Utata uliopo Mashariki mwa DRC

Utata uliopo Mashariki mwa DRC

Daby

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2014
Posts
33,894
Reaction score
76,810
Historia Inaonyesha Wanyamlenge/ wanyarwanda wameishi Mashariki mwa DRC kuanzia karne ya 19. Wengi walipelekwa na serikali ya kibelgiji na baadae wengi walihamia miaka ya 60-65.

1971 serikali ya Mobutu iliwapa uraia japo wananchi wengi wa Congo walilipinga hili. Hii tension ilisababishwa na wao kushiriki katika operation Simba. Iliyomtoa Lumumba madarakani.

Kitendo cha wananchi kukataa baadhi ya watutsi kupewa uraia kilisababisha iwe political agenda ya wanasiasa wa Kivu...baadhi ya watutsi walivuka mipaka kuiunga mkono RPF(kikundi cha watutsi kilichofanikiwa kuitoa serikali ya kihutu madarakani) chini ya Kagame.

Mauaji ya 1990s ya Burundi na Rwanda yalipelekea wakimbizi wa Kihutu kukimbilia Congo walipo Wanyamlenge (tutsi wa Congo) tayari hii ni tension.

Hawa wahutu waliunda vikundi kulipiza kisasi kwa Watutsi...moja ya kundi mashuhuri ni FDLR.

Kumbuka Mobutu aliiunga mkono serikali ya kihutu Rwanda. Miaka hiyo hiyo Laurent Kabila anasaidiana na Rwanda na Uganda chini ya ADFLC anaingia Congo kupitia mashariki walipo M23 na anafanikiwa kuichukua nchi.

Laurent Kabila akabadili jina la Zaire na kuwa DRC kama ilivyokuwa awali. Tension ikaongezeka kati ya watutsi wa Congo na wahutu(kumbuka pia Congo kuna wahutu asilia) waliohamia kukimbia mauaji ya kimbari.

Kagame na Museven walipoingia Congo kipindi cha kumsaidia Kabila hawakutoka ...lengo likiwa wavimalize vikundi vyote vya kihutu vinavyoitishia Rwanda. Hili lilileta taharuki saana....wacongo waliunda vikundi vya kujikinga na jeshi la Rwanda...mwaka 1998 kama sijakosea yakatokea mauaji ya wakongo zaidi ya 1000...Kasika massacre.

Kabila anayafukuza majeshi ya Rwanda na Uganda. Rwanda ilikataa kwendaa wakaanzisha vikundi kama RCD kutetea maslahi ya Watutsi.

Mwaka 2001 Kabila anauliwa , Kabila JR anachukua nchi.... Kabila Jr alifanikiwa kukaa chini na vikundi vya waasi akiwemo Laurent Nkunda na CNDP makubaliano yakiwa viwe vyama vya kisiasa na vijana waingizwe ndani ya jeshi.

Mwaka 2004 Laurent Nkunda akaungana na RCP kuwalinda Banyamlenge baada ya kulalamika kutokuridhika na serikali ya Kabila.

Mwaka 2009 March 23, waka kaa tena na serikali ya Kabila Jr. Baada ya kukamatwa kwa Nkunda na CNDP ikawa Chama cha siasa na waasi wakaingizwa jeshini. Wananchi wengi hawakupendezwa na hili. Likawa tena suala la kisiasa ...wanasiasa wakalitumia....mwaka 2012 vita ikaanza tena....kwa jina la M23

2013 zaidi ya nchi 10 za Africa zikasaini mkataba wa amani waasi wakakimbilia Uganda.

Mwaka 2021 wakarudi na kiongozi mwingine mpya...chokochoko zikaanza....Tshekedi akakimbilia EAC...baadae akawafukuza walinda amani wa EAC akaenda SADC.....

Tshekedi ni kabila moja na Laurent Kabila. Kabila Jr vyanzo vingi vinadai mama ni mtutsi na huenda sio mtoto halisi wa Kabila Sr.

Mgogoro unahistoria kubwa saana.....
 
Wakati ADF chini ya Kabila senior inamwondoa Mobutu aliungwa mkono na Rwanda. Na kwa namna hii....

Kama hawatazuiwa tutegemee Tshekedi ambaye ni kabila moja na Kabila kutimuliwa Kisha Rwanda wanaweka Kibaraka chao....kibaraka nacho kikibadilikia madarakani wanamleta mwingine.
 
Wakati ADF chini ya Kabila senior inamwondoa Mobutu aliungwa mkono na Rwanda. Na kwa namna hii....

Kama hawatazuiwa tutegemee Tshekedi ambaye ni kabila moja na Kabila kutimuliwa Kisha Rwanda wanaweka Kibaraka chao....kibaraka nacho kikibadilikia madarakani wanamleta mwingine.
Kwa Tshesekedi hawatofanikiwa.
 
Wakati ADF chini ya Kabila senior inamwondoa Mobutu aliungwa mkono na Rwanda. Na kwa namna hii....

