Utata Ocean Road Cancer Institute, mnavyofanya si sawa

Utata Ocean Road Cancer Institute, mnavyofanya si sawa

moonlightj12

Member
Joined
Dec 6, 2022
Posts
33
Reaction score
90
Wasalam wakuu, nimepata changamoto kidogo kwenye hii taasisi

Mzee wangu anasumbuliwa na Cancer alifanyiwa operation wakatoa uvimbe, then tukapewa referral kwenda Ocean Road Cancer Institute tulipofika tulipokelewa tukapewa utaratibu.

Tukaambiwa tulipie shilingi milioni tatu na laki sita kwa ajili ya dawa ambayo Mzee anatakiwa apewe, tukiwa tunajikanyaga tufanyaje kuna Mzee tulikuwa naye akatueleza kuna msamaha.

Tukafuatilia huo msamaha tukalipia shilingi milioni moja na laki sita, tukapewa maelekezo ya vyakula Mzee ambavyo hatakiwi kula na muda ambao tunatakiwa kurudi hospitali hapo.

Stori linaanza hapa, sasa tarehe ya kurudi Mzee imefika hawapigi simu, ikabidi tujichange tutafute nauli aende hukohuko Jijini Dar es Salaam.

Jamani unaweza lia basi tu hawa watu hawajui utafutaji wetu ulivyo wa shida, wanamwambia Mzee tulifanya mistake mara tuli-misplace risiti, mara kuna deni kubwa South Africa vitu ambavo personally nimeshindwa kuvielewa.

Hilo ni tisa, kumi wamemwambia kuna watu mbele yake ambao wameshaagiziwa hizo dawa, kwa hiyo yeye asubiri tena miezi miwili mbele, watampigia simu.

Kuna vyakula alikatazwa saizi wamemruhusu eti hadi watakapomgia simu watamwelekeza tena na upya.

Nyie watu mlioko huko maisha yetu ni magumu sana na hiyo hela mliipa 'limitations' ilipwe kwa wakati lakini saivi mnatuzungusha Mzee wangu anatoka mbali hadi kufika Dar anachoka sana.

Mungu anawaona lakini...

=============

Updates...

mafta.jpg

Dkt. Tausi Maftah

UFAFANUZI KUTOKA HOSPITALI YA OCEAN ROAD
Daktari Bingwa wa Mionzi ya Nyuklia, Dkt. Tausi Maftah wa Ocean Road anafafanua kuhusu malalamiko ya Mdau huyo:

Nianze kwa kueleza historia kwa ufupi, matibabu ya mionzi ya Nuklia huwa yanategemea na aina ya Saratani ya mgonjwa.

Msambazaji mkubwa wa dawa zetu za Mionzi ya Nyuklia yupo Afrika Kusini, mwingine ambaye tunamtumia kama akiba pale inapobidi yuko Ulaya.

Tunapofanya kazi na Msambazaji wetu wa Afrika Kusini ni rahisi kwa kuwa tunawasiliana naye kwa ukaribu na hata inapotokea kuna mabadiliko ya ‘oda’ za dawa ni rahisi kufanya maadiliko tofauti na yule wa Ulaya.

Pia itambulike kuwa Dawa tunazoagiza kutoka Afrika Kusini zina gharama kubwa na Serikali inachangia kwa asilimia kubwa kuwezesha zinafika Tanzania.

Mbali na hapo dawa zinazoagizwa kwa ajili ya Wagonjwa wa Saratani kutoka Afrika Kusini huwa zinakuja kwa oda maalum, mbali na hapo kitaalam dawa hizo huwa zina muda wake maalum (time limit), muda ukizidi hapo inaharibika na haziwezi kufaa kwa matumizi.

Hivyo, ni jambo gumu kuweka oda kisha ije na umpatie mgonjwa mwingine au usimpe mhusika, haiwezekani kuiweka tu.

Hata huyo Mdau aliyelalamika ni wazi anajua taratibu zote zinazofanyika ndio maana kaelezea kwenye maelezi yake, labda inawezekana hakuwa na subira ya kusubiri dawa, changamoto kama hiyo huwa inatokea mara kadhaaa kwa baadhi ya Wagonjwa kushindwa kuwa na subira wakati wa kusubiri dawa.

Aidha, kabla ya Dawa kutufikia (Tanzania) huwa zinatengenezwa kulingana na oda za wenye uhitaji, hatuwezi kuagiza dawa ambazo hazipo kwenye oda kwa kuwa zitakuja na kuharibika huku.

Hapo kati zikishatoka Afrika Kusini kunakuwa na michakato mingine kadhaa ikiwemo ukaguzi wa TMDA.

