wadogo wadogo wengi Sana Ambao kazi yao hua ni kupita kwenye kaya za watu kwa ajiri ya kuzoa taka kwa Bei nafuu na kuzipeleka kusiko julikana mwisho wa siku tunakutana nazo zimesambaa ovyo tu. Na mbeya ni eneo ambalo mvua ikinyesha maji hua Yana tiririka Sana kitu ambachoni hatar Sana kwa afya zao, nadhani ndio sababu iliopelekea kutokea kwa kipindu pindu huko mbeya hivi karibuni.
Yes ni kweli
 
Halmashauri ya jiji la mbeya na watu wa mipango miji hata sielewagi wanafanyaga kazi gani.Jiji liko rafu kila sekta kuanzia mpangilio wa makazi ,mauchafu kuzagaa barabarani na mitaani ..yaani very local kwakweli.
Hili Jiji ni chafu sana
 
Back
Top Bottom