Kama hawatazuiwa tutegemee Tshekedi ambaye ni kabila moja na Kabila kutimuliwa Kisha Rwanda wanaweka Kibaraka chao....kibaraka nacho kikibadilikia madarakani wanamleta mwingine.
Tayari wamaye kibaraka alikuwa mkurugenzi wa tume ya uchaguzi, ndiye aliyemtangaza tisheshekedi mshindi zidi ya mzee wa Tp Mazembe.

Ndio anajiita kipngozi wa Afdna M23 lengo ni kinshasa.
 
Tayari wamaye kibaraka alikuwa mkurugenzi wa tume ya uchaguzi, ndiye aliyemtangaza tisheshekedi mshindi zidi ya mzee wa Tp Mazembe.

Ndio anajiita kipngozi wa Afdna M23 lengo ni kinshasa.
Historia inaenda kujirudia tena....
 
Tayari wamaye kibaraka alikuwa mkurugenzi wa tume ya uchaguzi, ndiye aliyemtangaza tisheshekedi mshindi zidi ya mzee wa Tp Mazembe.

Ndio anajiita kipngozi wa Afdna M23 lengo ni kinshasa.
Huyu jamaa ni kabila gani? Anavinasaba vyovyote vya kitutsi?
 
Imeenda, Burundi na DRC wameingiza majeshi huko Goma. Sasa kama Kaingia mrundi na wasiwasi na Tanzania ataingia.
Hii vita haituhusu hata kidogo....

First Congo war hatukushiriki
Second war of Congo hatukushirki
Viongozi wetu wasije wakatuingiza.....kikumbwa walinde mipaka.

Rwanda kafunga GPS jamming mipakani.....
 
Hii vita haituhusu hata kidogo....

First Congo war hatukushiriki
Second war of Congo hatukushirki
Viongozi wetu wasije wakatuingiza.....kikumbwa walinde mipaka.

Rwanda kafunga GPS jamming mipakani.....
Tanzania mgogoro unaohusu Burundi lazima aingie, na sijui Huwa ni Kwa nini. Raisi wa Burundi anasema kama KAGAME atafanikiwa huko DRC basi atakaefuata ni yeye. na Jeshi la Burundi limejengwa kwa 80% na Tanzania. Ngoja tuone itakuaje, Warundi wote watazama huko Goma. kisha Wabongo wataenda kulinda mipaka ya Burundi. Hili naamini litatokea kwa zaidi ya 90%.
 
Tanzania mgogoro unaohusu Burundi lazima aingie, na sijui Huwa ni Kwa nini. Raisi wa Burundi anasema kama KAGAME atafanikiwa huko DRC basi atakaefuata ni yeye. na Jeshi la Burundi limejengwa kwa 80% na Tanzania. Ngoja tuone itakuaje, Warundi wote watazama huko Goma. kisha Wabongo wataenda kulinda mipaka ya Burundi. Hili naamini litatokea kwa zaidi ya 90%.
Kwamba na sisi kuna nchi tunailinda kwa hali na mali?? Kwa maslahi gani mkuu sisi sote si ni nchi choka mbaya.?
 
Kwamba na sisi kuna nchi tunailinda kwa hali na mali?? Kwa maslahi gani mkuu sisi sote si ni nchi choka mbaya.?
Tanzania inajenga reli SGR kuelekea Congo kupitia Burundi (Uvinza-Gitega).Kwa namna yoyote lazima tumtumie Burundi kufanya kazi na Congo.
Tanzania_SGR_plans.jpg
 
Tanzania inajenga reli SGR kuelekea Congo kupitia Burundi (Uvinza-Gitega).Kwa namna yoyote lazima tumtumie Burundi kufanya kazi na Congo.
View attachment 3221864
Anhaa kumbe na sisi tunalinda maslahi yetu, kwa wachangiaji huko juu inaonekana ni ishu ya muda kidogo, hii reli si ni juzi tu, huko nyuma tulikua na maslahi gani na Burundi??
 
H
Tanzania mgogoro unaohusu Burundi lazima aingie, na sijui Huwa ni Kwa nini. Raisi wa Burundi anasema kama KAGAME atafanikiwa huko DRC basi atakaefuata ni yeye. na Jeshi la Burundi limejengwa kwa 80% na Tanzania. Ngoja tuone itakuaje, Warundi wote watazama huko Goma. kisha Wabongo wataenda kulinda mipaka ya Burundi. Hili naamini litatokea kwa zaidi ya 90%.
Hii inaelekea kuwa vita ya kikanda sasa faida ya mataifa haya kuyaingiza EAC ni nini. Bora tungebaki nchi 3 hata federation ingewahi. sasa hivi limekuwa kokoro nchi zote ambazo ni security risk tukaziingiza hii hatari. ukweli kwa sasa baadhi hazina sifa tena ya kuwa kwenye EAC kwa mujibu wa Mkataba wa EAC.
 
Back
Top Bottom