Hata wao TMDA waliwahi kutushauri tuagize dawa za miezi sita tukawajulisha hilo haliwezekani kwa kuwa dawa zinaagizwa kwa od ana zinakuja kwa wagonjwa maalum, pia time limit inatubana.

Tunachokifanya wakati mgonjwa anapokuwa anasubiri oda ya dawa zake kwenye mifumo yetu kunakuwa na maelekezo yote muhumu kuhusu yeye na anajulishwa kabisa kuwa Dawa yake inatarajiwa kufika lini, anapangiwa ratiba yake ya matumizi ya chakula na taratibu nyingine.

Uagizaji wa Dawa unaweza kuchukua wiki mbili hadi mwezi, huwa inategemea na oda ya dawa zilizoagizwa.

Wagonjwa wetu sisi ni rafiki zetu kwa kuwa huduma wanayopata hapa si ile ya kundikiwa dawa na kutakiwa kwenda, bali wanapewa maelekezo na tunawapa muda wa kuwasikiliza.

Kuna dawati la malalamiko na wapo huru kutoa malalamiko yao, wapo huru, hivyo changamoto zipo lakini ni suala la kueleweshana tu.
 
Pole sana Mkuu, kwa mtu anayeijua Cancer anaelewa changamoto mnayokutana nayo.
 
Kumbe watu wanapaswa kuwa na subira tu na kufata maelekezo ya madaktari mana hata hiyo mionzi ya nyuklia yenyewe kumbe kuagiza kwake ni tabu, asanteni madaktari wa Ocean Road kwa ufafanuzi
 
Wasalam wakuu, nimepata changamoto kidogo kwenye hii taasisi

Mzee wangu anasumbuliwa na Cancer alifanyiwa operation wakatoa uvimbe, then tukapewa referral kwenda Ocean Road Cancer Institute tulipofika tulipokelewa tukapewa utaratibu.

Tukaambiwa tulipie shilingi milioni tatu na laki sita kwa ajili ya dawa ambayo Mzee anatakiwa apewe, tukiwa tunajikanyaga tufanyaje kuna Mzee tulikuwa naye akatueleza kuna msamaha.

Tukafuatilia huo msamaha tukalipia shilingi milioni moja na laki sita, tukapewa maelekezo ya vyakula Mzee ambavyo hatakiwi kula na muda ambao tunatakiwa kurudi hospitali hapo.

Stori linaanza hapa, sasa tarehe ya kurudi Mzee imefika hawapigi simu, ikabidi tujichange tutafute nauli aende hukohuko Jijini Dar es Salaam.

Jamani unaweza lia basi tu hawa watu hawajui utafutaji wetu ulivyo wa shida, wanamwambia Mzee tulifanya mistake mara tuli-misplace risiti, mara kuna deni kubwa South Africa vitu ambavo personally nimeshindwa kuvielewa.

Hilo ni tisa, kumi wamemwambia kuna watu mbele yake ambao wameshaagiziwa hizo dawa, kwa hiyo yeye asubiri tena miezi miwili mbele, watampigia simu.

Kuna vyakula alikatazwa saizi wamemruhusu eti hadi watakapomgia simu watamwelekeza tena na upya.

Nyie watu mlioko huko maisha yetu ni magumu sana na hiyo hela mliipa 'limitations' ilipwe kwa wakati lakini saivi mnatuzungusha Mzee wangu anatoka mbali hadi kufika Dar anachoka sana.

Mungu anawaona lakini...

=============

Updates...

View attachment 2727402
Dkt. Tausi Maftah

UFAFANUZI KUTOKA HOSPITALI YA OCEAN ROAD
Daktari Bingwa wa Mionzi ya Nyuklia, Dkt. Tausi Maftah wa Ocean Road anafafanua kuhusu malalamiko ya Mdau huyo:

Nianze kwa kueleza historia kwa ufupi, matibabu ya mionzi ya Nuklia huwa yanategemea na aina ya Saratani ya mgonjwa.

Msambazaji mkubwa wa dawa zetu za Mionzi ya Nyuklia yupo Afrika Kusini, mwingine ambaye tunamtumia kama akiba pale inapobidi yuko Ulaya.

Tunapofanya kazi na Msambazaji wetu wa Afrika Kusini ni rahisi kwa kuwa tunawasiliana naye kwa ukaribu na hata inapotokea kuna mabadiliko ya ‘oda’ za dawa ni rahisi kufanya maadiliko tofauti na yule wa Ulaya.

Pia itambulike kuwa Dawa tunazoagiza kutoka Afrika Kusini zina gharama kubwa na Serikali inachangia kwa asilimia kubwa kuwezesha zinafika Tanzania.

Mbali na hapo dawa zinazoagizwa kwa ajili ya Wagonjwa wa Saratani kutoka Afrika Kusini huwa zinakuja kwa oda maalum, mbali na hapo kitaalam dawa hizo huwa zina muda wake maalum (time limit), muda ukizidi hapo inaharibika na haziwezi kufaa kwa matumizi.

Hivyo, ni jambo gumu kuweka oda kisha ije na umpatie mgonjwa mwingine au usimpe mhusika, haiwezekani kuiweka tu.

Hata huyo Mdau aliyelalamika ni wazi anajua taratibu zote zinazofanyika ndio maana kaelezea kwenye maelezi yake, labda inawezekana hakuwa na subira ya kusubiri dawa, changamoto kama hiyo huwa inatokea mara kadhaaa kwa baadhi ya Wagonjwa kushindwa kuwa na subira wakati wa kusubiri dawa.

Aidha, kabla ya Dawa kutufikia (Tanzania) huwa zinatengenezwa kulingana na oda za wenye uhitaji, hatuwezi kuagiza dawa ambazo hazipo kwenye oda kwa kuwa zitakuja na kuharibika huku.

Hapo kati zikishatoka Afrika Kusini kunakuwa na michakato mingine kadhaa ikiwemo ukaguzi wa TMDA.

Hata wao TMDA waliwahi kutushauri tuagize dawa za miezi sita tukawajulisha hilo haliwezekani kwa kuwa dawa zinaagizwa kwa od ana zinakuja kwa wagonjwa maalum, pia time limit inatubana.

Tunachokifanya wakati mgonjwa anapokuwa anasubiri oda ya dawa zake kwenye mifumo yetu kunakuwa na maelekezo yote muhumu kuhusu yeye na anajulishwa kabisa kuwa Dawa yake inatarajiwa kufika lini, anapangiwa ratiba yake ya matumizi ya chakula na taratibu nyingine.

Uagizaji wa Dawa unaweza kuchukua wiki mbili hadi mwezi, huwa inategemea na oda ya dawa zilizoagizwa.

Wagonjwa wetu sisi ni rafiki zetu kwa kuwa huduma wanayopata hapa si ile ya kundikiwa dawa na kutakiwa kwenda, bali wanapewa maelekezo na tunawapa muda wa kuwasikiliza.

Kuna dawati la malalamiko na wapo huru kutoa malalamiko yao, wapo huru, hivyo changamoto zipo lakini ni suala la kueleweshana tu.
Ocean Road Hoapital badilikeni (Reform).

Maelezo yako yanaonesha kuna gap kubwa sana ya uzembe katika kutowa huduma zenu.

Au ndiyo mnawasukumia wagonjwa waende "private" hospital zenu kama alivyokuwa akifanya Dokta Ngoma?

Nendeni na wakati, Reform. Kuweni "professionals ", msitowe maelezo na sababu ya kutokufanya. Huko ni kujaribu kuhalalisha dhambi zenu.

Resilience: Chukulieni matatizo haya kuwa ni fursa ya kuonesha kuwa mnaweza bila kusimamiwa mgongoni.
 
MLET SIASA ZA KULAUMU UONGOZI MJINGA. Maelezo ya Daktari ni kichekesho tena taarabu ya hovyo kabisa. Yaani huko South Africa wanatengeneza dawa kwa oda moja moja kama makange ya bar? Seriously? Sijawahi sikia duniani upuuzi kama huu. Hapo pamezidi RUSHWA. Hebu mleta mada pitia TAKUKURU wakupe hela zao upeleke. Hata procurement unit ya Ocean Road ni rushwa tupu. Nimefanya nao kazi mara moja ni kichefu chefu. 2017 nilikua na mgonjwa hapo. Huduma zilikua bure. Leo mgonjwa tena Mzee mnaleta blah blah ? DAKTARI ULIYOJIBU UGORO ULAANIWE.
 
Dkt. Tausi. kidogo umeeleweka.

Nashauri Oda mfanye kwa kipindi kifupi japo cha wiki moja.

Yaani mnakusanya mahitaji ya matibabu ya wagonjwa kwa wiki moja halafu mnatuma oda huko Afrika ya kusini. Kwa wiki wiki.

Hii itafanya mgonjwa apate matibabu kwa kipindi kisichopungua wiki tatu.

Tatizo mgonjwa anaacha taarifa za matibabu yake leo wanasubiri zaidi ya mwezi kupata matibabu.

Hamwoni kuwa kwa wagonjwa wenye kipato duni na wanaoishi mbali na Hospitali watapata usumbufu mwingi ?

Naomba Serikali uwe karibu na Hospitali ya Ocean Road. Walipa kodi tuko radhi kodi zetu zitumike hapo haraka sana.

Wagonjwa wake wanahitaji matibabu ya haraka sana la sivyo wanapoteza maisha.

Sasa hivi kuna Utaalamu wa Medical System.

Mgonjwa anafika hospital.
Mala tu anapo andikiwa dawa zake za oda, na oda inafika muda huohuo kwa (mtengenezaji-dawa) popote alipo.

Huyo Mkaguzi-dawa, aajiriwe na apewe ofisi hapo hapo Ocean Road ili kuokoa muda wa uhakiki. Dawa inakuja leo na anaikagua leo leo hakuna kupoteza muda.

Mwenyezi Mungu awape wepesi wa kusaidia waliopata ugonjwa huu hatari kwa maisha yetu.
Awape moyo wa huruma na uvumilivu.

Ee Mwenyezi Mungu Tusaidie.[emoji120][emoji120][emoji120]
 
Dkt. Tausi. kidogo umeeleweka.

Nashauri Oda mfanye kwa kipindi kifupi japo cha wiki moja.

Yaani mnakusanya mahitaji ya matibabu ya wagonjwa kwa wiki moja halafu mnatuma oda huko Afrika ya kusini. Kwa wiki wiki.

Hii itafanya mgonjwa apate matibabu kwa kipindi kisichopungua wiki tatu.

Tatizo mgonjwa anaacha taarifa za matibabu yake leo wanasubiri zaidi ya mwezi kupata matibabu.

Hamwoni kuwa kwa wagonjwa wenye kipato duni na wanaoishi mbali na Hospitali watapata usumbufu mwingi ?

Naomba Serikali uwe karibu na Hospitali ya Ocean Road. Walipa kodi tuko radhi kodi zetu zitumike hapo haraka sana.

Wagonjwa wake wanahitaji matibabu ya haraka sana la sivyo wanapoteza maisha.

Sasa hivi kuna Utaalamu wa Medical System.

Mgonjwa anafika hospital.
Mala tu anapo andikiwa dawa zake za oda, na oda inafika muda huohuo kwa (mtengenezaji-dawa) popote alipo.

Huyo Mkaguzi-dawa, aajiriwe na apewe ofisi hapo hapo Ocean Road ili kuokoa muda wa uhakiki. Dawa inakuja leo na anaikagua leo leo hakuna kupoteza muda.

Mwenyezi Mungu awape wepesi wa kusaidia waliopata ugonjwa huu hatari kwa maisha yetu.
Awape moyo wa huruma na uvumilivu.

Ee Mwenyezi Mungu Tusaidie.[emoji120][emoji120][emoji120]
Umeongea kwa busara sana haya ndo tunahitaji kuyasikia sio watu wengine huko juu wanabwabwaja hovyo hata hawajui kinachoendeleq mi nashauri tuendelee kuwasikiliza madaktari wanavyosema kuna changamoto inawezekana wagonjwa nao ni wengi sana mana hata sisi tulikuwa na wagonjwa pale tukafatilia wagonjwa waliotutangulia ni wengi sana zaidi ya Mia nne wote wanasubiri huduma sasa watawezaje? inabidi wengine tusubiri hawa wa mwanzo waliopita na wala hatukulalamika ila kuna watu wanataka kujifanya wao ndo wana priority sanaaaa na waliowakuta hawana mana upuuzi tu uewajaa na ubinafsi, Asante kwa andiko lako nimelielewa sana ndg yangu, mungu wajaalie madaktari wa Ocean Road watuhudumie kwa ufanisi
 
Ocean Road Hoapital badilikeni (Reform).

Maelezo yako yanaonesha kuna gap kubwa sana ya uzembe katika kutowa huduma zenu.

Au ndiyo mnawasukumia wagonjwa waende "private" hospital zenu kama alivyokuwa akifanya Dokta Ngoma?

Nendeni na wakati, Reform. Kuweni "professionals ", msitowe maelezo na sababu ya kutokufanya. Huko ni kujaribu kuhalalisha dhambi zenu.

Resilience: Chukulieni matatizo haya kuwa ni fursa ya kuonesha kuwa mnaweza bila kusimamiwa mgongoni.
Faiza umevurugwa.
Wewe kila mahali unakopita ni lawama tu.
 
Back
Top Bottom